Mabibi na mabwana moja kwa moja kwenye mada.
Siyo siri tena zama zimebadilika na matukio yanakwenda kwa kasi sana. Taifa letu likipita katika kipindi kigumu ambapo kwa bahati mbaya kumezuka hata makundi katika jamii ambayo yamelenga kupiga makelele tu yakijaribu kulazimisha kuufanya uongo kuonekana kuwa ukweli au ukweli kuwa uongo. Mithili ya kujidanganya mchana kuwa ni usiku au usiku kuwa ni mchana.
Mifano iko mingi mno na katika nyanja nyingi.
Ikumbukwe kuwa ukweli ni ukweli na uongo ni uongo na utabakia kuwa hivyo bila ya kujali nani kasema nini au nani atasema nini.
Ukweli mchungu hulka mpya hii haikuwahi kushuhudiwa katika awamu yoyote ya uongozi kabla ya awamu ya hii.
Hivi karibuni tumeondokewa na mzee wetu rais mstaafu mzee Mkapa (rip). Pamoja na sisi kushiriki sana katika shughuli zote za wenzetu, ni Burundi peke yake ndiyo walioweza kutuma ujumbe wao rasmi kuja kutuhani kwenye msiba huu mkubwa kutoka nyumbani kwao.
Si Malawi tulikokwenda kwenye kuapishwa kwa rais Chakwera. Si Zimbabwe tulikokwenda kumhani raisi wao Mugabe (rip). Si Afrika kusini tulikokwenda kumhani Mandela (rip) wala Winnie (rip). Wote hawa, hawakutuma wawakilishi wao rasmi tokea makwao kuja msibani sisi yalipotukuta.
Si Kenya tulikotuma ujumbe wetu mzito kabisa wakiwamo marais Kikwete na Mkapa (rip) kwa pamoja kuwahani kwenye msiba wa rais Moi (rip), kuwa walikuja kutuhani sisi yalipotusibu miezi michache tu baadaye.
Si Zambia, si Mozambique, si Rwanda, si Congo wala Uganda waliofika msibani.
Si nchi za Comesa, SADC, Ulaya, Marekani kaskazini wala kusini, Si Asia zikiwamo Uarabuni, Afrika wala Australia waliotukumbuka.
Hamkani si shwari tena bila ya kujali makelele yetu yote, kwa hakika hatuko vizuri. Kama waungwana tunapaswa kujiangalia. Vinginevyo makelele yetu mengi yanaweza kuwa ni kutokea kwenye madebe matupu yasiyoacha kuvuma.
Tukumbuke maneno matupu hayavunji mfupa.
Alipotutoka baba wa taifa (rip), Afrika yote hata dunia walikuwa hapa. Marais karibia wote, SADC, COMESA, ECOWAS, nk achilia mbali wawakilishi wazito wazito wa mabeberu walikuwa hapa kutuhani msiba ule.
Walikuwapo hapa hadi kina Madeline Albright waziri wa mambo ya nje wa Marekani.
Hiyo ndiyo Tanzania iliyokuwa ikisomeka vilivyo duniani kote chini ya rais Mkapa (rip).
Uzi huu kwa hakika tulipo upo, unatuhusu sana na hasa katika zama za leo:
Corona: Mizozo ya mipakani, wa kulaumiwa ni Tanzania
Matatizo hayatanzuliwi kwa kuyakimbia, kujificha au kuyafumbia macho.
Kupafahamu wapi tulipojikwaa ni hatua njema katika kujipanga vizuri zaidi. Kujitenga au kuruhusu kutengwa kamwe hauwezi kuwa uchaguzi ulio bora.
Kujikwaa si kuanguka.
Na huo ndiyo ulio ukweli mchungu.
Siyo siri tena zama zimebadilika na matukio yanakwenda kwa kasi sana. Taifa letu likipita katika kipindi kigumu ambapo kwa bahati mbaya kumezuka hata makundi katika jamii ambayo yamelenga kupiga makelele tu yakijaribu kulazimisha kuufanya uongo kuonekana kuwa ukweli au ukweli kuwa uongo. Mithili ya kujidanganya mchana kuwa ni usiku au usiku kuwa ni mchana.
Mifano iko mingi mno na katika nyanja nyingi.
Ikumbukwe kuwa ukweli ni ukweli na uongo ni uongo na utabakia kuwa hivyo bila ya kujali nani kasema nini au nani atasema nini.
Ukweli mchungu hulka mpya hii haikuwahi kushuhudiwa katika awamu yoyote ya uongozi kabla ya awamu ya hii.
Hivi karibuni tumeondokewa na mzee wetu rais mstaafu mzee Mkapa (rip). Pamoja na sisi kushiriki sana katika shughuli zote za wenzetu, ni Burundi peke yake ndiyo walioweza kutuma ujumbe wao rasmi kuja kutuhani kwenye msiba huu mkubwa kutoka nyumbani kwao.
Si Malawi tulikokwenda kwenye kuapishwa kwa rais Chakwera. Si Zimbabwe tulikokwenda kumhani raisi wao Mugabe (rip). Si Afrika kusini tulikokwenda kumhani Mandela (rip) wala Winnie (rip). Wote hawa, hawakutuma wawakilishi wao rasmi tokea makwao kuja msibani sisi yalipotukuta.
Si Kenya tulikotuma ujumbe wetu mzito kabisa wakiwamo marais Kikwete na Mkapa (rip) kwa pamoja kuwahani kwenye msiba wa rais Moi (rip), kuwa walikuja kutuhani sisi yalipotusibu miezi michache tu baadaye.
Si Zambia, si Mozambique, si Rwanda, si Congo wala Uganda waliofika msibani.
Si nchi za Comesa, SADC, Ulaya, Marekani kaskazini wala kusini, Si Asia zikiwamo Uarabuni, Afrika wala Australia waliotukumbuka.
Hamkani si shwari tena bila ya kujali makelele yetu yote, kwa hakika hatuko vizuri. Kama waungwana tunapaswa kujiangalia. Vinginevyo makelele yetu mengi yanaweza kuwa ni kutokea kwenye madebe matupu yasiyoacha kuvuma.
Tukumbuke maneno matupu hayavunji mfupa.
Alipotutoka baba wa taifa (rip), Afrika yote hata dunia walikuwa hapa. Marais karibia wote, SADC, COMESA, ECOWAS, nk achilia mbali wawakilishi wazito wazito wa mabeberu walikuwa hapa kutuhani msiba ule.
Walikuwapo hapa hadi kina Madeline Albright waziri wa mambo ya nje wa Marekani.
Hiyo ndiyo Tanzania iliyokuwa ikisomeka vilivyo duniani kote chini ya rais Mkapa (rip).
Uzi huu kwa hakika tulipo upo, unatuhusu sana na hasa katika zama za leo:
Corona: Mizozo ya mipakani, wa kulaumiwa ni Tanzania
Matatizo hayatanzuliwi kwa kuyakimbia, kujificha au kuyafumbia macho.
Kupafahamu wapi tulipojikwaa ni hatua njema katika kujipanga vizuri zaidi. Kujitenga au kuruhusu kutengwa kamwe hauwezi kuwa uchaguzi ulio bora.
Kujikwaa si kuanguka.
Na huo ndiyo ulio ukweli mchungu.