Watanzania 27 wanamiliki mabilioni Uswisi

Ndugai amesema huyo mandishi anatafuta cheap popularity..........a new term in the hood.

Wewe ukiona wanatumia terms zenye utata, mwenye akili unajuwa kwamba kuna kitu pale si bure! Kumbuka spika SITA alivyo brush aside list ya mafisadi iliyo andikwa na wazalendo mtandaoni - nini kilitokea baadae, ikaja gundulika kwamba taharifa hizo za mtandaoni ni za kweli.

Watanzania tulivyo wa hajabu wakati mwingine kwa kushindwa kutabirika, SITA huyo huyo kahanza kulivalia njuga swala la ufisadi ambalo aliwahi kulipinga na kubeza sources zake, si ajabu historia ikajirudia tena katika suala hili - time will TELL.
 
Wanabodi,

Watanzania 27 wakiwamo wanasiasa na wafanya biashara, imebainika kuwa ndio wameficha mabilioni ya fedha nchini Uswisi, huku mmoja wao akiwa anamiliki Dola za Marekani milioni 56 (sawa na Sh89.6 bilioni).

Taarifa hizo zinaeleza kuwa mbali na kigogo anayemiliki Sh90 bilioni, wapo wengine wanne, ambapo anayefuatia anamiliki Dola 30 milioni (Sh48 bilioni) mwingine Dola 20 milioni (Sh32 bilioni) na wengine wawili kila mmoja anamiliki Dola 10 milioni (Sh16 bilioni). Katika orodha ya walioweka fedha nchini humo, pia wamo wawili waliowahi kuwa mawaziri katika Serikali ya Awamu ya kwanza ya Mwalimu Julius Nyerere, ambao wanamiliki Dola 500,000 kwa kila mmoja.

Miongoni mwa wanaomiliki fedha hizo ni kiongozi wa juu nchini pamoja na aliyepata kuwa waziri katika Serikali ya Awamu ya Tatu iliyoongozwa na Rais Benjamin Mkapa.

SOURCE: MWANANCHI AGOSTI 18 2012

Vipi Ritz,Nape amesitisha allowance???au ni nini?
 
Tatizo wenye dhamana ya kutaja ndio hao hao MAFISADI kesi ya ngedele unampa nyani
 
kwangu mimi hii si habari,,,,,NAHITAJI HABARI,HABARI YENYE MAJINA YA WALIOFICHA,,,,NA SI KUWATAJA PIA WAFIKISHWE MAHAKAMAN,NA SI TU KUWEKWA MAHAKAMAN PIA WAPOKWE HAYO MAHELA,NA SI KUPOKWA TU WANAPASWA KUHUKUMIWA JELA,NA SI KUHUKUMIWA TU PIA WAFILISIWE

mkuu umesahau WANYONGWE hadharani.!
 
Wewe ukiona wanatumia terms zenye utata, mwenye akili unajuwa kwamba kuna kitu pale si bure! Kumbuka spika SITA alivyo brush aside list ya mafisadi iliyo andikwa na wazalendo mtandaoni - nini kilitokea baadae, ikaja gundulika kwamba taharifa hizo za mtandaoni ni za kweli.

Watanzania tulivyo wa hajabu wakati mwingine kwa kushindwa kutabirika, SITA huyo huyo kahanza kulivalia njuga swala la ufisadi ambalo aliwahi kulipinga na kubeza sources zake, si ajabu historia ikajirudia tena katika suala hili - time will TELL.
Nakumbuka clearly kwenye mahojiano ITV, alikuwepo Dr Slaa, Sita na some other guys, Dr. Slaa akaonyesha jinsi gani fedha zimeibiwa na kuonyesha evidence mpaka za receipt na scanned letters.

Sita, wakati huo akiwa speaker, akasema haya ni makaratasi ya mtandaoni, hatuwezi kufanya kazi kwa maratasi ya mtandaoni. Serikali ya CCm ipo imara na hakuna wizi wowote.

Sasa hivi nikimuona Sita anajifanya mpambanaji nasikia kichefuchefu kabisa......wanasiasa hawa wa CCM wanatakiwa kunyongelewa mbali.
 
Huyo ni Jakaya Kikwete tu

Afadhali umeshaconclude, wala hakuna kubabaisha hapo, sasa kama Rais ni mwizi je wananchi huko si wote watakuwa vibaka. Kutoka moyoni Kikwete amekosa credibility ya kuwa Rais ninmwomba tu kwa ridhaa yake ajiuzulu ili ajiwekee heshima kwa watanzania. Na sisi watanzania tuache upole tumtoe huyu mkuu wa Mafisadi Tanzania other wise nchi yetu inazidi kuteketea
 
Hivi mpaka hizi propaganda ziishe,hawa wezi si watakuwa wameshahamisha hizi fedha kwenda kwenye account nyingine mbili tatu?
 
Nasikia wameshaanza ,kuzihamisha kutoka uswiss kwenta uholanzzi
 
Andrew Chenge Alifanya jambo la msingi sana kutamka kuwa Tsh 1.2bilioni zake huko ugaibuni ni vijisenti tu, mtu mmoja anaiibia nchi Tsh 90bilioni?. Nimeichoka nchi hii mimi dah!.
Wanabodi,

Watanzania 27 wakiwamo wanasiasa na wafanya biashara, imebainika kuwa ndio wameficha mabilioni ya fedha nchini Uswisi, huku mmoja wao akiwa anamiliki Dola za Marekani milioni 56 (sawa na Sh89.6 bilioni).

Taarifa hizo zinaeleza kuwa mbali na kigogo anayemiliki Sh90 bilioni, wapo wengine wanne, ambapo anayefuatia anamiliki Dola 30 milioni (Sh48 bilioni) mwingine Dola 20 milioni (Sh32 bilioni) na wengine wawili kila mmoja anamiliki Dola 10 milioni (Sh16 bilioni). Katika orodha ya walioweka fedha nchini humo, pia wamo wawili waliowahi kuwa mawaziri katika Serikali ya Awamu ya kwanza ya Mwalimu Julius Nyerere, ambao wanamiliki Dola 500,000 kwa kila mmoja.

Miongoni mwa wanaomiliki fedha hizo ni kiongozi wa juu nchini pamoja na aliyepata kuwa waziri katika Serikali ya Awamu ya Tatu iliyoongozwa na Rais Benjamin Mkapa.

SOURCE: MWANANCHI AGOSTI 18 2012
 
Watanzania tulivyo wa hajabu wakati mwingine kwa kushindwa kutabirika, SITA huyo huyo kahanza kulivalia njuga swala la ufisadi ambalo aliwahi kulipinga na kubeza sources zake, si ajabu historia ikajirudia tena katika suala hili - time will TELL.

Siku atakapotokea mwenye ujasiri wa kuyaweka hadharani majina, sitashangaa hata wale wanaojiita wapambanaji toka CCM wakawemo.
 
Hii nchi kweli shamba la bibi mpaka wakati wa Nyerere napo watu wamefanya ufisadi, tatizo muandishi kaficha majina.

tatizo lako ukiwa na njaa ndio unakua mzalendo, ukishiba tu tatizo unaanza kuhesabu kesi zilizoko mahakamani na kusifia serika kwamba ni sikivu...!!!kuwa mzalendo wa kudumu kutetea nchi yako kwa maslai ya vizazi vijavyo,angali isije kutokea vizazi vijavyo vikafukua makaburi yetu kupima upeo wetu wa kufikiri ulikuaje. Maana watashangaa kusikia kwamba tulikua na Twiga tukasafirisha nje,tulikua na madini yamebaki mahandaki na nchi bado maskini.!
 
Hivi mpaka hizi propaganda ziishe,hawa wezi si watakuwa wameshahamisha hizi fedha kwenda kwenye account nyingine mbili tatu?

Ni suala la uamuzi tu, hata 2016 (if and only if CCM will be ousted) serikali itakayokuwa madarakani ikitaka kujua transactions baada ya kujulikana linawezekana tu mkuu.

Hapa ni issue ya ithubutu wa kufanya maamuzi magumu, lakini siioni serikali YEYOTE ya CCM kuchukua hatua, maana hata CCM yenyewe ni sehemu ya ufisadi.
 
Upuuz mwwingine huu,mnachoficha majina ni nini,kama mnataja midolare halafu hamsemi ni akina nani na wamezipata vp kuna haja gani ya kutuambia mambo kama haya,hii taarifa itakuwa haina maana ni sawa na hadidhi za shigongo tu,nyambaaaaaafu leaders,tutaishi kwa kuogopana mpaka lini?nchi ya kipuuuzi sana hii,maana ya kuwa na vyombo ya usalama ni nini?
 
Licha ya kumchukia kumbe kubenea ni mtu muhimu sana.hawa waandishi wengine vipi wanaogopa kutaja majina kama habari ni ya ukweli?
 
kumbe kubenea ni mtu muhimu sana.hawa waandishi wengine vipi wanaogopa kutaja majina kama habari ni ya ukweli?
 
Kuwa na fedha nyingi si tatizo. Watu wangependa kujua zilivyopatikana.
Pili, kama kiasi kinajulikana kwa nini majina yasiwekwe hadharani ili nao wapate kutueleza jinsi walivyopata utajiri huu?
Ni vyema majina yakawekwa wazi hususan yale ya wanasiasa na maofisa Wa Serikali.
 
Kuwa na fedha nyingi si tatizo. Watu wangependa kujua zilivyopatikana.
Pili, kama kiasi kinajulikana kwa nini majina yasiwekwe hadharani ili nao wapate kutueleza jinsi walivyopata utajiri huu?
Ni vyema majina yakawekwa wazi hususan yale ya wanasiasa na maofisa Wa Serikali.

Sawa kabisa Dr. Ndungulile. Tujue kama kwa kipato halali kunanuwezekano mtumishi wa umma au mwanasiasa akawa na 90 billion kwen akauntu binafsi?
 
Kuwa na fedha nyingi si tatizo. Watu wangependa kujua zilivyopatikana.
Pili, kama kiasi kinajulikana kwa nini majina yasiwekwe hadharani ili nao wapate kutueleza jinsi walivyopata utajiri huu?
Ni vyema majina yakawekwa wazi hususan yale ya wanasiasa na maofisa Wa Serikali.

Dr unatuangushaaa,fedha hizo si walisema walihongwa na makampuni ya madini na mafuta? Au umesahau? Tar30 october ndio mkinukishe bungeni tuwajue ni kina nani zitto alishasema kama hamkuwataja atawataja live!! Maana hadi mkuu wa chama chenu yumo!!
 
10 Reactions
Reply
Back
Top Bottom