Wanabodi,
Watanzania 27 wakiwamo wanasiasa na wafanya biashara, imebainika kuwa ndio wameficha mabilioni ya fedha nchini Uswisi, huku mmoja wao akiwa anamiliki Dola za Marekani milioni 56 (sawa na Sh89.6 bilioni).
Taarifa hizo zinaeleza kuwa mbali na kigogo anayemiliki Sh90 bilioni, wapo wengine wanne, ambapo anayefuatia anamiliki Dola 30 milioni (Sh48 bilioni) mwingine Dola 20 milioni (Sh32 bilioni) na wengine wawili kila mmoja anamiliki Dola 10 milioni (Sh16 bilioni). Katika orodha ya walioweka fedha nchini humo, pia wamo wawili waliowahi kuwa mawaziri katika Serikali ya Awamu ya kwanza ya Mwalimu Julius Nyerere, ambao wanamiliki Dola 500,000 kwa kila mmoja.
Miongoni mwa wanaomiliki fedha hizo ni kiongozi wa juu nchini pamoja na aliyepata kuwa waziri katika Serikali ya Awamu ya Tatu iliyoongozwa na Rais Benjamin Mkapa.
SOURCE: MWANANCHI AGOSTI 18 2012
Hakuna mwandishi wa habari wa kweli na jasiri kama KUBENEA. Mpaka sasa angeshataja majina, account namba za wahusika na balance kwenye kila account. Miss U Mr Kubenea.
I cant believe, tunaomba serikali ithibitishe hili, nimemkumbuka Nyerere alisamee pension yake kwa kuwa nchi ni maskini, kumbe kuna nyang'au walikuwa wanasubiria aondoke waanze kuamisha hizi fedha. Mimi nawaomba wananchi tuamke nakulipigania hili. Hata kama serikali itakataa kuwataja na kuwachukulia hatua kali ikiwemo kufilisiwa, sisi tukutane jangwani kuelekea ikulu kumshinikiza rais arudishe hizo fedha au ajiuZulu. Currently we are talking inflation which is 20%+ shame on CCM
Watanzania tumegeuka watu wa kulalamika zaidi kiasi hata wale waliopewa madaraka nao wanaongoza tena kulalamika badala ya kutatua matatizo
Kubenea....... Ungekuwa ni wewe ungetupatia hadi acc number zao, achilia majina yao ambayo najua unayo kwenye wallet.
Wanabodi,
Watanzania 27 wakiwamo wanasiasa na wafanya biashara, imebainika kuwa ndio wameficha mabilioni ya fedha nchini Uswisi, huku mmoja wao akiwa anamiliki Dola za Marekani milioni 56 (sawa na Sh89.6 bilioni).
Taarifa hizo zinaeleza kuwa mbali na kigogo anayemiliki Sh90 bilioni, wapo wengine wanne, ambapo anayefuatia anamiliki Dola 30 milioni (Sh48 bilioni) mwingine Dola 20 milioni (Sh32 bilioni) na wengine wawili kila mmoja anamiliki Dola 10 milioni (Sh16 bilioni). Katika orodha ya walioweka fedha nchini humo, pia wamo wawili waliowahi kuwa mawaziri katika Serikali ya Awamu ya kwanza ya Mwalimu Julius Nyerere, ambao wanamiliki Dola 500,000 kwa kila mmoja.
Miongoni mwa wanaomiliki fedha hizo ni kiongozi wa juu nchini pamoja na aliyepata kuwa waziri katika Serikali ya Awamu ya Tatu iliyoongozwa na Rais Benjamin Mkapa.
SOURCE: MWANANCHI AGOSTI 18 2012
hakuna mwandishi wa habari wa kweli na jasiri kama kubenea. Mpaka sasa angeshataja majina, account namba za wahusika na balance kwenye kila account. Miss u mr kubenea.
Du huyu mleta 3d ndio yuleyule naemjua mimi au?
taarifa itakubalika pindi tutakapoona majina, lakini nashangaa tunae rais na hazungumzii suala muhimu kama ili na inatufanya tuamini na yeye yumo.
Ndugai amesema huyo mandishi anatafuta cheap popularity..........a new term in the hood.Nape na Ndugai wanasemaje kuhusu hili!!??
Tatizo lako wewe ni Chadema Addicted kila sehemu unaleta ushabiki wa vyama unadhani watanzania wote ni wafuasi wa vyama vya siasa hapa tunaongelea maslahi ya Taifa.