Mwaka 2000 nikiwa Malaysia kwenye kongamano la dini ya Buddha pale Malaysia university nilikutana na mhindi mmoja tajiri aliyewahi kuishi na kutajirikia bongo.
Kwa utani unaouma na kuakisi ukweli akasema usipotajirika Tanzania ni ngumu kutajirika pengine Niliumia sana naye aliyaona maumivu yangu lakini huo ndio ulikuwa ukweli
Mkataba mbovu wa bandari zetu zote na kampuni kubwa ya DPW umeshapigiwa kelele na kila kaliba ndani ya taifa hili lakini bado kuna mazuzu wajinga wachache wanaona unafaa
Kati ya hao kuna wale walioko mamlakani ambao wamepata chochote ili kuutetea.. Hawa kwangu ni wahaini na wasaliti wakubwa na hukumu yao kuna siku itafika
Ninaowahurumia ni hawa wafuata mkumbo kwasababu za kiimani, itikati za kisiasa jinsia na wote wenye fikra finyu kwamba nwafrika hawezi kitu bila msaada wa ngozi nyeupe ama manjano..
Kinachopiganiwa ni kwa maslahi ya watoto, vijukuu, vitukuu na vining'ina vya taifa hili la Tanganyika.. Bila kujali
Imani zao
Rangi zao
Itikadi zao nk
Haya yote hawayaoni.. Inafika mahali unajiuliza je wana matatizo ya akili?