Mkuu hilo unalolilaani kila great thinker hawezi lifanya.
Isipokuwa kwa muktadha wa Bandari tunashitukia tumeingizwa mkenge wa kujadili itikadi za kidini bila kujua ama kutaka!
Unaijua mbinu ya watawala kuivuruga jamii ya divide and rule, ndiyo hii sasa ujue!
Mjadala umechepushwa kutoka kwenye uhalisia na sasa tunagonganishwa vichwa kwenye udini, ukanda na Utanganyika!
Hivi dini zinaingizwaje kwenye mkataba huu?
Umoja tunaoimbishwa kuwa tunao, je tunao kweli iwapo kila mtu anatetea dini yake badala ya kuitetea jamii aliyomo?
Umoja maana yake ni mseto wa dini, kabila tamaduni mbali mbali katika jamii wanaostahiana na kuvumiliana na kila mmoja akielewa kuwa hakuna aliye bora kuliko mwenzake!
Na ninavyoona mimi, mpasuko unapaliliwa na viongozi wa dini wanapotoka hadharani kuitetea serikali kuwa walichofanya ni chema bila ya kupima upepo jamii inataka nini katika suala hili.
Mimi ni mtu ninayeamini katika umoja wa kijamii, nikiamini kuwa, mtu unapoegemea itikadi za dini wakati jamii tuliyomo ina dini kamchanganyikeni huwa ni kuusambaratisha umoja uliopo.