Watanganyika wanaoitetea DP World wana matatizo ya akili?

Watanganyika wanaoitetea DP World wana matatizo ya akili?

Kwa wale wenye akili, naomba tujadili ubovu wa vipengele (maudhui) vya mkataba ambavyo vimeibuliwa na maaskofu kuliko kuwajadili wao na imani zao ambazo hazimo kwenye mkataba.

Kubwa kuliko yote, baada ya miaka 60 ya uhuru tungeelekeza nguvu zetu katika kuimarisha uwezo wetu wa kuendesha, kusimamia na kudhibiti wenyewe bandari zetu.

Kama hatuwezi kutafuta maarifa na teknolojia ya kupakia, kupakua, kuhifadhi na kusafirisha mizigo tutaweza kipi??!!
 
Umenena vema sana!
Wanapeana peana vyeo kwa kuangaliana huyu ni mtoto wa mwenzetu, wizi ukitokea mtu anahamishwa kutoka Katavi kwenda Njombe eti hiyo ndio adhabu ya kuiba pesa. Baada ya hapo wanakuja humu kulialia hamna ufanisi tubinafsishe bandari.

Sijui ni kwanini Mungu alitupa Nchi nzuri na yenye kila aina ya mali watu tulio wajinga kiasi hiki.
 
Mwaka 2000 nikiwa Malaysia kwenye kongamano la dini ya Buddha pale Malaysia university nilikutana na mhindi mmoja tajiri aliyewahi kuishi na kutajirikia bongo.

Kwa utani unaouma na kuakisi ukweli akasema usipotajirika Tanzania ni ngumu kutajirika pengine Niliumia sana naye aliyaona maumivu yangu lakini huo ndio ulikuwa ukweli

Mkataba mbovu wa bandari zetu zote na kampuni kubwa ya DPW umeshapigiwa kelele na kila kaliba ndani ya taifa hili lakini bado kuna mazuzu wajinga wachache wanaona unafaa

Kati ya hao kuna wale walioko mamlakani ambao wamepata chochote ili kuutetea.. Hawa kwangu ni wahaini na wasaliti wakubwa na hukumu yao kuna siku itafika

Ninaowahurumia ni hawa wafuata mkumbo kwasababu za kiimani, itikati za kisiasa jinsia na wote wenye fikra finyu kwamba nwafrika hawezi kitu bila msaada wa ngozi nyeupe ama manjano..

Kinachopiganiwa ni kwa maslahi ya watoto, vijukuu, vitukuu na vining'ina vya taifa hili la Tanganyika.. Bila kujali
Imani zao
Rangi zao
Itikadi zao nk

Haya yote hawayaoni.. Inafika mahali unajiuliza je wana matatizo ya akili?
FB_IMG_1692523280552.jpg
 
Toa ujinga wako hapa. Hizi propaganda tushazizoea.
Unaweza ukawa ujinga kwa mjinga ila mwerevu ananielewa. Magaid karibu wote wametengenezwa na marekan kwa kushirikiana na Saudia kama hutaki acha. Watu wapo kwenye mission zao we mwenye akili fupi baki ukishangilia tu. Anyways miafrica ndivyo tulivyo
 
Wanapeana peana vyeo kwa kuangaliana huyu ni mtoto wa mwenzetu, wizi ukitokea mtu anahamishwa kutoka Katavi kwenda Njombe eti hiyo ndio adhabu ya kuiba pesa. Baada ya hapo wanakuja humu kulialia hamna ufanisi tubinafsishe bandari.

Sijui ni kwanini Mungu alitupa Nchi nzuri na yenye kila aina ya mali watu tulio wajinga kiasi hiki.
Wenye akili na werevu kama wewe tupo, japo tu wachache. Ila bahati mbaya tunatawaliwa na wajinga wengi, tena wengine wamesoma kwa kukariri na kunukuu tu maandishi ya wengine, si kuelimika!
 
Hizo comments wewe unaona zinatoka kwa watu wenye akili timamu na wanajitambua?
Kuna tofauti gani na yule mzee aliyesema: "kwetu sisi watu hawataki mambo ya katiba, wanataka maji"?
Wengi wape
 
Kwa wale wenye akili, naomba tujadili ubovu wa vipengele (maudhui) vya mkataba ambavyo vimeibuliwa na maaskofu kuliko kuwajadili wao na imani zao ambazo hazimo kwenye mkataba.

Kubwa kuliko yote, baada ya miaka 60 ya uhuru tungeelekeza nguvu zetu katika kuimarisha uwezo wetu wa kuendesha, kusimamia na kudhibiti wenyewe bandari zetu.

Kama hatuwezi kutafuta maarifa na teknolojia ya kupakia, kupakua, kuhifadhi na kusafirisha mizigo tutaweza kipi??!!
Kwa wale wenye akili, naomba tujadili ubovu wa vipengele (maudhui) vya mkataba ambavyo vimeibuliwa na maaskofu kuliko kuwajadili wao na imani zao ambazo hazimo kwenye mkataba.[emoji419][emoji375]
 
Mkuu hilo unalolilaani kila great thinker hawezi lifanya.

Isipokuwa kwa muktadha wa Bandari tunashitukia tumeingizwa mkenge wa kujadili itikadi za kidini bila kujua ama kutaka!

Unaijua mbinu ya watawala kuivuruga jamii ya divide and rule, ndiyo hii sasa ujue!

Mjadala umechepushwa kutoka kwenye uhalisia na sasa tunagonganishwa vichwa kwenye udini, ukanda na Utanganyika!

Hivi dini zinaingizwaje kwenye mkataba huu?

Umoja tunaoimbishwa kuwa tunao, je tunao kweli iwapo kila mtu anatetea dini yake badala ya kuitetea jamii aliyomo?

Umoja maana yake ni mseto wa dini, kabila tamaduni mbali mbali katika jamii wanaostahiana na kuvumiliana na kila mmoja akielewa kuwa hakuna aliye bora kuliko mwenzake!

Na ninavyoona mimi, mpasuko unapaliliwa na viongozi wa dini wanapotoka hadharani kuitetea serikali kuwa walichofanya ni chema bila ya kupima upepo jamii inataka nini katika suala hili.

Mimi ni mtu ninayeamini katika umoja wa kijamii, nikiamini kuwa, mtu unapoegemea itikadi za dini wakati jamii tuliyomo ina dini kamchanganyikeni huwa ni kuusambaratisha umoja uliopo.
Umeandika hekima tupu! Asante🙏🙏
 
Unaweza ukawa ujinga kwa mjinga ila mwerevu ananielewa. Magaid karibu wote wametengenezwa na marekan kwa kushirikiana na Saudia kama hutaki acha. Watu wapo kwenye mission zao we mwenye akili fupi baki ukishangilia tu. Anyways miafrica ndivyo tulivyo
419a044ca6522623ed51a0ac35ac56b7.jpg
 
Ninao since day one ulipovuja na ni kati ya watu wa kwanza kuuweka hapa JF
Kwamba ule ni mkataba?

Katafute mkataba wa TICTS na TPA uone afu uje usome na huo unaosema ni mkataba
 
Kwamba ule ni mkataba?

Katafute mkataba wa TICTS na TPA uone afu uje usome na huo unaosema ni mkataba
Ndio ule ni mkataba ndio maana bunge likaupitisha na mahakama imethibitisha kama ni mkataba! Hiyo mingine siihitaji kwasasa kufanya ulinganifu ni kunitoa kwenye reli
 
Unaweza ukawa ujinga kwa mjinga ila mwerevu ananielewa. Magaid karibu wote wametengenezwa na marekan kwa kushirikiana na Saudia kama hutaki acha. Watu wapo kwenye mission zao we mwenye akili fupi baki ukishangilia tu. Anyways miafrica ndivyo tulivyo

Sijisifii ila umemuandikia mtu ambaye angalau anafahamu yanayoendelea katika siasa za mashariki ya kati na jamii za kiislam. Unayaongelea kirahisi rahisi na kipropaganda mambo ambayo yako very complicated na unataka kuyatumia ili kujaribu kuwagombanisha Waislam wa Tz na ndugu zao wa ghuba na Saudia?

Ila ngoja nikae kimya na akili zangu fupi. Ila hizi propaganda zenu baadhi yetu tushazishtukia.
 
bado kuna mazuzu wajinga wachache wanaona unafaa

Kati ya hao kuna wale walioko mamlakani ambao wamepata chochote ili kuutetea.. Hawa kwangu ni wahaini na wasaliti wakubwa na hukumu yao kuna siku itafika

Hao Wanazingatia MAOKOTO ya Mwarabu.
 
Nanukuu

"Mwaka 2000 nikiwa Malaysia kwenye kongamano la dini ya Buddha pale Malaysia university nilikutana na mhindi mmoja tajiri aliyewahi kuishi na kutajirikia bongo
Kwa utani unaouma na kuakisi ukweli akasema usipotajirika Tanzania ni ngumu kutajirika pengine Niliumia sana naye aliyaona maumivu yangu lakini huo ndio ulikuwa ukweli"

Ni watu wachache sana wa Tanzania wanaoijua hii siri Mshana Jr
Sikumbuki Gazeti, ila nililisoma miaka ya 2000 kipindi cha utawala wa Dr. Mkapa. Kwenye hilo Gazeti, kulikuwa na makala yaliyodadavua kile kilichosemekana mahojiano ya BBC na mfanyabiashara mwenye asili ya India.

Huyo mfanyabishara alitaka kuwekeza kwenye ufugaji wa Kamba, nafikiri, kwenye bonde la Mto Rufiji, lakini mpango wake ulikwama baada ya Serikali kumnyima kibali.

Alipoulizwa juu ya fursa zilizopo Tanzania, alisema, " Tanzania ndiyo nchi pekee ambayo unaweza ukaenda ukiwa maskini ukarudi ukiwa tajiri".
 
Back
Top Bottom