Mwita Maranya
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 10,564
- 7,973
Kumbe mzee Ndege alishafariki then huyo anakuwaje mke wa mtu?
Umeniwahi mkuu hata mimi nilitaka kuuliza hivyohivyo!!Mleta hoja tunaomba majibu tafadhari!
Kwanza kabisa inaonekana hamkumsoma na kumuelewa muanzisha thread. Anasema mzee wassira alianza kuishi na huyo mama mke wa marehemu Ndege wakati mumewe akiwa bado hai, hali iliyomsababishia presha na hatimaye akatangulia mbele ya haki.
Pili, nataka niwasaidie kuelewa japo kidogo mila za kikurya, hasa kwenye suala la ndoa. Kwa wakurya mwanamke anaolewa mara moja tu, ikitokea anaolewa mara ya pili ni hadi pale mwanamke huyo amepewa talaka na mumewe na familia ya mwanamke huyo wameweza kurudisha mahari iliyokuwa imetolewa kwa ajili ya kuolewa kwa binti yao. Sasa inapotokea mume amefariki, mahari haiwezi kamwe kurudishwa, na mwanamke huyo anabaki kuwa mke halali wa huyo bwana aliyefariki na familia ya mwanamke haiwezi kamwe kupokea mahari kutoka kwa mwanaume mwingine.Kwahiyo hata ikitokea amepata bwana na kuamua kuishi naye bado anahesabika ni mke halali wa bwana'ake wa awali.
Kwa muktadha huo ni dhahiri kwamba mzee wassira anaishi na mke wa marehemu Ndege, na anachofanya ni kulea familia ya mwanaume mwenzake, ambaye kwa namna moja ama nyengine yeye wassira alichangia kuivuruga familia yake pamoja na kampuni yake ya Ndege insurance ambayo kwa sasa sina uhakika kama bado ipo.