Wasichana wasichana ugali tu

Wasichana wasichana ugali tu

Napata hofu kidogo baadhi ya wasichana hasa wa mjin mpaka kufikia umri wa kuolewa lakin hawezi kupika ugali tu.Dada zangu kuna ugumu gani kupika ugali,kijijin hata mtoto wa kike wa darasa la tatu anapikia familia ya watu watano na kuendelea mjini kazi ipo unakuta binti kafika mpaka chuo Kikuu kupika hawezi.nini tatizo jaman

Sasa kama tumekutana mimi nawewe wote hatujui kupika ugali kwenye ndoa, y blaming zije kwangu tu. Mkuu we unajua kupika ugali?
 
Namshukuru sana mama yangu.maana alikuwa anakwambia songa ugali.unausonga ukiivisha anakuja anaukata anarusha ukutani.dah ukinasia ukutani anakwambia mbichi kula mwenyewe.alafu unamsongea mwingine adi uive.sasa kasheshe ule ugali wa mwanzo tena mwingi na adhabu yako adi umalize kuula ili usirudie kupika ugali mbichi.vile vile wali ukipika utoke na kiini utajuta jamani.kweli sijisifii najua kupika ila yote ni juhudi ya mama.je akina mama wenzangu mnawafundisha mabinti zenu kupika?au ndo kutwa kuchwa kwenye TV na kumbi za sherehe.
 
mimi mwenyewe sijui kusonga ugali.lakini mahanjumati mengine mengi tu naweza.nilivyokuwa mdogo katika chakula nilichokuuwa sikipendi kilikuwa ugali,maybe imechangia.sie wa pwani ugali sio big deal.ukijua kupika maandazi,chapati,mikate ya ufuta,biriani,na mahanjumati mengineyo inatosha,na wewe mtoa mada kama mwenzako hajui si umfundishe?
 
Dah nilichogundua nikua wasichana wengi hiki chakula hawakipendi ndomana pia hawataki kujifunza kukipika ila lamsingi wanawake mnatakiwa kujifunza kupika vyakula tofauti tofauti kuna siku nilimwambia msichana wa kazi apike pilau akaniambia hawezi nilishangaa sana na ni msichana mkubwa tu wa kuolewa!mke akijua kupika nako kuna raha yake!
 
Mmms sio wote jamani wengine tunajua kupika kila kitu n we are proud,na hata hao wanaojishaua na kucha za bandia na ma make up usoni wanajua sana sema tu wanataka waonekane watoto wa kishua hawajui hata kupika chai ila kiukweli wanajua na ukiwakuta kwao wanapika vizuri tu.....kwanza I believe binti/mwanamke mzuri n yule anaejitunza yeye mwenyewe mrembo ila pia anaejua kutunza nyumba including mapishi.Mbona wakiolewa wanapika vitu vya kueleweka???
 
mimi mwenyewe sijui kusonga ugali.lakini mahanjumati mengine mengi tu naweza.nilivyokuwa mdogo katika chakula nilichokuuwa sikipendi kilikuwa ugali,maybe imechangia.sie wa pwani ugali sio big deal.ukijua kupika maandazi,chapati,mikate ya ufuta,biriani,na mahanjumati mengineyo inatosha,na wewe mtoa mada kama mwenzako hajui si umfundishe?
ugal rahis sana kupika hata leo tu kama hujui kupika ukiamua kujifunza unaweza kua mpishi mzuri tu,ingekua pilau ama vyakula vingne vinavyohitaj process nying na ndefu sawa lakin ugal hata dakika tano haichukui oneni aibu kidogo
 
ugali kale kwenu........

Jifunze kupika ugali leo dada kama hujui,ukiolewa unakua na kwako na mumeo ambae atahitaji kupikiwa nawe,elewa kua chakula kikuu cha sisi waafrika ni ugali tena na maharage labda udanganye hapa kua hujawahi kula ugali
 
Atapika saa ngapi na beki tatu afanye nini?!!! style ya maisha imebadilika sana wandugu!!!nawaonea sana huruma wadogo zangu watakaokuja kuoa lets say miaka 10 ijayo maana hawataoa wanawake bali wanawake jina maana watoto wa kike siku hizi wanapoteza kabisa ile haiba ya mwanamke!!!!
 
Jifunze kupika ugali leo dada kama hujui,ukiolewa unakua na kwako na mumeo ambae atahitaji kupikiwa nawe,elewa kua chakula kikuu cha sisi waafrika ni ugali tena na maharage labda udanganye hapa kua hujawahi kula ugali

correction.......mimi ni mke halali wa mtu na mume wangu si mpenzi sana wa ugali.....
 
Sasa kama tumekutana mimi nawewe wote hatujui kupika ugali kwenye ndoa, y blaming zije kwangu tu. Mkuu we unajua kupika ugali?
wewe unaona sawa mkikutana ndoani wewe hujui na mumeo hajui?
 
wewe unaona sawa mkikutana ndoani wewe hujui na mumeo hajui?

si kila kitu ni kujifunza, ye ajui nimfundishe, me sijui anifundishe, kwani walioanza kupk walijuaje? iv uwa mnaoa ili mpate lyfpartner ama slave?
 
Jifunze kupika ugali leo dada kama hujui,ukiolewa unakua na kwako na mumeo ambae atahitaji kupikiwa nawe,elewa kua chakula kikuu cha sisi waafrika ni ugali tena na maharage labda udanganye hapa kua hujawahi kula ugali
Hivi nyinyi wanaume kwanini kila kitu unarefer kuolewa? acheni ubinafsi bhana, kwani mtu anatakiwa kufahamu vitu kwa sababu tu ya kuolewa? mbona nyinyi hamjifunzi vitu ili mkioa muwafurahishe wake zenu? huu ndo utumwa tusio utaka sisi. By theway, kama mkeo hajui kitu si umfundishe? sio rahisi kufahamu vitu vyote. na isitoshe kila mtu anapreference zake katika maisha, so inatekemea unaemwoa anaprefer nini katika maisha yake kama wewe ulivyo na preference zako.
 
Hahahaha kiboko yao waolewe na wakurya au wasukuma mbona watajua kuupika? Mwanamke jiko bwana, ujue mapishi ya bara na pwani, tena siku hizi tunaongezea na ya kiitaliano, kichina, kifaransa na mengineyo. Mwanamke wa ukweeee lazima ujue kulitawala jiko.........Hakuna mahali nilifundishwa kupika ila juhudi binafsi zimenifanya walau vyakula vya kitanzania niviwezee.
 
Back
Top Bottom