Umeme ulikatika asubuhi. Nikaamua kwenda matembezi. Nimetoka Butiama kwenda kijiji cha jirani cha Busegwe,kilomita ngapi sijui,tano,sita,saba,I don't know. Wakati wa kurudi,natembea,nimewaona wamekaa chini katikati ya ile barabara ya vumbi.[murram]. Nadhani ni wachimba madini hawa. Walikuwa na vyombo vyao vya kuchimba madini,mitarimbo mingi,ya kunipiga nayo bila shaka.
Wale watu walikuwa wamekaa chini,na zikaja bodaboda kadhaa ,wakafika pale wakaanza kuzungumza nao,wanaonekana kama walikuwa wote conspirators.
Halafu akapita mdada mmoja,halafu likapita lorry,basi,wale watu wakaamua kuondoka. Na mimi wakati huo nilikuwa nimesimama,sitaki kwenda mbele,mpaka waondoke.
Walipoondoka,nilipokwenda mbele kidogo,nikaona gari imepakiwa machakani,pembeni ya barabara,wamo watu wamevaa kiraia,na mmoja alikuwa amevaa nguo za skauti. Wale watu nadhani walikuwa ni polisi,maybe they were keeping an eye on those folks I had just seen. Kwa sababu kama walitokea kijijini Butiama na ile mitarimbo,njia inapita kituo cha polisi.
Lakini kwa pale walipokuwa polisi,wangeweza kuwakamata wahalifu kama wangetenda tukio,lakini wasingeweza kuwazuia.
Ndio matatizo ya huku kijijini. The place is sparsely populated.
Dharma may find me in her hands at the keyboard--YOU WILL FIND ME IN THE WORD OF TRUTH--IN THE THOUGHT AS PRESENTED. And the ''physical'' signs? In the twinkling,strobing colored light beams of the viewable heavens---our army waiting twixt YOU and the very planets and stars you NAME so that you cannot miss us! To NOT recognize our presence,YOU HAVE TO DENY US!