Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma, linawatafuta watu wawili akiwemo mwanafunzi wa darasa la sita wakazi wa kijiji cha Lilondo wilayani Songea kwa tuhuma za kumvalisha mbwa fulana ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) yenye picha ya mgombea urais wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete.
Kamanda wa Polisi mkoani Ruvuma, Michael Kamuhanda, alisema jana kuwa tukio hilo lilitokea Oktoba 24, mwaka huu saa 9:00 alasiri eneo la Lilondo wilayani Songea.
Kamanda Kamuhanda aliwataja watuhumiwa hao wanatafutwa na polisi kuwa ni Ephraem Mahuwi anayekadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 25 na 27, na mwanafunzi wa darasa la sita katika Shule ya Msingi ya Lilondo (jina limehifadhiwa).
Alifafanua kuwa muda mfupi kabla ya tukio hilo, baadhi ya wakazi wa kijiji cha Lilondo, walimwagiwa sare za CCM zikiwemo fulana, kofia, khanga na skafu wakati msafara mkubwa wa magari yaliyokuwa yakimsindikiza mke wa mgombea urais kupitia CCM, Mama Salma Kikwete, ukipita kutokea Ruvuma kwenda mkoani Iringa.
Kamanda Kamuhanda aliongeza kuwa baada ya msafara huo kupita, mtuhumiwa Mahuwi na mwanafunzi huyo, walichukua moja ya fulana za CCM walizogawiwa ikiwa na picha ya mgombea urais kupitia chama hicho na kumvalisha mbwa.
Alisema baada ya kumvalisha mbwa huyo, watuhumiwa hao walimuacha aendelee kurandaranda sehemu mbalimbali za kijijini humo.
Kamanda Kamuhanda alisema wafuasi wa CCM walimuona mbwa huyo aliyevalishwa sare za chama chao na kuanza kumkimbiza kwa takriban saa moja na kufanikiwa kumkamata.
Alisema wafuasi hao wa CCM walibaini kuwa mbwa huyo ni mali ya Mahuwi na kwamba baada ya kusikia mbwa wake amekamatwa, yeye na mwanafunzi huyo, walikimbia na kwenda kusikojulikana.
Hata hivyo, Kamanda Kamuhanda alisema polisi wanafanya kila liwezekano kuhakikisha kwamba watuhumiwa hao wanakamatwa na kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili
Kwani shida iko wapi kumvika mbwa gauni au nguo ya aina yoyote? Check hizi picha za mbwa na tishet ya Obama. Kama obama anvaliwa na mbwa who is Kikwete?
Wewe Opinionated nadhani hauko sawa sawa. Kwani Obama wana uhusiano gani na Kikwete hata ukasema hivyo? Obama ni Mungu wako? Na mila na silka zao ziko sawa na za kwetu?
Hebu jadili mantiki ya hili jambo na sio kusema kama Obama anafanya hivi basi ndiyo dunia nzima waendelee kufanya hivyo.
Today this afternoon I were taking my son of 6yrs from school. I met one of my friend and he stopped me. I thought he has a something special! Without saying anything he threw a CCM cap to my car. Usishangae mtoto alimuuliza this for what? Akamwambia for your dad to put on. Boy alimwambia MY DAD DONT PUT ON SUCH COLOUR and he hand it over to him. Baadaye dogo akaniuliza kwani wewe ni ccm baba? Nikamwambia hapana, akasema afadhali maana lichama lenyewe la mafisadi kama nini. Nikamuuliza mafisadi ni nini? Akasema ni WEZI. A boy of 6 yeras! Anawajua ccm na rangi zao na ufisadi wao! SHAME YOU CCM!Hadi wanafunzi wa darasa la sita wamemchukia Jk. Maana hawa wanafunzi hawana chama. Haya mambo hayo!!!!!!!!!
.......Nilivyosoma hii habari nimecheka sana,its so damn funny!!! Sasa CCM wamechukia nini na wakati mbwa anashabikia naye uchaguzi kwa kuvaa t-shirt.