Sildenafil Citrate
JF-Expert Member
- Jan 29, 2021
- 573
- 2,553
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza tarehe 02.06.2023 muda wa 21:40 usiku huko maeneo va Sabasaba. Kata na Wilava va Ilemela limefanikiwa kumkamata mtuhumiwa aitwaye James Chacha, miaka 58, mfanyabiashara, mkazi wa lloganzara akiwa anafanya biashara ya Danguro kwenye nyumba yake na katika Nyumba hiyo walikamatwa watuhumiwa 53 kati yao wanawake 23 na wanaume 30 wakifanya vitendo vya ngono kinyume na maadili.
Mnamo tarehe 02.06.2023 muda wa 08:30 asubuhi Jeshi la Polisi lilipokea taarifa kutoka kwa raia wema kuwa eneo la lloganzara karibu na shule ya msingi Tulele @kwa Chacha kuna biashara ya Danguro. Baada ya taarifa hizo kuripotiwa askari walifanya ufuatiliaji ambapo walifika eneo hilo nakufanikiwa kuwakamata watuhumiwa hao. Watuhumiwa wanaendelea kuhojiwa na pindi upelelezi ukikamilika hatua stahiki za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Tarehe 01.06.2023 muda wa 14:00 mchana huko katika kijiji cha Chema, tarafa ya Kahunda, Wilaya ya Sengerema, kulipatikana taarifa kuwa kuna mtu anatoa mahubiri ya kupotosha jamii kwa kuwataka waumini wake wasiende Hospital kupata huduma ya matibabu pindi wakiugua au kuuguliwa; Badala yake wapelekwe kwenye kanisa lake liitwalo Neno kwaajili ya kuombewa na kupata uponyaji wa magonjwa yanayo wakabili.
Askari Polisi walifika katika kanisa hilo lililopo kijiji cha chema na kufanikiwa kumkamata Herman Magigita, miaka 60, mehungaji wa kanisa la Neno na mkazi wa Mwangika kwa tuhuma za kosa la kufanya shughuli za kanisa bila kuwa na kibali cha usajili kinyume cha sheria na kutoa mahubiri potofu kwa waumini wake.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza tunatoa wito kwa wakazi wote wa Mkoa wa Mwanza kuendelea kuliamini Jeshi la Polisi na kutoa taarifa zaidi za uhalifu na wahalifu wote ili hatua za kisheria ziendelee kuchukuliwa dhidi yao, kamwe tusifiche uhalifu kwa namna yoyote ile. Jeshi la Polisi tumejipanga vizuri kuhakikisha kuwa taarifa hizo zinafanziwa kazi kwa weledi na uaminifu mkubwa.
Mnamo tarehe 02.06.2023 muda wa 08:30 asubuhi Jeshi la Polisi lilipokea taarifa kutoka kwa raia wema kuwa eneo la lloganzara karibu na shule ya msingi Tulele @kwa Chacha kuna biashara ya Danguro. Baada ya taarifa hizo kuripotiwa askari walifanya ufuatiliaji ambapo walifika eneo hilo nakufanikiwa kuwakamata watuhumiwa hao. Watuhumiwa wanaendelea kuhojiwa na pindi upelelezi ukikamilika hatua stahiki za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Tarehe 01.06.2023 muda wa 14:00 mchana huko katika kijiji cha Chema, tarafa ya Kahunda, Wilaya ya Sengerema, kulipatikana taarifa kuwa kuna mtu anatoa mahubiri ya kupotosha jamii kwa kuwataka waumini wake wasiende Hospital kupata huduma ya matibabu pindi wakiugua au kuuguliwa; Badala yake wapelekwe kwenye kanisa lake liitwalo Neno kwaajili ya kuombewa na kupata uponyaji wa magonjwa yanayo wakabili.
Askari Polisi walifika katika kanisa hilo lililopo kijiji cha chema na kufanikiwa kumkamata Herman Magigita, miaka 60, mehungaji wa kanisa la Neno na mkazi wa Mwangika kwa tuhuma za kosa la kufanya shughuli za kanisa bila kuwa na kibali cha usajili kinyume cha sheria na kutoa mahubiri potofu kwa waumini wake.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza tunatoa wito kwa wakazi wote wa Mkoa wa Mwanza kuendelea kuliamini Jeshi la Polisi na kutoa taarifa zaidi za uhalifu na wahalifu wote ili hatua za kisheria ziendelee kuchukuliwa dhidi yao, kamwe tusifiche uhalifu kwa namna yoyote ile. Jeshi la Polisi tumejipanga vizuri kuhakikisha kuwa taarifa hizo zinafanziwa kazi kwa weledi na uaminifu mkubwa.