Warioba, Wananchi Walitaka "Serikali 3" au "Nchi 3?"

Warioba, Wananchi Walitaka "Serikali 3" au "Nchi 3?"

Ukitaka kujua kuwa hizo "Nchi Washirika" zina HADHI SAWA na Nchi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania soma Ibara ya 8 (4) inayosema kama ifuatavyo:

"Sheria yoyote, mila, desturi au uamuzi wowote wa chombo cha dola, Ofisa wa Serikali au chombo binafsi ni sharti afuate na kuendana na masharti yaliyomo kwenye Katiba hii na kwamba Sheria, Mila, Desturi au uamuzi wowote ambao hautawiana au kwenda sambamba na masharti ya Katiba hii utakuwa batili."

Hapa zinapozungumziwa Sheria, Mila, Desturi au uamuzi wowote maana yake ni Sheria, Mila, Desturi au uamuzi wowote wa Jamhuri ya Muungano (ie katika mambo ya Muungano) na sio Sheria, Mila, Desturi au uamuzi wowote wa "Nchi Washirika." Zaidi ya hapo Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haijatajwa kuwa ni
KUU kupita Katiba za Nchi Washirika! Sasa unawezaje kuwa na MAFAHALI WATATU (3) katika zizi moja? Kwa wapenda Muungano watakubaliana na mimi kwa hili!

Hapa ndio lilipo BOMU la kuulipua Muungano wetu, amini usiamini! Kama Muungano utavunjika (endapo Rasimu hii itakuwa Katiba) basi ni kupitia Ibara hii ya 8 na nyingine nilizotaja hapo juu!
 
Je, "wananchi walio wengi" walisema wanataka "Nchi 3" au "Serikali 3?"
Walitaka muungano unaofuata mfumo wa serikali tatu, ya Tanganyika, ya Zanzibar na ile ya Muungano. Kimsingi nchi zipo mbili - Tanganyika na Zanzibar. Ukiunganisha hizo nchi mbili unapata "dhana" ya nchi ya tatu kubwa. Kwa hivyo, kwa mambo yasiyo ya muungano, serikali ya Tanganyiaka itakuwa na mamlaka eneo (nchi) ya Tanganyika, serikali ya Zanzibar itakuwa na mamlaka eneo la Zanzibar na serikali ya muungano itakuwa na mamlaka kwa mambo ya muungano katika eneo lote linalojumuisha eneo la zanzibar na eneo la Tanganyika (nchi ya Tanzania).

Ukisema unataka uwepo wa serikali ni lazima uweze kupambanua eneo (nchi) ambalo serikali hiyo itakuwa na mamlaka. Kwa hivyo kama wananchi wamesema wanataka serikali tatu, mantiki inadai kupambanua maeneo ambayo serikali hizo zitakuwa na mamlaka.

"Waumini" wa serikali mbili, bahati mbaya sana hawatoi takwimu ni wananchi wangapi waritaka muundo huo (achilia mbali muungano wenyewe) wakati muungano unaasisiwa. Angalau hawa waumini wa serikali tatu (hata kama ni "wachache") tunaweza kuwatambua mmoja mmoja na hata kupitia taasisi zao kutokana na maoni waliyoyatoa kwa tume ya Warioba.
 
Wewe unaendeleza ubishi usio na maana.......kwa heri bwana!
Kwa hiyo "ubishi" wako ndio una maana? Kwani kuwa "Washirika" lazima muwe ni nchi? Si mnaweza kuwa "Serikali Washirika" na mambo yakasonga mbele? After all, ndio "maoni ya wananchi walio wengi," right? Mbona mnatumia "maoni ya wananchi walio wengi" kwa yale mnayoyataka nyinyi tu? Mkiona hayaendani na yale myatakayo basi mnakuwa wakali!!
 
Ukisema unataka uwepo wa serikali ni lazima uweze kupambanua eneo (nchi) ambalo serikali hiyo itakuwa na mamlaka. Kwa hivyo kama wananchi wamesema wanataka serikali tatu, mantiki inadai kupambanua maeneo ambayo serikali hizo zitakuwa na mamlaka.
Kwa hiyo Zanzibar kabla ya kuwa "nchi" (kama ni nchi anyway) haikuwa na eneo? Mikoa na Wilaya zetu ambazo zina maeneo ukiangalia ramani ni "nchi" simply kwa kuwa zina maeneo?
 
Kwa hiyo "ubishi" wako ndio una maana? Kwani kuwa "Washirika" lazima muwe ni nchi? Si mnaweza kuwa "Serikali Washirika" na mambo yakasonga mbele? After all, ndio "maoni ya wananchi walio wengi," right? Mbona mnatumia "maoni ya wananchi walio wengi" kwa yale mnayoyataka nyinyi tu? Mkiona hayaendani na yale myatakayo basi mnakuwa wakali!!

Ndugu si nimekwambia kwaheri? au kiswahili nacho kigumu kwako?
 
Buchayanani, unatakiwa kuzungumzia/kujadili kuhusu Tume ya Jaji Warioba na siyo Mh. Jaji Warioba. Unachofanya ni upotoshaji. Mjadala wa kujadili mtu badala ya Tume unaonekana kuwa ni mawazo ya mtu binafsi kwa nia ya kupotosha ukweli.
Unajua wazi kuwa Tume hii iliteuliwa na rais Kikwete. Mnapoinanga tume mjue mnamnanga rais kuwa aliteua watu wa ovyo.
Tafadhali zugumzia taarifa ya tume, acha upotoshaji kwa kumjadili Mh. Jaji Warioba.
 
Mkuu hapa sio Jina pekee bali kuna move ya kuvunja nchi yetu vipande vipande!

Mkuu kama kuvunjika sasa ndio imevunjika hasa baada ya kuundwa kwa katiba ya Zanzibar ya 2010. Kinachofanyika ndio kinaweza kuvunja kabisa kama hakutakuwa na dhamira njema bali kama dhamira ni njema serikali 3 zinaweza kuondoa kero na kuudumisha Muungano.


Sent from my iPad using JamiiForums
 
Kwa hiyo Zanzibar kabla ya kuwa "nchi" (kama ni nchi anyway) haikuwa na eneo? Mikoa na Wilaya zetu ambazo zina maeneo ukiangalia ramani ni "nchi" simply kwa kuwa zina maeneo?
Bila ya shaka ni nchi (kiingereza wanaita "territory"). Serikali ya sasa ya Mapinduzi si ni wazi kuwa ina mipaka ambayo jurisdiction yake inaishia? Kama ilivyo kwa Tanganyika/Tanzania Bara (tunajua itaishia wapi....Mzee Karume alisema "Chumbe"?).
 
Mimi nazungumzia maoni ya Wananchi, ni lini walisema wanataka Nchi 3, hayo maswali yako yanaingiaje hapa?
kama huna jibu la hili funga mdomo kisha log off, Tanganyika iwe nchi au serikali we dont care, we need it back, we need our flag back, tunahitaji nembo yetu ya taifa ( tanganyika). Tunahitaji utaifa wetu.
 
Mkuu kama kuvunjika sasa ndio imevunjika hasa baada ya kuundwa kwa katiba ya Zanzibar ya 2010. Kinachofanyika ndio kinaweza kuvunja kabisa kama hakutakuwa na dhamira njema bali kama dhamira ni njema serikali 3 zinaweza kuondoa kero na kuudumisha Muungano.


Sent from my iPad using JamiiForums
Tuko pamoja Mkuu, lakini kwa bahati mbaya Rasimu hii haidumishi Muungano bali imeufanya si kitu kabisa, angalia ADDITIONAL 2 hapo kwenye Post ya Kwanza hapo juu! Kumbuka maneno ya JK kuwa hata kama tunataka Serikali 3 zisiwe tegemezi wala egemezi! Tusiishie kuwa tunataka Serikali 3 tu basi, wanaojadili zaidi wanaonekana kuwa hawataki kudumisha Muungano!!
 
kama huna jibu la hili funga mdomo kisha log off, Tanganyika iwe nchi au serikali we dont care, we need it back, we need our flag back, tunahitaji nembo yetu ya taifa ( tanganyika). Tunahitaji utaifa wetu.
Unaposema "we" na "tunahitaji" unamaanisha ni miongoni mwa wale 37,000, UKAWA, TANZANIA KWANZA, "wananchi walio wengi" au akina nani? Kuhusu kufunga mdomo au kulog off wewe huna mamlaka yoyote ya kuniamuru kufanya hivyo, na unajua kabisa huna mamlaka, why wasting your precious energy?
 
Tuko pamoja Mkuu, lakini kwa bahati mbaya Rasimu hii haidumishi Muungano bali imeufanya si kitu kabisa, angalia ADDITIONAL 2 hapo kwenye Post ya Kwanza hapo juu! Kumbuka maneno ya JK kuwa hata kama tunataka Serikali 3 zisiwe tegemezi wala egemezi! Tusiishie kuwa tunataka Serikali 3 tu basi, wanaojadili zaidi wanaonekana kuwa hawataki kudumisha Muungano!!

Thanx mkuu nimekuaoma. Ila mie sio mtaalamu wa masuala ya katiba na najaribu kutumia nadharia ya mijadala. Waweza kuwa sahihi kabisa. Ila jambo linaloleta shida ni kuwa rasimu imepelekwa kwa majadiliano na maridhiano na jambo hilo lingefanyika sidhani kama kungekuwa na shida kubwa. Tatizo limeanza baada ya hotuba ya ufunguzi. JK katoa hotuba ya kuonyesha msimamo wa chama chake. Pamoja na kuwa haikuwa mahala pake, bado katoa msimamo huo katika mfumo wa kutishana na katumia kofia ya Urais hivyo kufanya maoni yake ya kichama yasiwe ya kichama tena bali AMRI ya Ki raisi. Buchanan lazima tukubaliane lile lilikuwa kosa kubwa sana. Ndio mwanzo wa kuchafuka hali ya hewa kulikojitokeza ndani ya Bunge. Wapo wajumbe wa CCM ambao kwao kauli ya mwenyekiti haijadiliki ni kama vifungu vya msahafu, ni mmoja tuu nimesikia ametamka wazi msimamo tofauti na yuko tayari kwa mjadala naye ni Lembeni.


Sent from my iPad using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Buchayanani, unatakiwa kuzungumzia/kujadili kuhusu Tume ya Jaji Warioba na siyo Mh. Jaji Warioba. Unachofanya ni upotoshaji. Mjadala wa kujadili mtu badala ya Tume unaonekana kuwa ni mawazo ya mtu binafsi kwa nia ya kupotosha ukweli.
Unajua wazi kuwa Tume hii iliteuliwa na rais Kikwete. Mnapoinanga tume mjue mnamnanga rais kuwa aliteua watu wa ovyo.
Tafadhali zugumzia taarifa ya tume, acha upotoshaji kwa kumjadili Mh. Jaji Warioba.
Buchayanani ndio nani? Kwani ukiandika kwa kuheshimiana ujumbe wako haufiki? Tume imeshavunjwa, unataka nizungumzie Tume ipi tena?
 
Kama ni "Ripoti ya Tume" mbona amekuwa anaongea sana utafikiri ana issue binafsi!! Tume ilishavunjwa lakini cha ajabu ameendelea kujitetea na kuwaponda wengine (kwa mfano Prof. Shivji) wenye mawazo tofauti na ya kwake!

Wewe thread yako umenukuu maneno ya rasimu,then mnamkashifu Warioba!kuvunjwa kwa tume hakuzuii wao kutoa ufafanuzi na ndio maana sheria ya kuunda Bunge la katiba inasema wanaweza kuitwa kwa ufafanuzi!kama haujahadithiwa kuhusu Shivji na Warioba nadhani ndani ya moyo wako unajua nani alianza personal attacks.
 
Thanx mkuu nimekuaoma. Ila mie sio mtaalamu wa masuala ya katiba na najaribu kutumia nadharia ya mijadala. Waweza kuwa sahihi kabisa. Ila jambo linaloleta shida ni kuwa rasimu imepelekwa kwa majadiliano na maridhiano na jambo hilo lingefanyika sidhani kama kungekuwa na shida kubwa. Tatizo limeanza baada ya hotuba ya ufunguzi. JK katoa hotuba ya kuonyesha msimamo wa chama chake. Pamoja na kuwa haikuwa mahala pake, bado katoa msimamo huo katika mfumo wa kutishana na katumia kofia ya Urais hivyo kufanya maoni yake ya kichama yasiwe ya kichama tena bali AMRI ya Ki raisi. Buchanan lazima tukubaliane lile lilikuwa kosa kubwa sana. Ndio mwanzo wa kuchafuka hali ya hewa kulikojitokeza ndani ya Bunge. Wapo wajumbe wa CCM ambao kwao kauli ya mwenyekiti haijadiliki ni kama vifungu vya msahafu, ni mmoja tuu nimesikia ametamka wazi msimamo tofauti na yuko tayari kwa mjadala naye ni Lembeni.


Sent from my iPad using JamiiForums

Kwa upande wangu mimi niliiona Hotuba ya Rais Kikwete kama angalizo badala ya msimamo au amri, ndio maana aliwaambia Wajumbe kuwa "mamlaka mnayo nyinyi!" Still watu wana uwezo wa kumpinga Kikwete kwa manufaa ya umma, kama wanavyodai! Ndio maana Kikwete alisema kuwa kama tunataka Serikali 3 basi ziwe imara, je hapa kosa la Kikwete ni lipi? Hata kama asingeonesha msimamo Bungeni, still Sera ya CCM kuhusu Serikali 2 inajulikana! Ni chama gani ambacho hakitaki Sera yake kufanyiwa kazi? Obviously hakuna, kwa hiyo hakuna wa kumlaumu mwenzake! Ndio maana UKAWA wako busy, si kutetea maslahi ya wananchi kama wanavyodai bali ni kucomply na sera zao!
 
Wewe thread yako umenukuu maneno ya rasimu,then mnamkashifu Warioba!kuvunjwa kwa tume hakuzuii wao kutoa ufafanuzi na ndio maana sheria ya kuunda Bunge la katiba inasema wanaweza kuitwa kwa ufafanuzi!kama haujahadithiwa kuhusu Shivji na Warioba nadhani ndani ya moyo wako unajua nani alianza personal attacks.
Kwa jinsi Warioba alivyolichukulia suala hili ni kama la kwake, hiyo kwa sababu ameendelea "kuiwakilisha" Tume hata baada ya kuvunjwa!! Labda anataka kugombea Urais wa Tanganyika, who knows? Na kwa uzoefu nilio nao kuhusu viongozi wa nchi hii, ukiona mtu anakomalia sana jambo ujue liko jambo!
 
Bila ya shaka ni nchi (kiingereza wanaita "territory"). Serikali ya sasa ya Mapinduzi si ni wazi kuwa ina mipaka ambayo jurisdiction yake inaishia? Kama ilivyo kwa Tanganyika/Tanzania Bara (tunajua itaishia wapi....Mzee Karume alisema "Chumbe"?).
Kwa hiyo kwa maoni ya "wananchi walio wengi" walitaka "Nchi 3," "Territory 3," au unataka kusema nini hasa? Au definition yako inatusaidiaje kujua maoni ya wananchi yalilenga nini?
 
Back
Top Bottom