SMU
JF-Expert Member
- Feb 14, 2008
- 9,613
- 7,902
Acha kuruka ruka. Soma post zangu vizuri.Kwa hiyo kwa maoni ya "wananchi walio wengi" walitaka "Nchi 3," "Territory 3," au unataka kusema nini hasa? Au definition yako inatusaidiaje kujua maoni ya wananchi yalilenga nini?
Walitaka muungano unaofuata mfumo wa serikali tatu, ya Tanganyika, ya Zanzibar na ile ya Muungano. Kimsingi nchi zipo mbili - Tanganyika na Zanzibar. Ukiunganisha hizo nchi mbili unapata "dhana" ya nchi ya tatu kubwa. Kwa hivyo, kwa mambo yasiyo ya muungano, serikali ya Tanganyiaka itakuwa na mamlaka eneo (nchi) ya Tanganyika, serikali ya Zanzibar itakuwa na mamlaka eneo la Zanzibar na serikali ya muungano itakuwa na mamlaka kwa mambo ya muungano katika eneo lote linalojumuisha eneo la zanzibar na eneo la Tanganyika (nchi ya Tanzania).
Ukisema unataka uwepo wa serikali ni lazima uweze kupambanua eneo (nchi) ambalo serikali hiyo itakuwa na mamlaka. Kwa hivyo kama wananchi wamesema wanataka serikali tatu, mantiki inadai kupambanua maeneo ambayo serikali hizo zitakuwa na mamlaka.
"Waumini" wa serikali mbili, bahati mbaya sana hawatoi takwimu ni wananchi wangapi waritaka muundo huo (achilia mbali muungano wenyewe) wakati muungano unaasisiwa. Angalau hawa waumini wa serikali tatu (hata kama ni "wachache") tunaweza kuwatambua mmoja mmoja na hata kupitia taasisi zao kutokana na maoni waliyoyatoa kwa tume ya Warioba.
Kama hoja zimekwisha katika hili, anzisha mjadala mwingine: