Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,192
- 1,976
Mheshimiwa Jaji Joseph Sinde Warioba,
Ulitueleza kuwa "wananchi walio wengi" walitaka Serikali 3, japokuwa Takwimu zenyewe nazo zina ukakasi mwingi! Hatujasikia kuwa ukilieleza Bunge wakati wa kuwasilisha Rasimu kuwa "wananchi walio wengi" wakitaka "Nchi 3!"
Sasa hayo ya "Nchi 3" umeyapachika kwenye Ibara ya 64 (1) ya Rasimu uliyatoa wapi?
Au kwako "Nchi" na "Serikali" ni kitu kile kile ukiamini tu wananchi 37,000 waliotaka "Serikali 3" walimaanisha "Nchi 3?"
=========
ADDITIONAL 1
=========
Ibara ya 64 inayozungumzia kuhusu Nchi Washirika (Nchi 2) inasema kama ifuatavyo (hiyo nchi ya 3 imeelezwa kwenye Ibara ya 1):
"(1) Kwa mujibu wa Katiba hii, Nchi Washirika ni Tanganyika na Zanzibar.
(4) Nchi Washirika zitatekeleza majukumu yao kwa kuzingatia masharti ya Katiba hii na Katiba zao.
(5) Nchi Washirika zitakuwa na hadhi na haki sawa ndani ya Jamhuri ya Muungano na zitatekeleza majukumu yao kwa mambo yote yasiyo ya Muungano katika mamlaka ya Nchi Washirika kwa mujibu wa masharti yaliyowekwa na Katiba za Nchi Washirika."
Ibara nyinginezo zinazozungumzia Zanzibar na Tanganyika kama "Nchi" ni hizi zifuatazo: Ibara ya 1, 44 na 60 (3).
==========
ADDITIONAL 2
==========
Ukitaka kujua kuwa hizo "Nchi Washirika" zina HADHI SAWA na "Nchi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania" soma Ibara ya 8 (4) inayosema kama ifuatavyo:
"Sheria yoyote, mila, desturi au uamuzi wowote wa chombo cha dola, Ofisa wa Serikali au chombo binafsi ni sharti afuate na kuendana na masharti yaliyomo kwenye Katiba hii na kwamba Sheria, Mila, Desturi au uamuzi wowote ambao hautawiana au kwenda sambamba na masharti ya Katiba hii utakuwa batili."
Hapa zinapozungumziwa Sheria, Mila, Desturi au uamuzi wowote maana yake ni Sheria, Mila, Desturi au uamuzi wowote wa Jamhuri ya Muungano (ie katika mambo ya Muungano) na sio Sheria, Mila, Desturi au uamuzi wowote wa "Nchi Washirika." Zaidi ya hapo Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haijatajwa kuwa ni KUU kupita Katiba za Nchi Washirika! Sasa unawezaje kuwa na MAFAHALI WATATU (3) katika zizi moja? Kwa wapenda Muungano watakubaliana na mimi kwa hili!
Hapa ndio lilipo BOMU la kuulipua Muungano wetu, amini usiamini! Kama Muungano utavunjika (endapo Rasimu hii itakuwa Katiba) basi ni kupitia Ibara hii ya 8 na nyingine nilizotaja hapo juu!
Ulitueleza kuwa "wananchi walio wengi" walitaka Serikali 3, japokuwa Takwimu zenyewe nazo zina ukakasi mwingi! Hatujasikia kuwa ukilieleza Bunge wakati wa kuwasilisha Rasimu kuwa "wananchi walio wengi" wakitaka "Nchi 3!"
Sasa hayo ya "Nchi 3" umeyapachika kwenye Ibara ya 64 (1) ya Rasimu uliyatoa wapi?
Au kwako "Nchi" na "Serikali" ni kitu kile kile ukiamini tu wananchi 37,000 waliotaka "Serikali 3" walimaanisha "Nchi 3?"
=========
ADDITIONAL 1
=========
Ibara ya 64 inayozungumzia kuhusu Nchi Washirika (Nchi 2) inasema kama ifuatavyo (hiyo nchi ya 3 imeelezwa kwenye Ibara ya 1):
"(1) Kwa mujibu wa Katiba hii, Nchi Washirika ni Tanganyika na Zanzibar.
(4) Nchi Washirika zitatekeleza majukumu yao kwa kuzingatia masharti ya Katiba hii na Katiba zao.
(5) Nchi Washirika zitakuwa na hadhi na haki sawa ndani ya Jamhuri ya Muungano na zitatekeleza majukumu yao kwa mambo yote yasiyo ya Muungano katika mamlaka ya Nchi Washirika kwa mujibu wa masharti yaliyowekwa na Katiba za Nchi Washirika."
Ibara nyinginezo zinazozungumzia Zanzibar na Tanganyika kama "Nchi" ni hizi zifuatazo: Ibara ya 1, 44 na 60 (3).
==========
ADDITIONAL 2
==========
Ukitaka kujua kuwa hizo "Nchi Washirika" zina HADHI SAWA na "Nchi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania" soma Ibara ya 8 (4) inayosema kama ifuatavyo:
"Sheria yoyote, mila, desturi au uamuzi wowote wa chombo cha dola, Ofisa wa Serikali au chombo binafsi ni sharti afuate na kuendana na masharti yaliyomo kwenye Katiba hii na kwamba Sheria, Mila, Desturi au uamuzi wowote ambao hautawiana au kwenda sambamba na masharti ya Katiba hii utakuwa batili."
Hapa zinapozungumziwa Sheria, Mila, Desturi au uamuzi wowote maana yake ni Sheria, Mila, Desturi au uamuzi wowote wa Jamhuri ya Muungano (ie katika mambo ya Muungano) na sio Sheria, Mila, Desturi au uamuzi wowote wa "Nchi Washirika." Zaidi ya hapo Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haijatajwa kuwa ni KUU kupita Katiba za Nchi Washirika! Sasa unawezaje kuwa na MAFAHALI WATATU (3) katika zizi moja? Kwa wapenda Muungano watakubaliana na mimi kwa hili!
Hapa ndio lilipo BOMU la kuulipua Muungano wetu, amini usiamini! Kama Muungano utavunjika (endapo Rasimu hii itakuwa Katiba) basi ni kupitia Ibara hii ya 8 na nyingine nilizotaja hapo juu!