Ndio maana nikawashangaa Njiwa na Doula walipoingiza udini badala ya sifa kama alivyosema mleta mada.Tunatamani tuwe na rais mwenye kudhubutu bila kuuma uma maneno pale inapotokea maswala nyeti yanayotishia... kwani swala la kuchinjana na kuchoma nyumba za ibada wewe unaliona ni zuri... udini kwa sasa siyo jambo la kuficha....
Kiongozi yeyote wa ccm ambaye hana udhubutu wa kupaza sauti pale wanyonge wa nchi hii wanapoumia hafai... Kazi yao kulindana tu na kuoneana aibu.
hili jambo la mauaji ya znz na kwengineko ni jambo pana sana! hujui nani katenda na kwa faida gani! kisiasa au kidini? naona mauwaji haya yamekaa kisiasa siyo kidiniNdio maana nikawashangaa Njiwa na Doula walipoingiza udini badala ya sifa kama alivyosema mleta mada. Hata sasa sijamsikia yoyote miongoni mwa wanotajwa kugombea via CCM kuzungumzia kadhia ya udini, kwangu huo ni upungufu mkubwa kiuongozi.
Kwa jinsi siku zinavyopita, Kuna hatari ya nchi kupata Rais 2015 ambaye ni bogus zaidi ya Marais waliopata kuliongoza Taifa tokea tupate uhuru. Jamii kwa sasa imeanza kuona Rais bora ni yule mwenye imani ya dini kama wao bila kujali uwezo wake. Taifa limeanza kuonyesha dalili zote za kuelekea Taifa Mfu. Kwa Watanzania wengine wenye upofu wa fikra, Mwanasiasa mahili ni yule anayepiga kelele majukwaani bila hata ya kujua mipaka ya matamshi yake. Unfortunate, Salim Ahmed Salim hayupo kwenye haya makundi na siyo ajabu, kwa sasa ameanza kuzodolewa kwa sababu kwao, anaonekana hana vazi la Urais.
SAS ni mwanadiplomasia, na msingi mkuu wa kuwa mwanadiplomasia mahili ni kuwa CALM, COLLECTED AND ON BALANCE.
Ni kitu cha kushangaza pale watu wanamtaka aende sokoni kujiuza kama wanaSiasa wengine wanavyofanya kwa sasa. Salim Ahmed Salim hahitaji kwenda sokoni kujiuza kwa sababu kazi hiyo aliisha ifanya siyo kwa Tanzania tu bali hata katika mataifa. Pale alipopewa kazi ya kufanya katika nchi au mataifa, aliifanya kwa uadilifu na ufanisi mkubwa. What more you want!!.
Please Candid Scope , usichanganye bidhaa za kisiasa zinazojiuza kwa sasa na bidhaa iliyojipambanua tayari ndani ya soko la kisiasa.
hili jambo la mauaji ya znz na kwengineko ni jambo pana sana! hujui nani katenda na kwa faida gani! kisiasa au kidini? naona mauwaji haya yamekaa kisiasa siyo kidini
Kauli ya kiuongozi ni muhimu sana, mauaji ni jinai- iwe kidini, kisiasa au kisasi. Kwa hali iliyopo na matukio ya kidini yaliyotukia kabla, tungetarajia Kiongozi/ Mwanasiasa makini atoe hata kauli ya kulaani tu.
Candid Scope Kwanza Hatumtendei haki Salim Ahmed Salim kumuongelea swala la Urais kwa sababu tunajitwika wajibu wake kitu ambacho ni kinyume hata kwenye macho ya haki. Kama atajitokeza na kusema atagombea basi hapo ndipo tunaweza kuanza kumzodoa.Unanasiplomasia ni hatari kwa maana hawako na msimamo wa uwazi, na pengine wanaweza kuwa ndumila kuwili. Uwazi ni mambo ya msingi katika utendaji kisiasa. Utendaji kisiasa ni tofauti na kazi ya kiofisi tu, kwanis unapambana na mengi katika mazingira tofauti bila kuchagua uwanja wa kurusha mpira. Awapo kwenye siasa anatakiwa acheze nafasi zote, picher, catcher and striker, huo ndio ubora wa mtandaji mkuu katika kuongoza nchi.
Tunahitaji rais mwenye kuleta ufafanuzi na kupambanua mambo bila woga, bila haha na kwa uwazi. Anatakiwa aonyesha matatizo tuliyo nayo yamesababishwaje na njia mwafaka za kuyatatua.
Mambo mazito mazito yalimetokea, yanatokea na huenda yataendelea kutokea yanayotikisa nchi, haonyeshi kushtushwa wala kuonea uchungu, yeye amenyamaza tu.
Kizazi cha leo cha watanzania ni cha mfumo wa demokrasia ya vyama vingi, anatakiwa kufugua mdomo tofauti na mfumo uliozoeleka wa chama kimoja kushika hatamu hahitaji kufungua mdomo.
Aaah Wapi,
Mmeshaanza siasa zenu za majitaka sasa,,
Hebu niambie wewe sasa.humpendi huyu kwa chuki zako binafsi au humpendi kwa kuwa yuko CCM??
Akisimama huyo 2015 hatuna budi kumpatia nchi hii,mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni..
Au kwa kuwa ni Muislam??
Mbona Kikwete alipewa,au naye si mwislam? BTW, Jemedali Mwislam Kikwete alimfanyia Zengwe na Fitna Mwislam mwingine Dr Salim A Salim. Hivyo MBWA KALA MBWA. The rest ni chuki na upungufu wa hekima kichwani.
Dr. Salim Ahamed Salim (Tanzania) and Henry A. Kissinger (USA)
Dr. Salim Ahmed Salim ana jina kubwa nchini na kimataifa katika masuala ya kimataifa. He is a diplomatic figure. Naweza kumlinganisha na baadhi ya wanadipolamasia kama Henry Kissinger pamoja na umaarufu wao kimataifa hawakufaa kushika dola katika taifa.
Majukumu mazito aliyowahi kuyafanya kitaifa na kimataifa ni pamoja na:
Pamoja na umaarufu alioweza kuwa nao katika masuala ya kimataifa na kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania:
- Mwenyekiti wa Baraza la Usalama Umoja wa Mataifa
- Katibu Mkuu Umoja wa nchi Za Afrika
- Mgombea Ukatibu Mkuu umoja wa Mataifa - hakupita
- Nafsi ya juu aliyowahi kuishika Tanzania ni kuwa Waziri Mkuu
- Hajaonyesha msimamo wake katika masuala ya kitaifa,
- Hayuko wazi
- Mkimya asiye weza kushirikisha aliyo nayo.
- Pamoja na kwamba ni mwana CCM sijawahi kuona ushirikishaji wa uongozi wake kwa CCM zaidi ya kuwa mhudhuriaji.
- Anaonekana kupokeleka zaidi kwa sura badala ya vitendo na fikra.
- Anaonekana kufaa shughuli za kiofisi zaidi kuliko siasa za majukwani.
Kwa mtazamo huu ana dira gani katika kuongoza Tanzania ya leo kama atagombea urais?
Je, Tanzania tuendelea kunadishwa majina makubwa ya wagombea urais pasipo kuonyesha uwezo wao?
Candid Scope , kwa kweli kumlaumu Salim Ahmed Salim katika siasa za maji taka za siku hizi ni kumwonea tu.
Huyu ni mmoja wa viongozi waadilifu na watiifu mno nchi hii.
Tumeona jinsi alivyoumizwa katika kinyang'anyiro cha urais wa mwaka 2005.
Lakini alivyo mstaarabu hkujibu neno, na yuko kimya kabisa.
Hii ni pamoja na ukweli kuwa alishafikiaa ngazi ya juu kabisa katika uongozi wa Tanzania -Uwaziri Mkuu.
Sasa kumtaka zaidi naona n kumwonea tu, na wala hajatamka kuutaka urais, maana hata kwa kutazama tu waliomuumiza mwaka 2005 ni mitandao ile ile iliyopo.