Waraka wangu kwa JWTZ, Watanzania

Waraka wangu kwa JWTZ, Watanzania

Mkakati uleule unaotumiwa na mafisadi kuepusha maswali magumu kwa wahusika.

Hiki ni kiini macho. Tutaelekeza macho yetu Rwanda ilhali mchwa na majambazi wa kitanzania wakiendelea kuifilisi nchi yetu.

Tutaambiwa tatizo ni Paul Kagame ilhali tuna rais asiyejua kwanini yupo ikulu, mzururaji mahiri, na atakumbukwa (pindi akikubali kutoka madarakani) kwa uongozi wake dhaifu kupindukia.

Waungwana, hiki ni kiini macho. Hivi hamjiulizi UZALENDO wa gazeti la Mtanzania ktk ishu ya DRC/Rwanda unatoka wapi? Kwamba Rostam ana uchungu na Tanzania kiasi hicho? Hawa ni akina Salva Rweyemamu wapo kazini, na wanaelewa udhaifu wa Watanzania: ni rahisi kuwaingiza mkenge!

Mkuu,

Sijui niku-support kiasi gani nieleweke kwa wengine. Kinachofanyika ni plan za magamba aidha kuzolotesha mchakato wa katiba mpya au kuzua vita vitakavyosogeza utawala dhaifu miaka mingine mbele.
 
Manyerere anazungumzia Dola ya Bahima wakati hajui hata hilo kabila ni akina nani!

Masikini mwandishi mjinga. Hajui kuwa propagandists wa hii dola walikuwa wanamwingiza hata Baba wa Taifa Nyerere kuwa yeye ndo kinara anaowatumia vijana wake Museveni na Kagame, sasa na wewe unadandia treni usiojua inakokwenda.

Sipendi kuona mwandishi makini anaandika upuuzi, sipendi kabisa. Nilidhani upuuzi unaandikwa na akina Mtikila au wanaotoa comment humu ambao ni watu tu wa kawaida, hata Manyerere? aliyelelewa na kula nafaka kwa Nyerere? Jamani, uandishi Tanzania unaelekea kubaya.

Manyerere ingia google, tafuta Tutsi, then Hima, then Bairu, then Hutu... then utajua tofauti. Kuhusu vita kuhitimishwa Kigali, nadhani Manyerere amevurugikiwa akiri. Vita Enzi hizi ambazo watu wanaangalia uchumi na kushirikiana?

Ona sasa unazungumzia kuingia EAC ikiwa ni mkakati wa Himaya, huoni Kenyatta ana take advantage ya matatizo yetu kujinufaisha? Wakati tunapiga kelele za empire, kupeleka majeshi kuwasaidi wacheza ndombolo, Kenyatta anazindua bandari na kuweka mpango wa kuhakikisha inatumiwa. We upo tu kwenye Hima empire.

Na hujui kuwa ili upigane vita Enzi hizi lazima ui-convice UN, Marekani, etc. Hujui kuwa Congo iko vile kwasababu kuna dola dhaifu, na kuna utamaduni wa uasi tangu Enzi za Mobutu? Sasa unaleta hadithi za Hima empire hapa, kweli nimekudharau, you are an empty basket.

tatizo lako wewe mnyarwanda una jazba mno,unashindwa kujua kwamba kila mtu anahaki ya kusema yake aliyonayo moyoni,nathani Manyere ajakurupuka tu kafanya uchunguzi, acha hizo propaganda za uko kwenu Rwanda.
 
MukamaMasimba nikushauri tu uache kumshabikia Kagame na kagenge chake cha wahuni...labda kama na wewe ni mmojawapo! Kagame ni mtu dhaifu sana ndio maana hata elimu yake ni ya kuunga-unga.....taarifa zilizopo ni kuwa alikuwa-drop out secondary school, hata mafunzo aliyopelekwa USA kiupendeleo hakumaliza. Hivyo usikubali kuyumbishwa na kiongozi asiye na ufahamu na mbumbumbu...!

Ni kamanda James (Kabarebe) na watu wachache ndio wanaendesha Rwanda sio hata Kagame....! Kamanda James kila mtu anajua ni mwehu, ndio maana pamoja na kutandikwa makofi na Kagame enzi zile Mulindi bado ameendelea kuwa mlamba viatu wa Kagame....tofauti na wenzie wenye kuheshimika ndani ya jeshil la Rwanda...! Ni wehu wake huu Kamanda James aliutumia baada ya kufukuzwa Congo pale alipoenda Ikulu kujifanya anaaga kumbe anataka kumuua Mzee Kabila kwa bastola aliyoficha kwenye kofia kichwani, thanks to mlinzi wa Kabila aliyeamua kumvua kofia na kuiona......! Ni ujasiri huu wa kipumbavu wa Kamanda James alirudi nao Kigali na kumwambia Kagame 'kama unataka kuendelea kuwa kiongozi wetu, niache niandae mashambulizi kuivamia Congo'

Ni Kamanda James na ujinga wake na akina Bizima Karaha na maneno yao ya kipuuzi yalisababisha tena mauaji wa watutsi wasio na hatia Congo....mpaka leo hii kama una shingo ndefu, uwe mrefu mwembamba huwezi kukatiza mitaa ya Kinshasa kwa amani.....wacongoman watakugawana kama fenesi...!

Ni vizuri kama wewe sio mmoja wao uache kumshabikia Kagame na kagenge chake cha wahuni kwa vile anazidi kuweka taswira mbaya ya kabila la watutsi....na kuhatarisha maisha ya wale wasio na hatia...! Nikuhakikishie kuwa mauaji ya halaiki hayatatokea Rwanda kwa vile hata watutsi wanafahamu kuwa adui yao sio wahutu bali watawala wenye tamaa na kukosa ubinadamu kama Kagame.....! Tofauti ya Kagame sasa na ilivyokuwa Habyarimana ni nini...? Cha zaidi Kagame ameua watu wengi zaidi wasio na hatia na pia hataki kuzungumza na waasi, wakati mwenzie angalau alikubali kuzungumza...!

Ni kundi dogo tu la inner-circle ya Kagame na kagenge chake cha wahuni wasiozidi 2,000 ambayo itaathirika kwa sasa

Inshallah....with JWTZ tutakunywa chai Kigali...!

Mkuu huja ni convince hata kidogo,pamoja nahizo shule zake ndie kiongozi aliye na awards kuzidi wate afrika,na ndie aliyeweza kuitoa rwanda katika hali mbaya ya kiuchumi na kuifikisha hapa ilipo,je hao wenye shule ingawa sikubaliani na wewe najua kwamba alijiendeleza na elimu baadaye,lakini he is genius,hayo blablabla ya congo sina muda ya kuyaongelea,lakini kitu nilicho gundua unaakili kama za idi amini,kwani wakati wavita vya kagera alisema chai atainyweya mwanza aka ambulia kipondo mutukula,na wewe naona unandoto kama za nduli kabisa,halafu wewe unaweza kua kati ya wale wafuasi wa kayumba kwani naona unajua ya wakati ule wamapambano ya kabila mkubwa,lakini mengi niuongo mtupu,na hako kadharau ka masomo ??????
 
We ndio umetembea sana au vita ya huko kwenu ndio ilikuleta Tanzania? Watanzania wanatembea sana lakini katika nchi zenye amani kama ya kwao.

Wewe jaribu ufike kigali watu wanatembea na magold na simu za bei mbaya 24hours bila wasiwasi,jaribu bongo kama hawajakutoa shingo! uliza vizuri ni nchi iliyo na amani kuzidi nchi zote katika ukanda huu,we sema unajikanyaga kwasababu unajua ulichofanya rwanda unaogopa kuulizwa,wewe njoo tu uombe msamaha,utubu dhambi zako utasamehewa.
 
Ndg Manyerere shalom ningalipenda kupingana nawe kwenye swala la vita huu sio wakati kwa nchi yetu kukimbilia vita kwani imetugharimu ya uganda na mpaka leo tunafunga mikanda na umasikini wetu , Kuhusu swala la bandari hatuhijitaji kulaumu kenya Rwanda au Burundi, Tunahitaji kujilaumu wenyewe na ukasuku wetu na viongozi wetu pia, Standish wa habari njaa tulio nao ambao hawana uzalendo na nchi yetu zaidi yahoo familia zao.Kuhusu bandari ya Dar es salaam tatizo kubwa ni huduma kwa wateja /rushwa mambo hayaendi yanavyopaswa, mizigo inapokuwa transit mizani usumbufu wa polisi usalama barabarani inachangia mizigo kutofika kwa wakati na kusababisha gharama zisizo za muhimu, Namshukuru Ndg Mwakyembe angalau amewaamsha usingiizini watu wa bandari.

Kuhusu Ndg Rais P Kagame tunabaki kumshambulia kisa hakuwa au hana uhusiano na Ndg Rais Jakaya kikwete hayo Mimi mambo binafsi yao kama viongozi wa nchi mbili tofauti hivyo hatuhitaji ushabiki wa simba na yanga kwenye jukwaa na kuhimiza vita sio mchezo. Je kama ni uuwaji sisi kama nchi hatuhusiki? Wewe kama mwandishi unakumbuka silaha zilizo pitiswaga bandari ya Dar nakupelekwa uganda kusiko julikana yawezekana ndizo za m23?

Hivyo tutoe boriti kwenye jicho letu ndipo tutaona kibanzi kwa Kagame na Mu7 tusiwe wanafiki pia hao Wazungu wa America , ufaransa, ujerumani na waingereza. Hawana Rafiki mzuri au adui isipokuwa yeyote anayekinzana na masilahi ya nchi Yao tuamke tusiwe majogoo wa kushabikia ugomvi kila la kheri Tanzania
 
Tunachopingana hapa ni ushamba wa kukimbilia vita, huu ni ushamba mkubwa tutafaidikaje hasa na vita hii wewe unaweza kutueleza faida za huu upuuzi? nauita upuuzi kwasababu kama mtanzania naona aibu kubwa kushabikia vita nje ya nchi yangu nikifahamu fika watanzania kwa maelfu wanatekea kwa madawa ya kulevya, kufa kwa kukosa huduma bora za afya, elimu duni na hatuelewi tutatokaje huko. Yatupasa kupigania uchumi wetu na sis kushabikia kagomnvi kasiko na mashiko tena kakikuda kati ya mh kikwete na kagame.
Hakuna aliekimbilia vita ila wao tutsi na Pk ndio wanataka vita kwa sababu;
Jk alitoa ushauri bila kutukana wala kumtisha mtu na hata Mbingu imeuona Upendo wake,kama Pk aliona sio sahihi angejibu kiungwana na sio kutisha watu.
 
mambo mengi ktk dunia ya leo ni yakutengeneza.
naam hata hii vita ni yakutengeneza,
mara ya kwanza tanzania tuliikataa AFRICOM. baadae wakaturubuni na(3 D's) yaani defence,deplomas and development. na muda si mrefu kikaundwa kikundi kinaitwa AMISOM,tukakiona kinaingia somalia kwenda kuwatowa al-shabbab.
leo hii kimeundwa kikundi kinaitwa FIB, nacho kipo goma congo kwenda kuwatoa M23.


"ukisikia vita au tetesi ya vita, usiogope kwa maana hayo hayanabudi kutoke"
asema YESU
 
acha unafiki, kwa nini hujakiri kwanza kagame ndiye aliyemuua mzee kabila? Huji wakongo wanachinjwa kama kuku na wahuni wa m 23 ambao wanafadhiliwa na rwanda na kusaidiwa kijeshi na jeshi la rwanda?
well,naweza kuwa mnafiki kwa tafsiri yako,sikatai hicho cheo na sifa...baada ya taarab zako turudi kwenye hoja.Kagame ndio muasisi wa vita ya Kongo?Tukana ukimaliza, jibu swali...
 
Wewe jaribu ufike kigali watu wanatembea na magold na simu za bei mbaya 24hours bila wasiwasi,jaribu bongo kama hawajakutoa shingo! uliza vizuri ni nchi iliyo na amani kuzidi nchi zote katika ukanda huu,we sema unajikanyaga kwasababu unajua ulichofanya rwanda unaogopa kuulizwa,wewe njoo tu uombe msamaha,utubu dhambi zako utasamehewa.

Uko sahihi kwamba hakuna atakayekupora cimu yako lakini pia si useme kwamba Kigali imejaa wanajeshi kila baada ya mita 5 au sivyo? Sasa kama kuna amani inayotokana na mioyo ya watu wenyewe, wale wanajeshi wanalinda nini? Kiuhalisia Kigali hakuna amani ila wananchi wana woga wa hali ya juu kwasabu hata kibaka akipora simu hana pa kukimbilia kutokana na kutanda kwa wanajeshi, dunia tunaijua sana kuliko unavyodhani. watanzania hatukufika Ulaya kwasababu ya ukimbizi au kutaka hifadhi. Ulijue hilo vizuri.
 
PK hanasababu yakupigana na tanzania,unakumbuka minister mshikiwabo alisema watanzania waishio rwanda msiwena wasiwasi mjisikie nyumbani kwani sisi wote ni waafrika na wana east afrika,ungejua jinsi pk anawapenda watanzania,tatizo ni dissapointment iliyo fanywa na mtu mmoja tu ambayo inaleta hili joto,pk anajua anao pigana nao mtazania atapigananaye kwa shida ipi labda mkijaribu kuingia anga zake hapo ata wahit.
Anga zipi?,hizo za DRC,JK alitoa ushauri kama aliona haufau asingetisha,JK ni rais wa tz na sio wa familia,anawakilisha watanzania kila sekta ndan na nje..,ukitaka kujua ilo ampige risasi ndio utajua ni umempiga yeye au watanzania..
 
kwa unyama huu wa rwanda na kiburi cha pk TANZANIA haina jinsi mbali na kuingiza askari rwanda kusimamisha vitisho, dharau, mauji ya halaiki na uporaji wa mali asili ya DRC.

Unaifaham vita wewe? hebu toa sababu za msingi kulifanya taifa kuingia vitan? yaani nyie wachumia tumbo manatuaibisha kweli watanzania tunafikiri very low! wakati wenzetu wanajipanga kiuchumi sisi tunashupalia upuuzi.


Tunamatatizo chungu nzima hapa Tanzania kwa kutumiwa na serikali mmekuwa mazuzu kushabikia vita utazani ni soda mnazifahamu gharama za vita nyie?.
 
Vita inatakiwa kuwa last resort sio kushabikia vita tuu hasa kwa Watz ambao hawajazoea hali ya mapigano ata kama upo sawa katika kila kitu vita inasababisha resources out flow sasa na benefits zake haziko guaranted hasa kwa hizi nchi ambazo hazina power katika maamuzi ya UN
 
Tumeanza kuwatambua watutsi humu JF. Tujadili mada, kejeli na matusi tuviweke pembeni.

Umezungumza mengi na muhimu kaka! Na nakubaliana nawe isipokuwa kwenye suala la vita! Kama kweli tunataka kumtoa Kagame tutafute njia nyingine halali za kumwondoa. Vita isiwe moja ya machaguo yetu!
 
Anga zipi?,hizo za DRC,JK alitoa ushauri kama aliona haufau asingetisha,JK ni rais wa tz na sio wa familia,anawakilisha watanzania kila sekta ndan na nje..,ukitaka kujua ilo ampige risasi ndio utajua ni umempiga yeye au watanzania..

Ushauri wake ulikosa maana pale alipotaka kuitumia fulsa hiyo kimataifa apate umaarufu, kagame ni jirani yake ilimshinda kitugani mh kikwete kumtembelea pale Kigali, au kumpigia simu, au kummualika hapa Dar es salaam waongee kwa upole na maarifa wakiwa wawili? Kilichofanyika ni unafika wala haukuwa ushauri wa heri.

Ukigombana na jirani, au ukiona jirani yako anamatatizo makubwa, huwezi kusubiri jukwaa la siasa kimataifa eti ndo umpe ushauri, huo ni utapeli na haikubaliki kabisa.
 
well,naweza kuwa mnafiki kwa tafsiri yako,sikatai hicho cheo na sifa...baada ya taarab zako turudi kwenye hoja.Kagame ndio muasisi wa vita ya Kongo?Tukana ukimaliza, jibu swali...

vita ya congo ilisukumwa na vita ya burundi na rwanda na baadae makundi ya waasi kama banya mulenge na wengineo kujichimbia congo. kwa hio bado kagame anabaki kama ndie muasisi wa vita ya congo kwa kile kinachoitwa mauwaji ya kimbali.
 
Hakuna aliekimbilia vita ila wao tutsi na Pk ndio wanataka vita kwa sababu;
Jk alitoa ushauri bila kutukana wala kumtisha mtu na hata Mbingu imeuona Upendo wake,kama Pk aliona sio sahihi angejibu kiungwana na sio kutisha watu.

Watu mbona mmekomalia vita? kwani kagame alisema ataishambulia tz au umesikia kwamba wamerundika majeshi mpakani kama vile tz ilivyofanya,hebu acheni kushabikia vita.
 
Ushauri wake ulikosa maana pale alipotaka kuitumia fulsa hiyo kimataifa apate umaarufu, kagame ni jirani yake ilimshinda kitugani mh kikwete kumtembelea pale Kigali, au kumpigia simu, au kummualika hapa Dar es salaam waongee kwa upole na maarifa wakiwa wawili? Kilichofanyika ni unafika wala haukuwa ushauri wa heri.

Ukigombana na jirani, au ukiona jirani yako anamatatizo makubwa, huwezi kusubiri jukwaa la siasa kimataifa eti ndo umpe ushauri, huo ni utapeli na haikubaliki kabisa.

kama ulikuwa hujui feedback ya kagame imeshaanikwa na generali nkunda.watu wanamjuwa pk kuanzia unya mpaka unye.
 
Magwiji wa vita kama akina General Msuguri watakuwa wanashangaa jinsi tunavyoijadili Rwanda Vs JWTZ!!!
Kagame anajua nini kinaweza kufata akishambulia vikosi vyetu.Nawahakikishia kwa uzoefu wa Kagame kuhusu JWTZ hawezi kufanya kosa kama hilo kamwe!!
Bila JWTZ hata Mobutu wasingemuweza!!!
 
kama ulikuwa hujui feedback ya kagame imeshaanikwa na generali nkunda.watu wanamjuwa pk kuanzia unya mpaka unye.


Hizi ni njaa zinawasumbuwa nyinyi, haiwezekani mtanzania na akili zake timamu aache shida zake kwake nyumbani akomalie matatizo katika nyumba ya jirani yake.

Nyinyi mnaoshabikia upuuzi huu na kutotowa watanzia nje ya mambo muhimu tusijadili haki zetu ninamashaka na uwezo wa akili zenu. Acheni kutupotosha watanzania turudi kuyatazama mauzauza ya shida zetu
 
Kuna wanyarwanda na Pro Kagame lukuki humu JF ,Subiri utawaona miongoni mwao ni

@R.B
@Adolay
@Koba
@Mukamasimba
Mkuu, mbona haujamtaja RUTAJUMBUKURWA? Kajivika jina la kihaya ili kuuficha ukweli ya kuwa yeye ni mnyarwanda!
 
Back
Top Bottom