Waraka wangu kwa JWTZ, Watanzania

Waraka wangu kwa JWTZ, Watanzania

Huu sasa ni upuuzi naanza kuona watanzania tunapoteza mwelekeo. Mtu akipinga vita dhidi ya Rwandatayari yeye ni mtusi. Hizi ni fikira zilizopotoka
 
Unaonaje ukaanzisha mada yako,mimi sio ccm..

Siyowewe uliyesema waasi wote wanyang'anywe silaha kule DRC, swali likaja hapa kwetu tanzania, wale wanaopiga risasi mapadri, kuuwa shehe kule zanzibar, kumwagia tindikali mashekhe kule Arusha na zanzibar, kulipuwa mabomu kwenye mikusanyiko ya kisiasa na kutesa watanzania kama vile kibanda na ulimboka mmefikia wapi kiasi kwamba sasa Tanzania ni safi hata mkrupuke kuenda DRC? au Kuitaka vita na Kagame? Msitufanye watanzania wajinga sawa we mlamba viatu wa magogoni! kama huna majibu bora kukaa kimya acha uzezeta.
 
Zipo sababu nyingi zinazomfanya Rais Kagame awe mbogo. Nitajaribu kuziainisha hapa kwa ufupi tu. Mosi, Tanzania tunakubalika sana kimataifa. Kwenye diplomasia tumeiacha mbali Rwanda. Hili linamuudhi sana kwani anaamini yeye ni bora na maarufu zaidi.

Kitendo cha Rais Barack Obama wa Marekani kuja Tanzania na kuziacha Rwanda, Uganda na hata Kenya kimewaudhi, na kwa kweli tunaweza kusema hii imekuwa nguzo imara iliyoibua mshikamano na mapenzi ya ghafla miongoni mwao. Rwanda ikijiona kuwa ndiyo nchi inayoinukia kiuchumi kwa kasi, ilidhani ina sifa zote za kuiwezesha kutembelewa na Rais Obama. Uganda ambayo ilikuwa mshirika mkuu wa Marekani, inaona Tanzania imechukua nafasi yake. Imeingiwa wivu! Kenya ambayo inaamini Obama ni wao kwa sababu babake ni Mkenya, imechukizwa kuona ikipigwa kumbo na Tanzania. Hawa watatu-Kagame, Museveni na Kenyatta-wameungana kuichukia Tanzania kwa sababu tu ya kumkosa Obama.

Pili, kinachomsumbua Rais Kagame na washirika wake ni uamuzi wa Tanzania wa kutaka Shirikisho la Kisiasa la nchi wanachama wa EAC liende hatua kwa hatua. Msimamo wa Tanzania umekuwa kwamba maoni ya wananchi ni muhimu mno kabla ya kuchukua uamuzi wowote. Kwao, Tanzania ndiyo kikwazo cha kuwa na serikali moja ya EAC. Hapa ni vema Watanzania wakakumbuka namna Rais Museveni alivyokuwa amejiandaa kuwa Rais wa Kwanza wa Shirikisho la Afrika Mashariki. Sidhani kama ameshaufuta mpango huo.

Baada ya kuona Tanzania tukitaka jambo hili liende hatua kwa hatua, watatu hawa wameungana sasa kutaka shirikisho lao la kisiasa, huku wakiiacha nje Tanzania na Burundi. Wanajidanganya bure. Lakini hapana sababu ya kulumbana nao. Kama wanataka kuanzisha, waanzishe tu. Hakuna haja ya ugomvi. Wakianzisha kutakuwa na nchi mbili-hiyo ya Shirikisho, na Tanzania kwa upande mwingine.

Hapa ni vema kwanza tukatambua kuwa Tanzania ni nchi kubwa. Ukichukua Rwanda, Burundi, Uganda na Kenya, ukaziweka pamoja, bado ni ndogo kwa Tanzania. Hatuna sababu ya kuogopa.

Tatu, hawa jamaa kiu yao kubwa kabisa ni ardhi ya Tanzania. Ukiacha tamaa ya kutaka kuitawala kanda yote hii, kiu yao ya kweli ni ardhi ya Tanzania. Wamepambana kwa hali na mali kuhakikisha kuwa ardhi inakuwa moja ya mambo kwenye shirikisho. Wanataka Mkenya, Mganda, Mnyarwanda na mwanachama mwingine yeyote, akitaka kuingia Tanzania, basi apewe uraia wa kudumu na apata ardhi bila masharti!

R.I.P Mshindo,
nimesoma hii post kwa uzuri kabisa...nilichoona zaidi ni kama ya uchochezi flani hivi...kwanza inamaanisha nini safari ya goma ihitimishwe kigali?(huu ni uchochezi) dunia ya sasa si ya vita tuna mambo mengi sana ya kupigana nayo...kwanza hatutaweza kupata muda wa kufikiria vita wakati adui technologia na biaashara vinatungoja...sababu ulizotaja kuna ambazo nakubaliana nazo ila nyingine naona kaka mipasho flani ya taarabu...acha utani hapa tunajadili na watu wenye akili zao...baadhi ya maneno kama ailye muua marais wa burundi na rwanda ni madai yenye kudhibitishwa na mahakama...watu weledi hatuwezi zungumzia hayo mambbo kiushabiki tu maana repercussion yake inaweza ikawa si nzuri hasa utakapoambiwa utoe ushahidi...pia nahisi Congo ina makundi mengi sana ya waasi ikiwa ni wale waloasi rwanda,burundi,uganda,na mengine mengi ni ya congo yenyewe (wenzao na M23) mbona congo isiwafukuzie mbali hao waasi zaidi ya kuwaacha waendelee kuumiza amani? si dhani JK kuomba mseven asaidie kumaliza mvutano si kubembeleza bali ni hatua ya kiungwana sana...pengine huoni maana kwa sababu si muungwana....sioni kwanini tuache hili soko la watu milion 130 kwa sababu za kisiasa tuu...ni soko kubwa..ni majirani zetu hatuna haja ya kufikia huko kote...

KWA MAONI YANGU SURUHISHO NI MAZUNGUMZO NA SI VITA...SIONI HAJA YA VITA KWA SASA
 
Siyowewe uliyesema waasi wote wanyang'anywe silaha kule DRC, swali likaja hapa kwetu tanzania, wale wanaopiga risasi mapadri, kuuwa shehe kule zanzibar, kumwagia tindikali mashekhe kule Arusha na zanzibar, kulipuwa mabomu kwenye mikusanyiko ya kisiasa na kutesa watanzania kama vile kibanda na ulimboka mmefikia wapi kiasi kwamba sasa Tanzania ni safi hata mkrupuke kuenda DRC? au Kuitaka vita na Kagame? Msitufanye watanzania wajinga sawa we mlamba viatu wa magogoni! kama huna majibu bora kukaa kimya acha uzezeta.
Me mlamba via2,wewe unalambwa nin mpaka ukawa fish,sema usifanywe mjinga na sio usimamie watanzania while wewe mtutsi mjinga..,maendeleo ya nchi yako palepale hata kama Pk atajipendekeza
 
Kagame hajagombana na Tanzania wamepishana maneno na JK, na wamemwomba Museveni awapatinishe, aidha maelekezo ya UN, Waziri Membe aliyatolea ufafanuzi mzuri tu ni kuhakikisha hakuna movement ya M23 au RPF kati ya mpaka wa Rwanda na DRC na Marekani walitaka wapeleke drones kwa ajili ya uchunguzi wa military movement across the border sasa wewe unaposema waishambulie Rwanda na waishie Kigali ni kwa maelekezo ya nani? Bila shaka wewe umezaliwa baada ya vita ya Tanzania na Uganda na sidhani kama JKT ulipitia, usingetoa mapendekezo haya, or else watu mnatumika kutaka ku divert attention yetu ya 2015 msingizie kuna vita msogeze mbele uchaguzi hatutaki na hatupigani na mtu!
 
Manyerere Jackton

Bila samahani kwa makala ndefu. Ulichokiandika ni sahihi na ukweli, mwingine nilikuwa siujui, asante kwa kunielimisha!

Sasa namjua vizuri huyu Kagame, kuwadi wa vita! Au tumwite Bwana wa Vita? (Lord of War)

Kweli, kuna faida kubwa kwetu kujitoa EAC kuliko kubaki. Hasara itakuwa kwa Rwanda, Uganda na Kenya, wapinge au wakubali.

Nia tunayo, uwezo tunao, sababu TELEEEEEEEEEEEEEEEEEE tunazo! Tunangoja nini kuondokana na UPUUZI HUU wa EAC?
 
Last edited by a moderator:
Manyerere, mara nyingi nilikuwa nikitofautiana na wewe katika masuala mbalimbali, hasa tunapozungumzia siasa za ndani ya nchi yetu tz, kwa leo nakuunga mkono na kukupongeza kwamba umeona mbali hadi kufikia kuachana na mawazo finyu ya kuwapaka mafuta viongozi hata kama hawajaoga!

Nakubaliana na wewe kwamba tufike mahali kama binadamu tuwe na huruma kwa mama zetu, binti zetu, watoto wetu, wazee wetu wanaoteseka nchini mwao, kisa tu ulafi wa watu wachache wenye uchu na kijicho, namaanisha kina Kagame.
Sote tunaielewa vyema historia ya Kagame na kikundi chake, madhambi yake na mbinu chafu anazotumia kuficha madhambi yake, ikiwa ni pamoja na kuwaua wanaojitokeza kumpinga na au kusema ukweli wanaoujua juu ya chanzo halisi cha mauaji ya kimbari Rwanda na Burundi 1994, anawaua ili kujaribu kuifanya dunia isijue ukweli ambao kwa hakika pamoja na juhudi zake bado ameshindwa kuzuia kabisa (ukweli) kujulukana. YEYE NI MUUAJI NA ANATAMANI SANA AWAUE WOTE WASIOKUWA UPANDE WAKE, WAWE NDANI AU NJE YA MIPAKA YA NCHI YAKE.
Bwana Ruta binafsi sikufahamu vizuri, ila kutokana na hoja lukuki zisizo na mashiko ya kimantiki ulizozitoa hapa, tena kwa jazba, umenifanya nitamani kukufahamu vizuri ili si tu nibaini chanzo cha wewe kuwa na fikra za kumtetea Kagame, dictator, katili, mtesaji na muuaji wa raia wake mwenyewe, bali pia niwafamishe wasomaji na jamii ya watz kwa ujumla kwamba wewe ni nani na kwanini huna huruma na raia wa DRC wanateseka katika nchi yao!
Upande wa Kagame, inavyoonekana sasa, anaweza kujidanganya hata kujaribu kumdhuru rais wetu kwa namna yoyote ile, namtahadhalisha, watz asiwaone wanamshambulia JK kwa uongozi mbovu ukadhani tumegawanyika, tia mkono uone umoja wetu, SIS tunakosoana ili tujenge nchi iliyobora zaidi, lakini kamwe hatuko tayari kuona jirani zetu wananyanyasika na kuvurugwavurugwa na Kagame halafu tukakaa kimmya, akifanikiwa DRC atahamia Tz na hata Kenya na kwingineko!
hebu TUUNGANE KUMPINGA KAGAME na genge lake, na si wanyarwanda wa kawaida, wao pia ndg zetu. Ikibidi KAGAME ang'olewe kama alivyong'olewa dictator mwenzie Idd Amini Dada!
 
Kagame hajagombana na Tanzania wamepishana maneno na JK, na wamemwomba Museveni awapatinishe, aidha maelekezo ya UN, Waziri Membe aliyatolea ufafanuzi mzuri tu ni kuhakikisha hakuna movement ya M23 au RPF kati ya mpaka wa Rwanda na DRC na Marekani walitaka wapeleke drones kwa ajili ya uchunguzi wa military movement across the border sasa wewe unaposema waishambulie Rwanda na waishie Kigali ni kwa maelekezo ya nani? Bila shaka wewe umezaliwa baada ya vita ya Tanzania na Uganda na sidhani kama JKT ulipitia, usingetoa mapendekezo haya, or else watu mnatumika kutaka ku divert attention yetu ya 2015 msingizie kuna vita msogeze mbele uchaguzi hatutaki na hatupigani na mtu!

Ukiona moshi jua kuna moto. Mwenzio akinyolewa, tia maji kichwani. Wala usimtetee huyu NDULI aliye sawa na Iddi Amin! Anautaka sana utajiri wa DRC na Ardhi ya Tanzania!
 
Manyerere anazungumzia Dola ya Bahima wakati hajui hata hilo kabila ni akina nani!

Masikini mwandishi mjinga. Hajui kuwa propagandists wa hii dola walikuwa wanamwingiza hata Baba wa Taifa Nyerere kuwa yeye ndo kinara anaowatumia vijana wake Museveni na Kagame, sasa na wewe unadandia treni usiojua inakokwenda.

Sipendi kuona mwandishi makini anaandika upuuzi, sipendi kabisa. Nilidhani upuuzi unaandikwa na akina Mtikila au wanaotoa comment humu ambao ni watu tu wa kawaida, hata Manyerere? aliyelelewa na kula nafaka kwa Nyerere? Jamani, uandishi Tanzania unaelekea kubaya.

Manyerere ingia google, tafuta Tutsi, then Hima, then Bairu, then Hutu... then utajua tofauti. Kuhusu vita kuhitimishwa Kigali, nadhani Manyerere amevurugikiwa akiri. Vita Enzi hizi ambazo watu wanaangalia uchumi na kushirikiana?

Ona sasa unazungumzia kuingia EAC ikiwa ni mkakati wa Himaya, huoni Kenyatta ana take advantage ya matatizo yetu kujinufaisha? Wakati tunapiga kelele za empire, kupeleka majeshi kuwasaidi wacheza ndombolo, Kenyatta anazindua bandari na kuweka mpango wa kuhakikisha inatumiwa. We upo tu kwenye Hima empire.

Na hujui kuwa ili upigane vita Enzi hizi lazima ui-convice UN, Marekani, etc. Hujui kuwa Congo iko vile kwasababu kuna dola dhaifu, na kuna utamaduni wa uasi tangu Enzi za Mobutu? Sasa unaleta hadithi za Hima empire hapa, kweli nimekudharau, you are an empty basket.


samahani Manyerere,
Huu waraka umeandika wewe au mtu katumia account yako? Huwezi kuwa mjinga Kaisi hiki nonono! nilipenda sana kusoma article zako hii imenitia kichefu chefu! Kwanza data hazina source na not analytical as used to be. Story ni moja umejaribu kuunga unga hadi uwongo unakuwa wazi. Hebu tuliza kichwa na hata Kama unatamani vita vya kumtoa kagame vitokee jenga Hoja sawasawa siyo kujiharishia bila kuchamba no fact mwanzo hadi mwisho ni hisia na uzushi.

kama umelipwa na FDLR kuwasemea basi waombe na data, acha kumtumia Meja Mshindo Kuseek sympathy tuko msibani sisi.
 
We kweli kilaza nikushawishi kwani nakuomba mchango wa harusi,siko hapa kukusanya maoni wewe kama unafikir nipo kukushawishi imekula kwako,muda ukifika utajua umepangiwa kuokota kuni,kupiga kwata au kubeba masufuria,wengine mnavipaji humu..

Kwahiyo hizo ulizoandika ndiyo sababu za kuigia vitan? Mulugo katuchafulia Taifa kweli kweli ndiyo haya ya naibu waziri kutamka muungano wa Tanganyika na Zimbabwe. Kijana namuuliza sababu za kutuingiza vitani anajibu tofauti kabisa.
 
Manyerere, nilikuwa napenda sana kusoma makala yako Rai, na nilikuwa nakuona mwandishi mahiri sana, nilikupenda, ila leo ume-ni disappoint, najua hapa utapata kudos nyingi kwasababu ya aina ya watu wanaojadili mijadala hapa, lakini sikutegemea kuwa mwandishi wa hadhi yako achochee vita na nchi jirani, hii haipo duniani mwandishi wa habari kuchochea vita waziwazi, fanya utafiti. Kisha unakuja na himaya ideology, hii nimeifanyia utafiti na nita-post walaka original ambao umekuwa ukitumiwa kueneza hii campaign

They do in USA, put your fact right!
I'm not saying if is right or wrong but they do.

Next,mtoa maada anaongelea kwa manufaa na usalama wa Taifa la TZ(patriotism)...ndio maudhui makuu ya maada yake.

And you bring issues over substance..
 
Haya mawazo ni ya hatari nadhani busara zitumike na zikishindikana ndio tufikirie tofauti.
 
Humu JF kuna watu wanaotumia jukwaa kufikisha chuki zao za kihistoria, Kwa mtanzania wa kawaida hawezi kuwa na chuki Kwa Rwanda Kaisi cha waraka huu wa Manyerere. Katika waraka wake na baadhi ya wanao unga mkono utaona kuwa wanachuki special na Tabaka la watutsi na siyo wahutu ambao ndiyo jamii kubwa Rwanda. Kwa Mtanzanai halisi ni vigumu sana kuchagua tabaka la watutsi tu ndiyo ukawachukia lazima uwe umeshiriki machungu Yao. Bila kumung'unya Manyerere either ni muhutu mmoja wa familia ya Ntarahamwe zilizoingia Tanzania 1994 kajifunza Kiswahili vizuri na kubadili Jina ili asijulikane, sasa anatumia ugomvi huu wa Congo kupambisha moto, Tanzania ipigane na Rwanda akina kagame watoke ili arudi kwao bila kesi za mauji. Watu wengi wakisikia mnyarwanda wanadhani ni wale wembamba wenye pua ndefu tu na wanasahau kuwa wegine ni wafuasi na puam fupi wanajiitam waha.
 
@Manyerere Jackton nenda na wewe ukafe kishujaa! mnaniboa sana wabongo mnavyochochea huu ugomvi! ndugu zetu wanakufa, eti mnasema wamekufa kishujaa, kishujaa? "kishujaa my ass" kwanini na wewe usiende ukafe kishujaa!

kumbe upeo wako wa kuelewa mambo mdogo khaa, umesikiliza taarifa ya habari leo msemaji wa jeshi zanzibar akiwaambia wafiwa kuwa wasisikitike sana kufa ndugu yao ni jambo la kawaida jeshini

jeshi unaingia kwenda kupigana vita na kwenye vita kuna kufa na kupona!!
 
Mkuu Manyerere ahsante kwa kutuwakilisha.watz wengi tuna mawazo kama yako.hawa watu si wa kuchekea.nawajua vizuuri sana.tuwe wakali sana juu ya hili.Jk asirudi nyuma juu ya hili.mie nasema EAC haitufai kabisa.tuungane na Congo,Burundi,zimbabwe,zambia n.k.hawa wenzetu nyerere aliwashindwa si bure,wanafiki hawa,hawafai na hatufanani nao hata social behaviours,we sikiliza kila siku majambazi wakikamatwa ni wakenya,wanyarwanda,wananchi hatuwataki!kwa hili jk kanikuna sana.
 
@Manyerere Jackton nenda na wewe ukafe kishujaa! mnaniboa sana wabongo mnavyochochea huu ugomvi! ndugu zetu wanakufa, eti mnasema wamekufa kishujaa, kishujaa? "kishujaa my ass" kwanini na wewe usiende ukafe kishujaa!

hapo alichokosea kusema meja amekufa kishujaa ni wapi?? au basi matusi kejeli na chuki. huna la kusema nyamaza.
 
Tumeanza kuwatambua watutsi humu JF. Tujadili mada, kejeli na matusi tuviweke pembeni.
Manyerere Jackton ni kichaaa,,,,, huwezi kuzungumza ubaguzi wa waziwazi namna hii halafu ukaendelea kujiita muandishi wa habari. This is pathetic, poor you, unaendeshwa na jazba na mihemko badala ya thinking. Hihi sio zama za ubaguzi wa kikabila, inaelekea ukiwamaliza waTusi utatugeukia wabena. Shame on you broda.
 
@Manyerere Jackton nenda na wewe ukafe kishujaa! mnaniboa sana wabongo mnavyochochea huu ugomvi! ndugu zetu wanakufa, eti mnasema wamekufa kishujaa, kishujaa? "kishujaa my ass" kwanini na wewe usiende ukafe kishujaa!

We wawapi? Askari shujaa anafia vitani, acha zako
 
manyerere lazima utakuwa mwehu wewe,na sijui kwanini Jf wamekuachia umwage sumu zako humu na mnaomshangilia nina wasiwasi na kama vichwa vyenu ni vizima na nyie.
 
Manyerere Jackton ni kichaaa,,,,, huwezi kuzungumza ubaguzi wa waziwazi namna hii halafu ukaendelea kujiita muandishi wa habari. This is pathetic, poor you, unaendeshwa na jazba na mihemko badala ya thinking. Hihi sio zama za ubaguzi wa kikabila, inaelekea ukiwamaliza waTusi utatugeukia wabena. Shame on you broda.

manyerere lazima utakuwa mwehu wewe,na sijui kwanini Jf wamekuachia umwage sumu zako humu na mnaomshangilia nina wasiwasi na kama vichwa vyenu ni vizima na nyie.

Wahamiaji haramu na wazawa hatuwezi kuwa na lugha moja no matter what!
 
Back
Top Bottom