Waraka wa Tambwe Hizza kwa watanzania

naona kama najishusha kumdiscuss tambwe,..makamba alivyofukuzwa alipewa gari huyu juha alipewa nini?anatamani kurudi upinzani lakini anaogopa nani atampokea wakati alishawatukana..chama kinachoweza kupokea majitu kama haya ni ccm tu ilimradi apige propaganda
 
Richard Tambwe Hizza amechanganyikiwa na sasa anajaribu kutaka kuwatupia watu taulo au kwa kiingereza wanasema "throwing a towel".

Kutupa taulo ni kitendo cha kukubali kusamlimu amri kwamba umeshindwa na hata ulingoni mmoja wa mabondia ambae huona kwamba amezidiwa huamua mwenyewe kutupa taulo kuonysha ishara ya kushindwa.

Ukianza kufikiria jambo la kutupia CHADEMA taulo basi unakuwa umekubali kushindwa.
 
Huyu jamaa anajua kuwa alichoandika ni upuuzi mtu lakini tumsamehe, kafanya hivyo ili aonekane na mabosi wake kwamba nae kaongea kitu katika hili sakata. Anazidi kudhihirisha umbumbumbu wake pale anaposema Chadema wanahusika na mauaji ya Mwangosi huku akijua dhahiri ni nani aliyefikishwa mahakamani kwa kosa la mauaji au anataka kusema Chadema wana FFU wao walioenda Nyololo siku ya tukio?
 
( By Munambefu Huyo ndiye kiongozi anayetegemewa na CCM kukijenga chama!Anafikiri kwa kutumia tumbo au masaburi kama kawaida yao.Niliwahi kumsikia kwenye mkutano mkubwa wakati akiwa CUF pale temeke akisema "sitarudi CCM labda nimlale mama yangu"na sasa yupo huko,je huyu si punguani?Haraka ameshasahau kwamba CCM ilizindua kampeni huko bububu,hakukuwa na sensa?si Tz?polisi ni wa upande wa bara tu?Njaa mbaya jamani mhurumieni)

ye hajui kuwa hata dini zinakataza iyo ya kwenye red, ss haya ndiyo madhara yake. nampa pole huyo mama aliyenaniliwa na mwanae.
 
huyu Tambwe hiza sina hakika kama zinamtosha, watu kama hawa ndiyo waliostahili kuishi milembe kuliko hao walioko huko.
 
Tambwe Hizza naona sasa uananza kuibuka Upya baada chama cha Mapinduzi kukugeuza Vuvuzela kwa muda mrefu na kukutelekeza Mabwe pande naona umeibuka baada ya kupata msamalia mwema je utaweza kumpiku vuvuzela Nape maana yeye alianza na kujivua Gamba hadi leo Gamba limegangania mwilini kama jumba la Kobe tunakukaribisha tulikusahau wewe unaibuka nahili wana Jf tumkaribishe na mikono miwili kwa maana kupitia runinga walimpiga chini.
 
NA RICHARD TAMBWE HIZZA

WIKI hii waandishi wa habari kutoka katika vyombo mbalimbali nchini waliandamana kulaani kuuawa kwa mwandishi wa habari wa Kituo cha Chanel 10 huko Iringa, kifo cha mwandishi huyu kwa bahati mbaya na kwa mara nyingine tena kimewagawa wananchi katika makundi yanayotofautiana kifikra kuhusu chanzo na hatimaye kufariki kwake.

Wapo wanaoona na kuamini polisi wametumia nguvu kubwa katika kukabiliana na tatizo lililokuwepo, wapo wanaoamini kwamba jeshi la polisi lilikuwa linatimiza wajibu wake na madhara haya makubwa yaliyotokea yanatokana na CHADEMA kuendeleza ghasia katika nchi na kujaribu kuifanya isitawalike kama walivyoahidi baada ya kushindwa vibaya katika uchaguzi mkuu uliopita (walishinda viti 23 kati ya majimbo 239).

Hata hivyo, kabla ya kuingia katika tafakuri pana zaidi zinazotokana na msiba huu sina budi kutoa pole kwa familia ya Mwangosi, waandishi waliokuwa karibu naye katika kufanikisha majukumu yake ya uandishi wa habari, Kituo cha Channel 10 na Watanzania wote kwa ujumla, kwa kuondokewa na mwananchi mwenzetu katika mazingira ambayo wote hatukuyategemea.

Tumeshuhudia wakati taifa likiwa katika simanzi nzito kutokana na msiba huu, wapo wenzetu walioamua kuutumia kama turufu ya kuleta chuki baina ya jeshi la polisi na waandishi na zaidi umma wa Watanzania ambao usalama wao na mali zao unategemea sana uwepo wa jeshi hilo. Kuna mambo mengi ambayo nimekuwa najiuliza na ningependa Watanzania wote tujiulize, hivi ghasia zilizosababisha msiba huu zilisababishwa na nini/nani?

Je kulikuwa na ulazima kwa CHADEMA kukaidi amri ya polisi ya kusubiri sensa ipite? Je, ukaidi wa CHADEMA siyo chanzo cha maafa yaliyotokea na yanayotokea mara kwa mara nchini? Je, ingekuwa sawa kwa jeshi la polisi kuwaachia CHADEMA kufanya shughuli ambayo walikwisha wazuia wasiifanye? Je, polisi ingewaachia kufanya jambo ambalo walikwishawazuia wangekuwa wanatimiza sheria na wajibu wao? Na je, uhalali wa uwepo wa jeshi hilo ungeendelea kuwepo?

Wananchi wote tunapaswa kuheshimu sheria na polisi wana jukumu la kutulazimisha kufuata sheria tunapozikiuka vikiwemo vyama vya siasa, najua sheria ya vyama vya siasa inavipa fursa vyama kufanya maandamano na mikutano baada ya kutoa taarifa polisi, lakini sheria hiyo hiyo inasema vitafanya hivyo endapo tu kama havitapata amri pingamizi kutoka polisi (sheria ya vyama vya siasa 1992 kifungu cha 11).

Tujiulize kulikuwa na ulazima gani kwa CHADEMA ambao mwaka mzima wamekuwa wakiruhusiwa kufanya mikutano na maandamano kulazimisha kufanya mkutano uliosababisha kifo baada ya kupata amri pingamizi? Kama waliona polisi hawakuwafanyia haki je ilikuwa vyema kuandaa mapambano dhidi ya polisi? Jje walichukua hatua yoyote ya kisheria dhidi ya polisi au hawana imani na vyombo vya kisheria kama ambavyo Tundu Lissu anavyoziponda mahakama zetu bila kuheshimu kwamba zilimpa ushindi yeye binafsi katika kesi yake ya uchaguzi aliyofunguliwa na mgombea wa CCM, na zile zilizokipa ushindi chama chake zilizowavua ubunge wana CCM huko Sumbawanga na Igunga.

Naamini ili jeshi la polisi liweze kuendelea kulinda amani ndani ya nchi ni lazima tuliamini na lazima tujue kwamba lipo, likizuia jambo kwa mujibu wa sheria wote tuheshimu vinginevyo litakuwa halina sababu ya kuwepo. Si mara moja au mbili mamlaka za umma na vyombo vya sheria viliamua mambo muhimu katika maendeleo ya taifa, lakini yalipata upinzani hadi pale polisi ilipotumia nguvu kuhakikisha sheria inafuatwa na utekelezaji wake unatimia.

Je, kumfukuza waziri katika hafla ya kulaani mauaji na kumkaribisha mwana-CHADEMA Dk. Lweitama kuhutubia na kuilaani serikali ni sawa? Je, ni sawa kulilaumu jeshi zima la polisi kwa tatizo lililojitokeza sehemu moja ya nchi tena katika kutimiza wajibu wao? Kitendo cha kutowalaani walioanzisha uvunjaji wa sheria uliosababisha ndugu yetu Mwangosi kupoteza maisha katika umri mdogo kinaashiria nini kutoka katika taasisi zetu za habari?

Hapa ndiyo maswali mengine yasiyo na majibu yanapoanza, kwa nini tamko lililotolewa na CHADEMA na lile la wanahabari yanashabihiana. Kwa nini wanahabari hawakuilaumu CHADEMA hata mara moja kwa kutokutii sheria na kuanzisha ghasia zilizosababisha maafa ya ndugu yetu. Nadhani tunahitaji tafakuri pana zaidi. Je wametumwa? Wana hasira? au nao wameanza kushirikishwa katika ajenda za siri dhidi ya serikali na vyombo vyake?

Wote tumesikitishwa na msiba huu sidhani kama ni vyema kuendelea kushambulia jeshi la polisi bali kuangalia nani ameanzisha sokomoko ili awajibishwe kisheria, kama ikibainika aliyeua ni raia wa kawaida sheria ichukue mkondo wake, pia ikibainika muuaji ni askari akiwa katika kutimiza majukumu yake ni vyema taratibu za kijeshi na mahakama zitumike badala ya kuendeleza chuki zisizo na msingi.

Tusijisahau wote tunawahitaji polisi kama ambavyo tulikuwa tunamhitaji ndugu yetu Mwangosi nikiwemo mimi niliyeshirikiana naye katika shughuli mbalimbali. Tusiwe na hasira maana wahenga walisema hasira hasara. Tutafute suluhisho la yanayotokea yasijirudie.


Wakati mwingine njaa isitiri kidogo ili usiumbuke na kuonyesha ufinyu wa fikra au kiufisha fikra yako na kuishia kuwa intellectual zombie. Tambwe umesahau kuwa ulipiokuwa CUF ulikuwa unazunguka bar za Temeke mfano Bulyaga na Zebra unatukana polisi ukiwa under frustrations basda ya kuuza kila ulichokuwa nacho ili upate ubunge. Sasa ulivyorudi CCM na kufanikiwa kuwa vuvuzela lao leo hii unaona polisisiem ndio watu wazuri. Shame on you. What you are doing is a boomerang na CCM baada ya kukutumia sasa wamekuacha. You are now a common soldier na sio muda muda mrefu you get fliction na polisi unaowatetea ambao hata polisi wenyewe wanawalaumu kwa kutumia nguvu bila sababu. Siku litakapokukuta usije kulalamika. How can you blame death to CDM ambao hawakuwa na silaha. Askari kaua halafu unataka kutuaminisha kuwa CDM ndio walaumiwe. Kazi ya CDM kueneza siasa, mikakati na ukombozi kwa wananchi. Kazi ya polisi ni kulinda usalama wa raia sio kuua usalama wa raia. Na ndio maana askari mwingine ambaye dhamira ilimsuta alijitosa ndani ya maaskari wakatiri ili amnusuru marehemu. Sasa unasemaje mambo ya ajabu?
 
Hivi Tambwe HIZA yupo duniani?
Yupo chama gani nimemsahau kabisa toka afukuzwe NCCR ya mrema na akaenda Sijui TLP Na kurudi kwao chama kwa ufisadi then anataka kurudi kwa kutumia jina la mwongosi huyu ni mnafiki mtupu hana chake hapa na ukweli anaujua moyoni mwake na kama ndugu yetu mwongosi angekuwa mmoja kati ya familia yake angeongea nini juu ya kifo kigumu na chakusikitisha kama hicho?

f.........., k...........
 
Huyu kilaza si ndio aliwabeba watoto kuwapeleka karimjee kuziba nafasi?Hv zimo kweli au kawehuka?.....product za nepi zipo kinepi nepi tu...eti tambi hizo,shame on you.
 
huyu Tambwe hiza sina hakika kama zinamtosha, watu kama hawa ndiyo waliostahili kuishi milembe kuliko hao walioko huko.

..........mie nimesoma kama paragraph mbili kisha nikashindwa kuendelea, yaani naogopa kuambukizwa ujinga, aiseeh ! hivi kaendeleaje huko mbele ?
 
Hivi majuzi kulitokea maandamano ya wachimaji madini huko South Afrika kinyume cha amri ya Polisi na ikatokea watu zaidi ya 34 waliuawa. Serikali ya South Afrika wakiongozwa na polisi walifungua mashtaka kuwaadhibu viongozi wa maandamano hayo kama wao ndio walosababisha vifo vile. Dunia nzima ililaani kitendo hicho, balozi na hata marekani waliishutumu serikali ya South Afrika kuendelea kiutumia sheria ya Apartheid, kiasi kwamba iliwabidi ku withdraw mastaka hayo.

Mh. Tendwa inabidi ajifunze kuongozi badala ya kutumiwa kama kibaraka hasa pale mwandishi wa habari anapouawa pasipo huruma hata baada ya watu wote kusambaa. Ushahidi upo na unaonyesha wazi waliobakia pale walikuwa waandishi wa habari ambao walikuwa kazini wakiifanya kazi yao. Mauaji yamefanyika baada ya watu kusambaa..
Uzalendo sii sheria ya kutawala bali ni imani ya kuipenda nchi yako na watu wake..
 
Tambwe Hiza is a dead brain, to discuss what comes from his mouth ia a wastage of our valuable time. Tambwe, no one is here to swallow your stupidity. We need police, police in its real sence not a group of thugs.

Mkuu... Don't even bite your lips... Tambwe mwenyewe haamini hip waraka
Ccm is out of touch
 
NA RICHARD TAMBWE HIZZA

WIKI hii waandishi wa habari kutoka katika vyombo mbalimbali nchini waliandamana kulaani kuuawa kwa mwandishi wa habari wa Kituo cha Chanel 10 huko Iringa, kifo cha mwandishi huyu kwa bahati mbaya na kwa mara nyingine tena kimewagawa wananchi katika makundi yanayotofautiana kifikra kuhusu chanzo na hatimaye kufariki kwake.

Wapo wanaoona na kuamini polisi wametumia nguvu kubwa katika kukabiliana na tatizo lililokuwepo, wapo wanaoamini kwamba jeshi la polisi lilikuwa linatimiza wajibu wake na madhara haya makubwa yaliyotokea yanatokana na CHADEMA kuendeleza ghasia katika nchi na kujaribu kuifanya isitawalike kama walivyoahidi baada ya kushindwa vibaya katika uchaguzi mkuu uliopita (walishinda viti 23 kati ya majimbo 239).

Hata hivyo, kabla ya kuingia katika tafakuri pana zaidi zinazotokana na msiba huu sina budi kutoa pole kwa familia ya Mwangosi, waandishi waliokuwa karibu naye katika kufanikisha majukumu yake ya uandishi wa habari, Kituo cha Channel 10 na Watanzania wote kwa ujumla, kwa kuondokewa na mwananchi mwenzetu katika mazingira ambayo wote hatukuyategemea.

Tumeshuhudia wakati taifa likiwa katika simanzi nzito kutokana na msiba huu, wapo wenzetu walioamua kuutumia kama turufu ya kuleta chuki baina ya jeshi la polisi na waandishi na zaidi umma wa Watanzania ambao usalama wao na mali zao unategemea sana uwepo wa jeshi hilo. Kuna mambo mengi ambayo nimekuwa najiuliza na ningependa Watanzania wote tujiulize, hivi ghasia zilizosababisha msiba huu zilisababishwa na nini/nani?

Je kulikuwa na ulazima kwa CHADEMA kukaidi amri ya polisi ya kusubiri sensa ipite? Je, ukaidi wa CHADEMA siyo chanzo cha maafa yaliyotokea na yanayotokea mara kwa mara nchini? Je, ingekuwa sawa kwa jeshi la polisi kuwaachia CHADEMA kufanya shughuli ambayo walikwisha wazuia wasiifanye? Je, polisi ingewaachia kufanya jambo ambalo walikwishawazuia wangekuwa wanatimiza sheria na wajibu wao? Na je, uhalali wa uwepo wa jeshi hilo ungeendelea kuwepo?

Wananchi wote tunapaswa kuheshimu sheria na polisi wana jukumu la kutulazimisha kufuata sheria tunapozikiuka vikiwemo vyama vya siasa, najua sheria ya vyama vya siasa inavipa fursa vyama kufanya maandamano na mikutano baada ya kutoa taarifa polisi, lakini sheria hiyo hiyo inasema vitafanya hivyo endapo tu kama havitapata amri pingamizi kutoka polisi (sheria ya vyama vya siasa 1992 kifungu cha 11).

Tujiulize kulikuwa na ulazima gani kwa CHADEMA ambao mwaka mzima wamekuwa wakiruhusiwa kufanya mikutano na maandamano kulazimisha kufanya mkutano uliosababisha kifo baada ya kupata amri pingamizi? Kama waliona polisi hawakuwafanyia haki je ilikuwa vyema kuandaa mapambano dhidi ya polisi? Jje walichukua hatua yoyote ya kisheria dhidi ya polisi au hawana imani na vyombo vya kisheria kama ambavyo Tundu Lissu anavyoziponda mahakama zetu bila kuheshimu kwamba zilimpa ushindi yeye binafsi katika kesi yake ya uchaguzi aliyofunguliwa na mgombea wa CCM, na zile zilizokipa ushindi chama chake zilizowavua ubunge wana CCM huko Sumbawanga na Igunga.

Naamini ili jeshi la polisi liweze kuendelea kulinda amani ndani ya nchi ni lazima tuliamini na lazima tujue kwamba lipo, likizuia jambo kwa mujibu wa sheria wote tuheshimu vinginevyo litakuwa halina sababu ya kuwepo. Si mara moja au mbili mamlaka za umma na vyombo vya sheria viliamua mambo muhimu katika maendeleo ya taifa, lakini yalipata upinzani hadi pale polisi ilipotumia nguvu kuhakikisha sheria inafuatwa na utekelezaji wake unatimia.

Je, kumfukuza waziri katika hafla ya kulaani mauaji na kumkaribisha mwana-CHADEMA Dk. Lweitama kuhutubia na kuilaani serikali ni sawa? Je, ni sawa kulilaumu jeshi zima la polisi kwa tatizo lililojitokeza sehemu moja ya nchi tena katika kutimiza wajibu wao? Kitendo cha kutowalaani walioanzisha uvunjaji wa sheria uliosababisha ndugu yetu Mwangosi kupoteza maisha katika umri mdogo kinaashiria nini kutoka katika taasisi zetu za habari?

Hapa ndiyo maswali mengine yasiyo na majibu yanapoanza, kwa nini tamko lililotolewa na CHADEMA na lile la wanahabari yanashabihiana. Kwa nini wanahabari hawakuilaumu CHADEMA hata mara moja kwa kutokutii sheria na kuanzisha ghasia zilizosababisha maafa ya ndugu yetu. Nadhani tunahitaji tafakuri pana zaidi. Je wametumwa? Wana hasira? au nao wameanza kushirikishwa katika ajenda za siri dhidi ya serikali na vyombo vyake?

Wote tumesikitishwa na msiba huu sidhani kama ni vyema kuendelea kushambulia jeshi la polisi bali kuangalia nani ameanzisha sokomoko ili awajibishwe kisheria, kama ikibainika aliyeua ni raia wa kawaida sheria ichukue mkondo wake, pia ikibainika muuaji ni askari akiwa katika kutimiza majukumu yake ni vyema taratibu za kijeshi na mahakama zitumike badala ya kuendeleza chuki zisizo na msingi.

Tusijisahau wote tunawahitaji polisi kama ambavyo tulikuwa tunamhitaji ndugu yetu Mwangosi nikiwemo mimi niliyeshirikiana naye katika shughuli mbalimbali. Tusiwe na hasira maana wahenga walisema hasira hasara. Tutafute suluhisho la yanayotokea yasijirudie.

Hiza lini ukawa na akili timamu. ww unaona CDM ndo walikaidi amri halali ya police lkn CCM kule bububu hawakikaidi amri halali? Acha ujinga.
 
Kosa la kuandamana au kufanya mkusanyiko bila kibali cha polisi ni faini ya sh 50000 au kifungo cha miezi mitatu jela au vyote kwa pamoja...Sasa Tambwe anieleze wapi sheria inasema kuwa adhabu yake ni kifo achilia mbali kumuua mwandishi wa habari aliyekuwa kazini...naomba majibu
 
Back
Top Bottom