Mjukuu wa kigogo
JF-Expert Member
- Sep 19, 2023
- 200
- 431
Waraka kwa DED wa Halmashauri ya Mji wa Bunda, Emmanuel Mkongo
Heshima yako mkuu!
Nitajitahidi kuandika andiko fupi sana!Nakumbuka kwenye vikao vyako vingi huwa unawaencorage sana wana Bunda kupambana zaidi badala ya kukata tamaa! Awali hawakuweza kukuelewa ila Kwa sasa wamekuelewa vizuri kiongozi.
Mwaka juzi kwenye semina mojawapo ya walimu ulitoa ahadi ukasema umetokea Wilaya ya Arumeru,mahali ambapo kuna shule ya maarufu ya Kisimiri inayoongoza katika mitihani ya kidato cha sita.
Nakumbuka ulisema furaha Yako ni kuona Halmashauri ya Bunda pia inatoa shule Bora.Wengi walijua ni porojo ila kumbe kiongozi ulimaanisha. Majuzi shule ya Bunda High school imeingia katika kundi la shule 10 Bora kitaifa! Haikuwahi kabisa kutarajiwa Halmashauri ya Bunda kutoa shule itakayoingia katika 10 Bora kitaifa.Hongera mkuu kwa hili.
Pia pongezi zaidi kwa ujenzi wa haraka zaidi Kwa shule mpya ya Sekondari inakayojengwa katika kata ya Bunda. Lakini pia miaka ya nyuma wilaya yetu ilikejeliwa Sana Kwa kupata hati chafu kwenye suala zima la matumizi ya pesa. Kila CAG alipokuwa akitoa taarifa zake Bungeni ilikuwa nadra kulikosa jina la Bunda.
Kwa sasa hali ni tofauti,umefanikiwa zaidi kwenye matumizi (expenditures) ya mapato ndani ya halmashauri,uwazi (transparency)ni mkubwa pamoja na uwajibikaji (accountability)
Kuhusu suala la elimu katika halmashauri,imekuwa ni bahati nzuri sana unafanya kazi na maafisa elimu mahiri sana upande wa msingi na Sekondari ndio maana kumekuwepo na ongezeko zaidi la ufaulu katika shule ndani ya halmashauri.
Afisa elimu Sekondari ndani ya hamashauri ya mji hatujui kama tunaweza kuwa nae kwa siku nyingi maana Kwa namna anavyojituma,anavyotumia busara na alivyotengeneza mazingira rafiki Kwa walimu ambaye nae haitashangaza kuhamishwa na kupelekwa wizarani au kupandishwa cheo zaidi!
Bahati mbaya zaidi nafasi ya u-DED siyo ya kisiasa ni ya kiutendaji zaidi ndio maana wengi huwa hawaoni mazuri mnayoyafanya zaidi ya kusubiri mtajwe kwenye mabaya kupitia vyombo vya habari, ila kwa wafuatiliaji wa mambo huwa tunapenda kukosoa au kusifia ili mtu ajifunze hapo hapo!
Kwangu Mimi you are the best DED,Kisha namba pili naitupa Kwa Janeth Muyanja katika historia ya Bunda!
🙏 All the best, chalii ya Chugga!
NB: Maendeleo ya ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari kata ya Bunda unavyoendeleakwa Kasi.