Wapinzani wafanye nini ili kuing'oa CCM?

Mara nyingi tunahitaji nahodha (dereva) makini na utingo wanaomsaidia vizuri ili kufika salama.
Kwa nini tuishi kwenye siasa kwa kutegemea kudra za Mwenyezi Mungu? Fikiria kama leo katiba ya Marekani ndiyo ingekuwa kama hii ya kwetu kingetokea nini kwenye taifa hilo kubwa na lenye kumiliki silaha za nyukilia kwa aina ya matendo ya Trump?
 
Ningekuwa kiongozi wa upinzani (if wishes were horses.......) ningeweka mkazo na juhudi kubwa sana katika kuongeza wabunge na madiwani kwanza kuliko kupoteza hela kwenye kugombea urais.
Mwalimu alishatoa wazo kama hilo Mwaka 1995 na likatekelezwa. Kwa miaka kumi CHADEMA haikusimamisha mgombea Urais mpaka ilipofika mwaka 2005.

Kimkakati kwa siasa za Tanzania kusimamisha wagombea Udiwani na Ubunge bila ya kuweka mgombea Urais chama kinaonekana hakina mwelekeo na hakitaaminiwa na wapiga kura!

Mgombea Urais husaidia chama kujenga hamasa nchi nzima!!
 
Kwa nini tuishi kwenye siasa kwa kutegemea kudra za Mwenyezi Mungu? Fikiria kama leo katiba ya Marekani ndiyo ingekuwa kama hii ya kwetu kingetokea nini kwenye taifa hilo kubwa na lenye kumiliki silaha za nyukilia kwa aina ya matendo ya Trump?
Mkuu sidhani ni vizuri kuichukulia Marekani kama mfano wa kuigwa. Marekani kwa sasa hawana DEMOCRACY bali wana PLUTOCRACY.

Serikali ya Marekani inachofanya ni tofauti na wanachokitaka wananchi wao. Serikali inatekeleza matakwa ya vikundi vichache vilivyowanunua hawa maseneta na makongresman, na hata Rais (pengine Trump ni tofauti kidogo, lakini sio kwenye foreign policy).

Hivi vikundi vyenye nguvu Marekani wala havina mizizi yao nchini humo.

Amini usiamini, TZ is more democratic than USA.
 
Mwalimu alishatoa wazo kama hilo Mwaka 1995 na likatekelezwa. Kwa miaka kumi CHADEMA haikusimamisha mgombea Urais mpaka ilipofika mwaka 2005.

Kimkakati kwa siasa za Tanzania kusimamisha wagombea Udiwani na Ubunge bila ya kuweka mgombea Urais chama kinaonekana hakina mwelekeo na hakitaaminiwa na wapiga kura!

Mgombea Urais husaidia chama kujenga hamasa nchi nzima!!
Good luck.
 
Imezuka hoja hapa JF kwamba CCM kuendelea kwake kuwa madarakani ni kwa sababu Tanzania tuna vyama vya upinzani dhaifu. inawezekana hoja hiyo ina ukweli fulani ndani yake lakini lazima wanaouona upinzani ni dhaifu watoe maoni yao ni nini kifanyike ili CCM ing'oke madarakani Tanzania ikibaki salama.

Wengine hatuuoni uimara wa CCM bali tunaona mabavu ya CCM kutumia dola dhidi ya vyama vingine vya siasa. Leo hoja kubwa kwamba upinzani ni dhaifu ni madai kwamba wameiacha hoja "yao" ya ufisadi.

Lakini ni kweli kuwa Upinzani wameacha hoja yao ya kupiga vita ufisadi? Hivi kuna tofauti gani ya hatua zilizochukuliwa dhidi ya Lugumi kama ilivyokuwa kwa EPA ama Tegeta Escrow? Wakati ajenda ya wapinzani ilipokuwa kupiga vita ufisadi, CCM walifanya nini tofauti na sasa?

Lowassa aliitwa fisadi Pale Mwembe Yanga kwa kuvunja mkataba kati ya City waters na Dawasa, leo wapinzani wakizungumizia kuhusu Bombadier, ujenzi wa uwanja wa ndege Chato, matumizi nje ya bajeti,kukopa fedha kinyemela inaonekana hawazungumzii ufisadi, ni kwa nini?
Nadhani Hapa siyo Mahali pake (Huwezi kuweka hadharani mbinu za kumpiga Adui au mpinzani wako) There many ways to kill a Rat
 
Vyama Vyote Vya Upinzani Tz Viungane Viform Jeshi Kama Umkhonto We sizwe La ANC au RWANDAN PATRIOTIC FRONT-RPF viwachape CCm Kijeshi Ndio Njia Pekee Iliyobakia La Sivyo Kwa Sanduku La Kura CCM kutoka Ni Ndoto
 
Ni vema upinzani wakafahamu kuwa mbio za kuishika dola ni mbio za masafa marefu (Marathon) na sio za mita 400 (Sprinting).

Pace yourselves guys. Rome was not built in a day.
 
Watanzania bado hawajataka kuwapa wapinzani nchi
Kwa sababu gani unatoa hoja yako hii?

Kifyatu si kwamba hoja yako haina mantiki, hapana. Ila mimi kutokana na uzowefu wangu wa zaidi ya miaka 29 kwenye siasa, kule "field" propaganda zinazotumiwa na CCM huwa kali sana na kwenye zama hizi za utandawazi basi ndiyo inakuwa shida kabisa!

Hapa Iringa kuna uchaguzi kwenye kata ya Kitwilu. CCM wanazunguka hapa mjini na kuwaambia wapiga kura wa kata hiyo wamchague mgombea wao (Aliyekuwa diwani kupitia CHADEMA kabla ya kujiunga CCM) kuwa wakimchagua atakuwa anawasiliana moja kwa moja na Rais Magufuli.

Sasa ndiyo mnaingia kwenye uchaguzi bila ya kuwa na mgombea Urais ndiyo inakuwa balaa. Ila ukisema mfumo wa kumpata mgombea urais ndani ya CHADEMA unatakiwa ubadilishwe, hilo nalikubali kwa asilimia mia moja (100%)
 
Vyama pinzania ni wewe na mimi na sio vinginevyo!!!! Tujiulize sasa tumekosea wapi?? Wananchi kujitambua ndiyo solution ya kulitoa joka CCM!!!
 
Kwa sababu gani unatoa hoja yako hii?

Kifyatu si kwamba hoja yako haina mantiki, hapana. Ila mimi kutokana na uzowefu wangu wa zaidi ya miaka 29 kwenye siasa, kule "field" propaganda zinazotumiwa na CCM huwa kali sana na kwenye zama hizi za utandawazi basi ndiyo inakuwa shida sana!

Hapa Iringa kuna uchaguzi kuna uchaguzi kwenye kata ya Kitwilu. CCM wanazunguka hapa mjini na kuwaambia wapiga kura wa kata hiyo wamchague mgombea wao (Aliyekuwa diwani kupitia CHADEMA kabla ya kujiunga CCM) kwa kuwa wakimchagua atakuwa anawasiliana moja kwa moja na Rais Magufuli.

Sasa ndiyo mnaingia kwenye uchaguzi bila ya kuwa na mgombea Urais ndiyo inakuwa balaa. Ila ukisema mfumo wa kumpata mgombea urais ndani ya CHADEMA unatakiwa ubadilishwe, hilo nalikubali kwa asilimia mia moja (100%)
Nina sababu mbili:
1.Vyama vya upinzani Tanzania,sio la mapambano ya kifikra au itikadi.Viliorodheshwa tu kama vyama vya hiari.Ndio maana mpaka leo wananchi walio wengi hawajui hasa hivi vyama vinasimamia nini hasa.
2.Utaona ktk uchaguzi wa 2015 baada ya ujio wa Magufuli,watu wengi walisema Magufuli ndiye aina ya Rais wanae mtaka.Hata baada ya uchaguzi baadhi ya wapinzani walikiri kuwa Magufuli anatekeleza mambo ambayo wao wapinzani walikuwa wanayasimamia.
Kwahiyo utaona kuwa sio kwamba wananchi hawaitaki CCM,bali kuna mambo machache yakirekebishwa,then hawana tatizo.
 
Imezuka hoja hapa JF kwamba CCM kuendelea kwake kuwa madarakani ni kwa sababu Tanzania tuna vyama vya upinzani dhaifu. inawezekana hoja hiyo ina ukweli fulani ndani yake lakini lazima wanaouona upinzani ni dhaifu watoe maoni yao ni nini kifanyike ili CCM ing'oke madarakani Tanzania ikibaki salama.

Wengine hatuuoni uimara wa CCM bali tunaona mabavu ya CCM kutumia dola dhidi ya vyama vingine vya siasa. Leo hoja kubwa kwamba upinzani ni dhaifu ni madai kwamba wameiacha hoja "yao" ya ufisadi.

Lakini ni kweli kuwa Upinzani wameacha hoja yao ya kupiga vita ufisadi? Hivi kuna tofauti gani ya hatua zilizochukuliwa dhidi ya Lugumi kama ilivyokuwa kwa EPA ama Tegeta Escrow? Wakati ajenda ya wapinzani ilipokuwa kupiga vita ufisadi, CCM walifanya nini tofauti na sasa?

Lowassa aliitwa fisadi Pale Mwembe Yanga kwa kuvunja mkataba kati ya City waters na Dawasa, leo wapinzani wakizungumizia kuhusu Bombadier, ujenzi wa uwanja wa ndege Chato, matumizi nje ya bajeti,kukopa fedha kinyemela inaonekana hawazungumzii ufisadi, ni kwa nini?
Nani alimuita Lowassa fisadi?
 
Imezuka hoja hapa JF kwamba CCM kuendelea kwake kuwa madarakani ni kwa sababu Tanzania tuna vyama vya upinzani dhaifu. inawezekana hoja hiyo ina ukweli fulani ndani yake lakini lazima wanaouona upinzani ni dhaifu watoe maoni yao ni nini kifanyike ili CCM ing'oke madarakani Tanzania ikibaki salama.

Wengine hatuuoni uimara wa CCM bali tunaona mabavu ya CCM kutumia dola dhidi ya vyama vingine vya siasa. Leo hoja kubwa kwamba upinzani ni dhaifu ni madai kwamba wameiacha hoja "yao" ya ufisadi.

Lakini ni kweli kuwa Upinzani wameacha hoja yao ya kupiga vita ufisadi? Hivi kuna tofauti gani ya hatua zilizochukuliwa dhidi ya Lugumi kama ilivyokuwa kwa EPA ama Tegeta Escrow? Wakati ajenda ya wapinzani ilipokuwa kupiga vita ufisadi, CCM walifanya nini tofauti na sasa?

Lowassa aliitwa fisadi Pale Mwembe Yanga kwa kuvunja mkataba kati ya City waters na Dawasa, leo wapinzani wakizungumizia kuhusu Bombadier, ujenzi wa uwanja wa ndege Chato, matumizi nje ya bajeti,kukopa fedha kinyemela inaonekana hawazungumzii ufisadi, ni kwa nini?
CCM inang'olewa na wanaccm wenyewe wakiamua kuuasi mfumo wao.Hao wapinzani ni kama wameshindwa kwa miongo mitatu na wananchi hawana imani na upinzani
 
Watanzania kwa ujumla wanahitaji maendeleo basi, hawajali yanaletwa na CDM,CCM,CUF etc, hii kukaa mnahubiri u Chadema na U CCM ndo unaowarudisha nyuma, kama Chadema itaendelea kuongelea udikteta na kukosoa hotuba za Raisi, wasahau kuongoza nchi hii labda 2080 kizazi kijacho, sio hiki cha kubadili gia angani. Halafu muache kukaribisha mafisadi mliotuaminisha mna ushahidi na ufisadi wao na kuwapa sifa na vyeo. Dhambi ya kumuweka Lowassa mgombea 2015 itawatafuna miaka 40 ijayo.
Ulikuwa wapi mzee baba? Uchangiaji wa aina yako mimi ndiyo ninaoutaka, "komenti" fupi, lakini imebeba uhalisia wa siasa na jamii yetu hapa Tz kwa sasa.
Wengi hatuna vyama, lakini tunaunga mkono utawala, iwapo unaonesha mabadiliko.
Hili la kuabudu vyama vya siasa hata kama vinatenda hovyo ni upofu unaisababishwa na ghadhabu iliyotokana na kunyang'anywa tonge midomoni mwa watu na ukabila.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom