Wapinzani wafanye nini ili kuing'oa CCM?

Hoja za kichovu hizi! Eti watanzania kwa ujumla wanahitaji maendeleo, basi! Hizi ndizo blah blah mlizolishwa na Sizonje za kutaka kupumbaza wajinga. Kuna uhusiano mkubwa wa maendeleo ya nchi na sera za chama kinachoongoza nchi kwa wakati husika. Ni mtu mjinga pekee atakayeendelea kung'ang'ana na Lowasa kwa hoja ya ufisadi ilihali mambo yote yaliishawekwa wazi kwamba hiyo ilikuwa ni vita ya madaraka ndani ya CCM. Kwanini usijiulize swali dogo tu. Hivi Lowasa ana kinga gani kiasi kwamba kama alihusika na huo ufisadi asifikishwe kortni tangu mwaka 2008? Tena kwa siasa hizi za chuki, leo Lowasa angekuwa uraiani? Na kama hoja ni ufisadi, hawa akina Chenge, Ngeleja, Karamagi; na the like ambao wamejazana CCM mnawazungumziaje? Hakuna mtu mwenye mawaa atakayeondoka CCM kwenda upinzani, hifadhi ya mafisadi iko CCM, kama una akili lakini!
USHAIDI WA UFISADI WA LOWASA ANAO MNYIKA AU NA YEYE ALITUDANGANYA ?
 
Bila CHADEMA kumfukuza Lowassa na Sumaye na kisha kumuomba Msamaha Dr. Slaa Ikulu wataiona kwenye TV tuu.
 
Imezuka hoja hapa JF kwamba CCM kuendelea kwake kuwa madarakani ni kwa sababu Tanzania tuna vyama vya upinzani dhaifu. inawezekana hoja hiyo ina ukweli fulani ndani yake lakini lazima wanaouona upinzani ni dhaifu watoe maoni yao ni nini kifanyike ili CCM ing'oke madarakani Tanzania ikibaki salama.

Wengine hatuuoni uimara wa CCM bali tunaona mabavu ya CCM kutumia dola dhidi ya vyama vingine vya siasa. Leo hoja kubwa kwamba upinzani ni dhaifu ni madai kwamba wameiacha hoja "yao" ya ufisadi.

Lakini ni kweli kuwa Upinzani wameacha hoja yao ya kupiga vita ufisadi? Hivi kuna tofauti gani ya hatua zilizochukuliwa dhidi ya Lugumi kama ilivyokuwa kwa EPA ama Tegeta Escrow? Wakati ajenda ya wapinzani ilipokuwa kupiga vita ufisadi, CCM walifanya nini tofauti na sasa?

Lowassa aliitwa fisadi Pale Mwembe Yanga kwa kuvunja mkataba kati ya City waters na Dawasa, leo wapinzani wakizungumizia kuhusu Bombadier, ujenzi wa uwanja wa ndege Chato, matumizi nje ya bajeti,kukopa fedha kinyemela inaonekana hawazungumzii ufisadi, ni kwa nini?

Hii ni one of your best thread mkuu!!

Cha kwanza kabisa ni kuacha mapambano yotr wanayofanya na kuelekeza vita yote kwenye TUME HURU YA UCHAGUZI...waandamane, waweke mikutano.....kila wanachofanya kiwe muundo na uhuru wa tume ya uchaguzi
Hili ni la msingi na nashangaa kwa nn wanashiriki chaguzi wakati wanajua tume sio huru katu

La pili ni kuwa na sera au maoni au njia mbadala, badala ya kuwa wakosoaji ni kuweka alternative, watu wanavutika na kuishi kwa kujua kuna chama mbadala na sio wakosoaji, kwa mfano magufuli kanunua bombardier kwa zile hela, badala ya kulaumu na wao wanatakiwa kununua bombardier na waeleze chanzo

Tatu ni kuwa na dira ya kushuka ngazi za chini na kutengeneza viongozi kuanzia watot..
ccm did this kupitia chipukizi, hawa watoto au young leaders wanakuwa nje ya mfumo wa shule wanakuwa kama skauti, au waislam na visomo/madrasa n.k hii ni function ya kufundisha historia ya nchi, uzalendo, uongozi majukumu ya vijana na, kuwa ba debate clubs ..KAMWE sio kufundisha kukosoa!!


la kwanza ndio key, so unaposikia mtu anasema 2020 cdm itaingia ikulu, unaanza kucheka na kuidharau hii akili

ukiingia deep down, haiingii akilini kuwa lowassa alijua ataingia ikulu kwa tumr ile...ALIJUA HAWEZI, sasa kwa nini alidanganya na kuwapa watu false hope, muda utatueleza....hakutumwa na ccm? investigation continues.....
 
wapinzani hawawezi kuongoza taifa hili hata nyerere aliwahi kusema mkiwapa nchi wapinzani dunia itawacheka, upinzani wa tanzania ni upinzani hewa hawana viongozi wanasubilia wanaofukuzwa kutoka chama tawala kwa kashifa mbalimbali ndoo wanawasimamisha kugombea ngazi mbalimbali jambo ambalo kwacwatu waelewa hawawezi kuwapa nchi na hakuna wakuwachagua zaidi ya washrika wao ambao wamezoea kuiba, ni ndoto ya mchana wapinzani kushika nchi
 
Waberoya nashukuru kwa kutoa ushauri mzuri sana. Badala ya kurusha vijembe ni kheri kutoa mawazo hata kama tutatofautiana na mawazo hayo.

Nianze na la Lowassa. Mimi kwa mtazamo wangu kila siku ni kwamba Lowassa si tatizo bali tatizo ni CHADEMA. Kuna hoja aliitoa Dr. Slaa kwamba kabla ya kujiunga na CHADEMA ni lazima kwanza Lowassa atangaze hadharani kwamba yeye si mhusika na kashifa ya Richmond. CHADEMA wakapuuzia.

Haiwezekani mtu ambaye kila siku mlikuwa mnamwita majina mabaya ya kila aina ghafla tu bila ya maelezo mnapokea na kumfanya mgombea wenu bila hata ya kutoa maelezo ni nini kimewafanya kubadilika kwa kiasi hicho.

Ndiyo maana "marafiki" wa Dr. Slaa kina Mzee Mwanakijiji na idawa wanawananga kila siku CHADEMA kwa upuuzi huo walioufanya. Hawajajibu hoja kama walipokuwa wanasema wana "ushahidi" walikuwa wanamaanisha nini ama walikuwa wanatumia uongo kujipatia ufuasi tu?

Leo mtu anajiuliza ni kwa nini Msigwa, Lema, Mnyika na hata Mbowe ambao walikuwa wanawaaminisha watanzania kuwa Lowassa ni mtu "Mbaya sana", wanatakaje watanzania wamchague mtu mbaya kuwa Rais wao?

Sasa mimi nitakuwa mtu wa mwisho kuamini kwamba Lowassa alihusika na ufisadi wowote ule kwenye Richmond, lakini itakuwa ngumu sana kuwaamini viongozi wa CHADEMA wanaposema kwamba Lowassa anafaa kuwa Rais. Viongozi wa CHADEMA hawana nguvu ya kimaadili (Moral Authority) kumnadi Lowassa bila ya kwanza kuwaeleza watanzania ni kwa nini walikuwa wanamsema ni mtu mbaya kiasi kile?

Kuhusu Sera na ujenzi wa chama nadhani kuna matatizo mawili makubwa. Kwanza ni wana CHADEMA kutaka kumlinganisha Vincent Mashinji na Slaa. Mungu kampa kila mtu kipawa chake kwa ivo haiwezekani tukafanana. Mashinji anapata wakati mgumu sana kuiunganisha hii CHADEMA "mpya".

Jambo la pili ni CHADEMA kushughulika na Lowassa wakiwa wamemakinika. Lowassa alijitengeneza kama taasisi na alipokwenda CHADEMA alikwenda kama taasisi. CHADEMA wanatakiwa kumlazimisha Lowassa asiwe taasisi ndani ya taasisi.

Kuingia kwa Lowassa kulileta taharuki na fadhaa kwa baadhi watendaji ndani ya CHADEMA ambao walikuwa wanaamini waliipigania chama kwa muda mrefu wakati huo Lowassa "anakula raha" CCM. Kuna watu CHADEMA wamepotezwa kabisa kwa ujio wa Lowassa.

Jambo moja la kufurahisha ni kwamba hata CCM wanaposema vyama vya upinzani humaanisha CHADEMA. je CHADEMA wenyewe wanaijua na kuikuza thamani yao?
 
Imezuka hoja hapa JF kwamba CCM kuendelea kwake kuwa madarakani ni kwa sababu Tanzania tuna vyama vya upinzani dhaifu. inawezekana hoja hiyo ina ukweli fulani ndani yake lakini lazima wanaouona upinzani ni dhaifu watoe maoni yao ni nini kifanyike ili CCM ing'oke madarakani Tanzania ikibaki salama.

Wengine hatuuoni uimara wa CCM bali tunaona mabavu ya CCM kutumia dola dhidi ya vyama vingine vya siasa. Leo hoja kubwa kwamba upinzani ni dhaifu ni madai kwamba wameiacha hoja "yao" ya ufisadi.

Lakini ni kweli kuwa Upinzani wameacha hoja yao ya kupiga vita ufisadi? Hivi kuna tofauti gani ya hatua zilizochukuliwa dhidi ya Lugumi kama ilivyokuwa kwa EPA ama Tegeta Escrow? Wakati ajenda ya wapinzani ilipokuwa kupiga vita ufisadi, CCM walifanya nini tofauti na sasa?

Lowassa aliitwa fisadi Pale Mwembe Yanga kwa kuvunja mkataba kati ya City waters na Dawasa, leo wapinzani wakizungumizia kuhusu Bombadier, ujenzi wa uwanja wa ndege Chato, matumizi nje ya bajeti,kukopa fedha kinyemela inaonekana hawazungumzii ufisadi, ni kwa nini?
Mwambieni aruhusu mikutano ya kisiasa kama katiba na sheria inavyosema gogoro nn
 
Waberoya nashukuru kwa kutoa ushauri mzuri sana. Badala ya kurusha vijembe ni kheri kutoa mawazo hata kama tutatofautiana na mawazo hayo.

Nianze na la Lowassa. Mimi kwa mtazamo wangu kila siku ni kwamba Lowassa si tatizo bali tatizo ni CHADEMA. Kuna hoja aliitoa Dr. Slaa kwamba kabla ya kujiunga na CHADEMA ni lazima kwanza Lowassa atangaze hadharani kwamba yeye si mhusika na kashifa ya Richmond. CHADEMA wakapuuzia.

Haiwezekani mtu ambaye kila siku mlikuwa mnamwita majina mabaya ya kila aina ghafla tu bila ya maelezo mnapokea na kumfanya mgombea wenu bila hata ya kutoa maelezo ni nini kimewafanya kubadilika kwa kiasi hicho.

Ndiyo maana "marafiki" wa Dr. Slaa kina Mzee Mwanakijiji na idawa wanawananga kila siku CHADEMA kwa upuuzi huo walioufanya. Hawajajibu hoja kama walipokuwa wanasema wana "ushahidi" walikuwa wanamaanisha nini ama walikuwa wanatumia uongo kujipatia ufuasi tu?

Leo mtu anajiuliza ni kwa nini Msigwa, Lema, Mnyika na hata Mbowe ambao walikuwa wanawaaminisha watanzania kuwa Lowassa ni mtu "Mbaya sana", wanatakaje watanzania wamchague mtu mbaya kuwa Rais wao?

Sasa mimi nitakuwa mtu wa mwisho kuamini kwamba Lowassa alihusika na ufisadi wowote ule kwenye Richmond, lakini itakuwa ngumu sana kuwaamini viongozi wa CHADEMA wanaposema kwamba Lowassa anafaa kuwa Rais. Viongozi wa CHADEMA hawana nguvu ya kimaadili (Moral Authority) kumnadi Lowassa bila ya kwanza kuwaeleza watanzania ni kwa nini walikuwa wanamsema ni mtu mbaya kiasi kile?

Kuhusu Sera na ujenzi wa chama nadhani kuna matatizo mawili makubwa. Kwanza ni wana CHADEMA kutaka kumlinganisha Vincent Mashinji na Slaa. Mungu kampa kila mtu kipawa chake kwa ivo haiwezekani tukafanana. Mashinji anapata wakati mgumu sana kuiunganisha hii CHADEMA "mpya".

Jambo la pili ni CHADEMA kushughulika na Lowassa wakiwa wamemakinika. Lowassa alijitengeneza kama taasisi na alipokwenda CHADEMA alikwenda kama taasisi. CHADEMA wanatakiwa kumlazimisha Lowassa asiwe taasisi ndani ya taasisi.

Kuingia kwa Lowassa kulileta taharuki na fadhaa kwa baadhi watendaji ndani ya CHADEMA ambao walikuwa wanaamini waliipigania chama kwa muda mrefu wakati huo Lowassa "anakula raha" CCM. Kuna watu CHADEMA wamepotezwa kabisa kwa ujio wa Lowassa.

Jambo moja la kufurahisha ni kwamba hata CCM wanaposema vyama vya upinzani humaanisha CHADEMA. je CHADEMA wenyewe wanaijua na kuikuza thamani yao?

uko sahihi sana tu

kuna mahali CDM ilikosea na mahali penyewe ni kutokupata muda wa kutafakari ushauri wa watu wengine, kuna barrier ambayo chadema imeweka ukianza kutoa tu ushauri...tayari unajulikana wewe wa kule au wa huku au msaliti...kuna watu wameumizwa sana kisaikolojia pale ambapo wenzao waliwaita wasaliti wakati walikuwa royal na wanaipenda cdm yao

moyo wa kusikilizana, kujadili na kuamua kwa pamoja uliishaondoka chadema
 
Mtazamo wako bado unatia ugumu kuona ni namna gani ya kuweza kuiondoa ccm.
nguvu ya upinzani ni ndogo sana/dhaifu kuweza kupambana na ccm.
Namna ambayo mnaweza kufanya ni kuunganisha nguvu yenu ndogo( japo hamkubali) mliyo nayo kwa sasa, pamoja na nguvu ya kundi kubwa la watu wasioegemea upande wowote kisiasa.
Na hawa mtawapata kwa kuja na mkakati kabambe wa sera na hoja madhubuti zenye kuweza kulishawishi kundi hili kuwaunga mkono.
Daftari la tume ya uchaguzi walijiandikisha watu zaidi ya 20mil, waliopiga kura ni kama 15 mil.
Watu yapata 6mil.(karibu sawa na idadi ya kura za lowasa) hawakupiga kura.
Inawezekana kundi hili halikupata ushawishi wa kutosha.
Kama mnataka kupambana na ccm, anzeni na hili kundi.
 
Katiba mpya na Tume huru ya uchaguzi ndiyo suluhisho la kudumu.
Pengine unachosema ni kweli mkuu.

Lakini hebu iangalie Kenya leo. Katiba yao mpya na tume yao huru ya uchaguzi vinawasaidia kuepuka migogoro?

Saa nyingine sio lazima tuwe na gari jipya ili tufike tuendako salama.

Mara nyingi tunahitaji nahodha (dereva) makini na utingo wanaomsaidia vizuri ili kufika salama.
 
Miaka ya nyuma wapinzani walipewa ushauri mzuri sana na kama wangeufuata sasa hivi wangekuwa wamebakisha hatua chache sana kuiondoa CCM kosa walilofanya ni kupuuzia huo ushauri wakiamini tayari wana uwezo wa kuiondoa CCM
 
Ningekuwa kiongozi wa upinzani (if wishes were horses.......) ningeweka mkazo na juhudi kubwa sana katika kuongeza wabunge na madiwani kwanza kuliko kupoteza hela kwenye kugombea urais.

Mimi leo hii nikisimama mbele ya wapinzani kuwapa ushauri wanaweza kunitupia mawe au mayai viza. Basi naepusha shari.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom