Tunutu kiwavi
JF-Expert Member
- Jul 2, 2016
- 528
- 215
USHAIDI WA UFISADI WA LOWASA ANAO MNYIKA AU NA YEYE ALITUDANGANYA ?Hoja za kichovu hizi! Eti watanzania kwa ujumla wanahitaji maendeleo, basi! Hizi ndizo blah blah mlizolishwa na Sizonje za kutaka kupumbaza wajinga. Kuna uhusiano mkubwa wa maendeleo ya nchi na sera za chama kinachoongoza nchi kwa wakati husika. Ni mtu mjinga pekee atakayeendelea kung'ang'ana na Lowasa kwa hoja ya ufisadi ilihali mambo yote yaliishawekwa wazi kwamba hiyo ilikuwa ni vita ya madaraka ndani ya CCM. Kwanini usijiulize swali dogo tu. Hivi Lowasa ana kinga gani kiasi kwamba kama alihusika na huo ufisadi asifikishwe kortni tangu mwaka 2008? Tena kwa siasa hizi za chuki, leo Lowasa angekuwa uraiani? Na kama hoja ni ufisadi, hawa akina Chenge, Ngeleja, Karamagi; na the like ambao wamejazana CCM mnawazungumziaje? Hakuna mtu mwenye mawaa atakayeondoka CCM kwenda upinzani, hifadhi ya mafisadi iko CCM, kama una akili lakini!