Wapi nitapata headphones zenye akili?

CORAL

JF-Expert Member
Joined
Jun 26, 2011
Posts
2,828
Reaction score
1,862
Kwa kweli nimechoshwa na hizi takataka za kichina. Yaani unanunua headphones unaenjoy kwa miezi 2 na zikijiitahidi miezi 4 basi. Ugonjwa ni uleule bila kujali brand name yaani spika moja inaacha kufanya kazi bila sababu na mchezo ndio umeisha hivyo! Ukienda,kila duka ni hizohizo na hapo naongelea zile za bei kubwa kidogo (zaidi ya 10,000). Sasa naweza kupata wapi headphones nzuri?
 


Unahitaji headphone 🎧 kubwa au earbuds au in ear.

Kama upo Arusha, Moshi au Dar nenda Nakumatt. Kwenye shelf za computer accessories kuna headphone mbali mbali, zikiwemo za'
Wireless na wired.

Promate
Intex
Acme
Cliptec
Tembo
Canyon
 
Kwa tanzania mara mia umtafute mtu alonunua simu mpya au kitu chenye earphone umpe hela ya maana akuachie.

Mfano htc one inakuja na earphone za beats zenye thamani around dola 60 hadi 100 (120,000-200,000)

Lumia highend zinakuja na monster earphone ambazo ni equivalent ya beats

Mi ninazo za nokia za zamani zina miaka kama 7 hivi bado zinadunda japo sizitumii sana
 

Nashindwa kuelewa wafanyabiashara wetu. Hizo high quality headphones hawawezi kutuletea tushindwe wenyewe? Biaahara za wogawoga na kuigana ndizo zinazituponza.
 
Lakin wakat mwingne na utunzaji wako pia.. Mtu unakuta akishamalza anaikunja kunja km kamba ya katani anaitia mfukoni, mara azilalie, cjui mtoto azichezee.. Fata ushaur wa wana ni mzuri, ila matunzo yawepo
 

Unaweza pia kuagiza mbele kama accessory ya hiyo simu, utapata.
 
Agiza brand zinazoenda Australia, ukitaka ni-inbox ila itabidi uvumilie. Unapata Dr Dree kwa $100-300 ni choice yako tu na specs zako
 
Mambo yote kuagiza tu, hapa Bongo tunaibiwa sana haswa kwenye hizi Malls ndio midosho imejaa.
 
Nashindwa kuelewa wafanyabiashara wetu. Hizo high quality headphones hawawezi kutuletea tushindwe wenyewe? Biaahara za wogawoga na kuigana ndizo zinazituponza.

Acha kulialia wewe, mtu analeta biashara anayoona ina wateja wengi, bongo wateja wengi ni kama nyie mnaotaka headphones za elfu20 kushuka chini, sasa hiyo ni headphone au takataka?! Ingia online chukua headphones za maana, laki3 inakuja mpaka mlangoni kwako!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…