Mswahili Old Acc
JF-Expert Member
- Sep 27, 2006
- 488
- 24
Mbona yupo! kawa kinyonga au unaweza kusema kabadilisha Kanzu ila sheikh ni yule yule.hivi sasa yupo humuoni?Zitto kama hata kama unashindwa kuingia humu and i can understand lakini tutumie hotuba yako na ya kiongozi wa upinzani ambayo soon utakapoweza.....kule kweny thread ya hotuba ya bajeti
Usitususe wenzio ....
Tanzanianjema
As i said earlier, political strategy......
Tanzanianjema
Tizama katiba ya Nigeria kifungu 419.angekuwa huko wangesema huyo Mama ni kutoka kabila la IGBO. ana balaa.Then deal na mwanakijiji na si mama wa zitto...
Au hata mimi...
Tanzanianjema
Siko hapa kutaka heshima wako. ungeanza kumdharau Zitto kwa ugoni kwanza, halafu uje kwangu.Nadhani wakati umefika nikudarau sasa...
all the best
Tanzanianjema
Nilikwambia uombe ruhusa toka kwa Zitto mwenyewe akikubali niweke wazi full family background.msije kulalamika kuwa ooh Mswahili thats too personal. sikatai mama Zitto kuwa anakuja Dar huenda anafaa baibui style ya Ninja nani atamjua? kama huamini subiri siku akifa huyu mama utaona watu watakao kuja kuzuia jeneza hapo ndipo utanikumbuka Mswahili. nikiwa hai nitakukumbusheni au nikitangulia mtanikumbuka siku hiyo.
BI SENTI 50.
Utakata niweke history ya mama zitto na vimwanga vyake? nasubiri jibu.
Swali la "kuiba mwanamke wa mwananchi" kweli halijaweza kuingia akilini mwangu kabisa kwa vile Mbunge Zitto na Mbunge Amina ni watu wa calibre moja. Wakati ni kweli kabisa kuwa Zitto Kulala na m ke wa mtu ni kinyume cha maadili kwake yeye mwenyewe na kwa mwanamke aliyehusika, lakini matumizi ya neno "kuiba" nadhani linamdhalilisha Mbunge Amina kama vile alilazimishwa au alichukuliwa bila yeye mwenyewe kujua.
Hamuwezi kukubali jibu lolote isipokuwa "ndiyo mimi na Amina tulikuwa na uhusiano wa kimapenzi na ulikuwa mzuri kweli". Akijibu hivyo haina maana itakuwa mwisho maswali yatakuja "kwanini uvunje ndoa ya watu, wewe kama kiongozi.. tukuamini vipi na wake zetu? vipi mabinti zetu na dada zetu, unawezaje kukaa Bungeni ilhali hivi na vile".
Kila mtu ana haki ya kuuliza lolote lile kwa mtu yeyote yule, lakini huwezi kumlazimisha mtu kujibu kama hataki. Haki ya uhuru wa kusema, inahusisha na uhuru wa kutotaka kusema! Ndio maana wenzetu wamarekani wanayo mabadiliko ya tano ya katiba!
Inapohusu mambo ya umma na yanayohusu maslahi ya TAifa kila kiongozi analazimika kutoa habari sahihi kwa wananchi. Hata hivyo hatuwezi kumlazimisha kiongozi kwa suala ambalo si la kisheria kutueleza habari za maisha yake binafsi? Hivi Malecela ana watoto wangapi? Je Kikwete amewahi kulala na wanawake wangapi? Mbona hatujawahi kumuona mke wa Lipumba? Vipi kuhusu Mrema na mke wake? Vipi kuhusu Freeman na mahusiano yake na kina dada? etc etc etc..
Kitila, kama Zitto atatokea na kusema madai na shutma dhidhi yake hazina ukweli, tumwombe aseme zaidi au tutaridhika na kauli yake? Kwanini tumlazimishe aseme sasa hivi wakati wetu sisi na kwa kalenda yetu sisi? Nakubaliana kabisa na suala zima kuzungumza mambo binafsi ya viongozi lakini lazima tuyaweke kwenye maudhui yake yanayostahili. Ni kweli kwa public figure maisha ya binafsi hakuna kabisa, na ninakubali kutokuulizia itaoenekana ni kutoa leseni. Hata hivyo tunapoulizia lazima tuwe tayari kupokea majibu!
Mnaosema double standard, you have no idea what your setting up! Kama tunakubali (na ninaamini ndiyo hoja yenu) kuwa masuala ya chumbani na malezi ya familia za viongozi yanaweza kuchambuliwa hadharani. Basi tufungue mjadala huo na tusiishie kwa Zitto na viongozi wa Chadema tu, au viongozi wengine wa upinzani. Tuwazungumze wote kwa uhuru na uwazi.
Ninachosema na ninapenda kueleweka ni kuwa kama Zitto alikuwa anatuhumiwa kujihusisha na biashara fulani haramu, hilo linazungumzika; kama anatuhumiwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mfanyakazi wake hilo linajadilika; kama Zitto angekuwa anatuhumiwa kuingiza jimbo lake kwenye mkataba wa ajabu ajabu hilo linazungumzika. Ni kutokana na mawazo hayo ndio maana tunauwezo na kila sababu ya kuhoji utendaji kazi wa viongozi wa serikali yetu, nia na matumizi yao.
Kuamua kutong'ang'ani kutaka kujua mambo ya undani ya chumbani ya mheshimiwa Zitto kwa vile tu yeye ni Mwakilishi wetu siyo unafiki! Sijawahi mahala popote kutaka kujua mambo ya chumbani ya Malecela, Kikwete, Kawawa, Lowassa, Nchimbi n.k SIyo kwa sababu hakuna madai dhidi yao au kwamba watu hawajui, ni kwa sababu tu kwamba jambo hilo linafungua sanduku ambalo hatuko tayari kulifungua. Mnapotetea kulazimisha Zitto awape undani wa kile "kilichotokea" hata kama keshakanusha hamtaki ukweli, bali mnataka ukweli kama ulivyoandikwa na nyinyi! Nilionya huko nyuma kuwa wanaotaka Zitto aseme hawawezi kuridhika hadi akiri kuwa na mahusiano ya kimapenzi na ni hicho ambayo baadhi ya ndugu zetu hapa wanataka. Chochote chini ya hapo, hakitakubalika.
Ninawaomba na tena nina wasihi kutoka ndani ya moyo wangu, msifungue sanduku hili la kujadili mambo ya chumbani ya viongozi au madhaifu ya kibinadamu ya viongozi wetu endapo mambo hayo hayahusiani moja kwa moja na nafasi zao, pesa za walipa kodi au maslahi yoyote yale ya kitaifa. Na msilazimishe kuwa kiongozi akienda msalani basi hilo ni jambo la kitaifa na mnataka details zake, kisa tu alionekana akienda msalani kwa jirani yake! Kipimo ambacho mnataka kukitumia kwa Zitto kikikubalika siyo kwamba kitaonesha umakini wa forum hii bali kutaishusha hadhi yake kuliko tunavyofikiria. Nawahakikishia kama mnafikiri mambo yanayojulikana ni ya Zitto peke yake fikirini tena. Wenye data za viongozi au wanaotaka kujua mambo ya viongozi siyo nyinyi peke yenu! Kuna watu wanajua viongozi wanaposafiri huja na kina nani, wanakaa wapi, na kina nani wanakutana nao. Tukikubali kuwa Zitto LAZIMA azungumze hapa (licha ya kuwa tayari amezungumza) na akiri (licha ya kuwa ameshakanusha) kuwa amefanya kitendo fulani (ambacho tayari amesema hakufanya) basi siyo kwamba tunataka kutenda haki bali kufurahisha tu udadisi wetu wa kibinadamu. Nawasihi tena, kama kweli ninyi mnaitetea forum hii, basi heshimuni mambo ya binafsi ya viongozi na hilo litumiwe kwa viongozi wote.
Hata hivyo endapo mambo yale ya binafsi yanahusiana na nafasi, vyeo, au yanaweza kuwa ni matendo ya kihalifu (criminal acts) basi hilo halina mjadala kwani hakuna mtu yeyote aliyejuu ya bodi au juu ya wanachama. Wote wako chini ya ukweli, ukweli mtupu, na si kingine bali ukweli.
Hata hivyo, sitarajii kuwa mtakubali ushauri huu kwani tayari mmeshanipa chama kuwa miye Chadema na ninamtetea Zitto. Na hii ni mara ya mwisho kuweka jambo hili sawa, mimi SIYO mwanachama wa CHADEMA ila ni mfuasi madhubuti wa mafundisho ya Mwalimu na mpenzi wa classical ideas za CCM. Kwa vile ninaandikia Tanzania Daima basi baadhi ya watu wamedhani mimi ni Chadema. Sasa hivi ninaandikia Kulikoni pia na sijui hilo linaendana na chama gani, na muda si mrefu (inshallah) nitaanza kuandikia magazeti ya serikali.
Mzee ES,
Hujaelewa tu? wakisema Lowassa anakamua Waziri Batilda ni masuala muhimu ya kitaifa kujadiliwa. Ikiwa anaekamua Zitto ( or any Chadema leader for that matter) hilo ni suala binafsi halina maslahi ya kitaifa...!! Thats Jamboforums!
Im equally ashamed here....