Wanawake, Wanawake, Wanawake! Nimewaita mara 3

Wanawake, Wanawake, Wanawake! Nimewaita mara 3

Carleen

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2018
Posts
8,407
Reaction score
28,836
Hi guys,
Sijawasalimu siku nyingi wacha tu Leo niwasalimu,

Naomba tu nisichokwe, kuna vijitabia kwenye jamii wengine hatuwezi vifumbia macho, wahusika nawasema vizuri tu na wengine humu wenye vijitabia hivyo nawakumbusha tu aiseeh' waachane navyo maana vinaboaa!

Kuna hii tabia hasa naona hawa warembo wa sahii ndiyo wamepamba nayo moto khatari, hivi huu ujasiri wadada wa kuwajibu ovyo waume ama wapenzi wenu mbele za watu mnatoa wapi?

Good Lord! Vidada vya sikuhizi havina kheshima jamani mpaka kero.! Yaani unakuwa pahala mpaka pa kuweka uso wako unakosa, kama ndiyo upo ugenini unatamani kuaga.!

Yaani huwa naishiwa pozi mpaka wakati mwingine nalazimika kutoka nje maana najiskia vibaya sana, nawaza tu Mimi nahisi vibaya hivi, je huyu nwanaume wa watu maskiini! Walaqhi' you guys are passing through hell uwiiih'.. Naanza kupunguza kuwahukumu kuna mambo sisi wanawake ndiyo chanzo, vile nisivyopenda mtu anidharau halafu naona mwanaume, Baba, Kichwa cha familia anadhalilishwa kiasi kile mbele za watu, yaani mwanamke hajali kuna watoto ama mgeni, anaropoka tu neno lolote linalomjia kinywani, wanawake wenye hii tabia kuni yenu inachochewa, mlivyoambiwa 'watiini waume zenu' hamkuambiwa bahati mbaya..!

Hivi ni kizazi gani kinatengenezwa sahii.? Ni ukosefu wa malezi? Ni hizi pesa wanawake wanazomiliki? Ni wanaume kuna mahala mnafeli? Ama ni gani.? Hii kiburi na jeuri wako nayo wanawake wa sahii ni ya dunia nyingine, wametoka nayo wapi, maana khali ndiyo inazidi kuwa mbaya, yaani inafika pahala you can't differentiate the two, hujui here who issa husband, who issa wife maana wote wamemea pembe!

Naomba niachie hapa sintomaliza, Wanaume ni lazima mfanye jambo haqyamama, Ile 'Manhood' kwenye jamii yetu inaenda kutoweka kwa kasi sana, Ladies punguzeni uzungu jamani, this is too much!
 
Siku hizi wanawake wamekuwa niwatu wanafanya vibiashara vyenye kuwapa 10000-50000 kwa siku sasa hiii huwapa Sana confidence wanawake nakuoa kuwa nawao wanaweza kuwa baba ndo maaan sikuiz masingle. Maza wanazid kuongezeka hapa mjini na wengine wanpenda kuwa masingle maza yaaan.

Pia wanaume wengi hapa mjin wamekuja kuwa wavivu mnooo kuliko wanawake so unakuta mwanamke anamvisha anamnunulia pombe na mda mwingine mwanamke ndo anasaidia familia ya mwanaume.

Hiii ni mbaya sana mwanamke kumpita mwanaume kipato niheriii mwanamke akupite umri ila sio kipato bana hawa wanawak hawa wakiwa juuu kifedha.

Bro hata huongeeee nn hakuna kitu atakuelewa . Hiii ilinikuta kipind nipo marioo sitak hela ila nataka mwanamke mwenye hela nilikuwa napigiwa kelele bar daah nakuitwa kaka kuku yaaan😂😂😂😂
 
Angalia PM

Ushapata mume tyr...


Hapo umemjumuisha na Mzazi wako wa like!?


Usirudie kusemea wote.. Tumia baadhi,,,,

BtN sielewi hao waropokaji wanaishi wapi? Au unazungimzia hao wa uswahilini a.k a vigodoro,, kila MTU anapata mwenza kulingana na alivo,,, wewe km ni wa vogodoro utapata vigodoro wenzio, saaasa ukiwa km jirani ukasikia wanaropokeana unatoka baluu kuja kupost huku,, wacha watu maisha hao yaendelee huwezi huo mtaa hama naenda sehemu zilizo staarabika...
 
Mimi ninajua kuwa mwanamke akisimama kwenye nafasi yake amepewa "mamlaka" ya kujenga ndoa yake.
Ukisoma (Mithali 14:1)-
Kila mwanamke aliye na "hekima"hujenga nyumba yake, Bali aliye "mpumbavu" huibomoa kwa mikono yake mwenyewe".
Mara nyingi napenda sana kumkumbusha mwali wangu kwamba "ACHUNGE SANA ULIMI WAKE" kwani maneno yanaweza kuleta uharibifu na maumivu zaidi ya fimbo, kisu, jiwe, bunduki au hata bomu.
Maneno yanaweza kuleta madhara na majeraha ambayo sio rahisi kuyaponya.
Maneno yanaweza kusababisha vifo. Ukisoma katika Mithali 18:21 neno linasema; “Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi."
Maneno tunayosema kwa ulimi bila kujali ni mazuri au mabaya, yanachoma. Katika Mithali 12:18 neno linasema; “Kuna anenaye bila kufikiri kama kuchoma kwa upanga; Bali ulimi wa mwenye haki ni afya." Maneno yakinenwa kwa kukurupuka, bila kufikiri hata kama hayakunenwa kwa lengo la kuumiza huchoma kama upanga. Kinyume chake maneno yakinenwa kwa busara na hekima huponya na kutia moyo.
 
Angalia PM

Ushapata mume tyr...


Hapo umemjumuisha na Mzazi wako wa like!?


Usirudie kusemea wote.. Tumia baadhi,,,,

BtN sielewi hao waropokaji wanaishi wapi? Au unazungimzia hao wa uswahilini a.k a vigodoro,, kila MTU anapata mwenza kulingana na alivo,,, wewe km ni wa vogodoro utapata vigodoro wenzio, saaasa ukiwa km jirani ukasikia wanaropokeana unatoka baluu kuja kupost huku,, wacha watu maisha hao yaendelee huwezi huo mtaa hama naenda sehemu zilizo staarabika...
Bado hujanielewa mpenzi wangu..!!
 
Bado hujanielewa mpenzi wangu..!!
Hebu tuambie research yako hao wanawake wa wapi?

MTU alielelewa maisha ya kustaarabika sizani km ataropoka ovyo,,,

Lkn kwakuwa mpango wako ni kuwasema wanawake wote,,, hii kitu nakataaaaaa!!!!!!!

Ila tu ntakushauri toka huko uswahilini uje huku ustaarabuni ubadilishe saikolojia ya akili yako kidogo .
 
Back
Top Bottom