Wanawake wanatesa wanaume mabwege

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,340
51,900
WANAWAKE WANATESA WANAUME MABWEGE!

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli

Unaleta mambo ya kibwegebwege Kwa nini usiteswe.
Unaleta Tabia za kibwege nazi, Acha unyooshwe.

Hakuna mwanaume Duniani mwenye Akili zake, anayejitambua alafu ateswe na Wanawake. Kitendo cha wewe kuteswa na Mwanamke kinatafsiri moja tuu, nayo ni Ubwege.

Bwege ni mtu asiyeweza Kutumia Akili, asiyejua nini chakufanya, Hana mbinu za kimedani, hajielewi, haelewi nini afanye, hajiamini. Yaani yupoyupo. Kwa Lugha nyepesi tunaita mwanaume mjinga. Bwege.

Yaani unahudumia Mwanamke alafu anakupelekesha, wewe ni Bwege Nazi
Unahudumia Mkeo alafu anakupimia, wewe ni Bwege.

Kuna Vijana MABWEGE huwaga nawaoneaga Sana huruma, yaani kakijana kutwa kanahangaika kubeba zege, kutwa kukimbizana na vumbi la Bodaboda, alafu kibwegebwege unatoa Pesa Kwa Demu alafu haupewi unachokitaka, wewe ni Bwege tuu.

Unajua Ubwege upo WA Aina nyingi, lakini hakuna Ubwege Mbaya kama kuteswa na Wanawake.

Ili ndoa iwe ngumu basi itahitaji mwanaume Bwege Vs mwanamke Mpumbavu. Hiyo ndoa itakuwa ndoa ngumu Mno.

Vijana, jiaminini, heshimuni uanaume wenu, tambueni thamani yenu, lindeni jasho lenu. Acheni Ubwege alafu mnakuja kupiga piga kelele huku kuwa Wanawake wabaya.
Wanawake lazima wawachezee shere wanaume MABWEGE ili wakale na wanaume wenye Akili(wanaojua thamani ya uanaume).

Embu fikiria;. Pesa umetafuta Kwa nguvu, ukaipata, umerudi nyumbani au umetafuta demu, unambembeleza ili atumie Pesa zako, anachukua alafu bado anakunyima, kudadadeki huo usengerema huo,ubwege huo! Taikon Hilo kwangu ni kama nimejiua. Haliwezekaniki.

"Baby, nimekutumia elfu hamsini"
Anajibu; hiyo haitoshi, nilikuambia laki na nusu"
Alafu wewe Kwa Ubwege wako unabembeleza kum-please, yaani kama jinga Fulani hivi
Kwa nini asikudharau?

Hata kama kijana unasura personal, Sura ngumu hiyo sio sababu ya kuwa Bwege, boya wee!
Hata kama haujasoma hiyo sio sababu ya kuwa Bwege yaani uteswe na Wanawake.
Hata kama hauna Pesa hiyo sababu ya kuwa Bwege na kuteswa na Wanawake.

Wewe ni Mwanaume, Acha uboya, jiamini, fanya kazi, tafuta Pesa, utakachojaliwa hichohicho. Usitumie Pesa Kupata Wanawake, huo ni Utumwa, Ubwege la walivyo MABWEGE wengine, labda kama unanunua Makahaba, hapo Sawa.
Kwanza ukinunua kahaba hawezi kukufanya Bwege Kwa sababu wewe ni mteja, na mteja siku zote ni Mfalme.

Lakini hawa sijui mnawaita wapenzi sijui Wake ambao wanawaburuza ninyi MABWEGE Kwa ujinga wenu, msikubali.
Hataki apite kushoto.

Hupaswi kumtii Mwanamke huo ni Ubwege. Yeye ndiye anatakiwa kukutii.

Kama Mwanaume usiwe MTU wa kujali Matokeo hasa kwenye ishu za mahusiano pale heshima yako inapokuwa mashakani. Kuwa aggressive, mkali na usiyetaka mchezo.

Ooh! Akiniacha Watoto wataishije, wataishije kwani wewe ndiye uliingia Labor? Watakuwa Hawana maadili, yaani mawazo ya kibwege.
Hivi uliona wapi Familia ambayo Baba anaburuzwa Watoto wakawa na Maadili? Wapi uliona tuje tuone maajabu ya Dunia!

Acheni Ubwege Vijana.
Kutokujiamini, uoga, kudekadeka, umario na uvivu na kuvizia vipesa vya Wanawake ndio kunawafanya kuwa MABWEGE.
Udomo zege, uwezo mdogo wa kushindwa kupata MKE mwingine kunawafanya kuwa MABWEGE.

Uliona wapi Mwanamke akamburuza mwanaume ambaye anauhakika wa Kupata Wanawake wengine zaidi yake, wapi?
Leta ujinga tukuonyeshe Sisi ni wajinga kukuliko, tunaanzisha Darasa la wajinga wenzako kama kumi Mimi niwe Mwalimu wenu.

Usilete dini Kwa Mwanamke anayekuburuza anayekuburuza Bwege.
Tumia mkono wa Chuma na akili.
Usilete mambo ya Elimu sijui uzungu Kwa Wanawake wenye tabia za kuburuza wanaume, tumia Kanuni ya Uafrika Halisi.

Asije akakudanganya kuwa utakosa Wanawake, hakuna mwanaume kamili akakosa Mwanamke, hajawahi kutokea.
Ikiwa wanajiuza Huko Kwa nini uhofie kukosa Mwanamke. Hufanyi kazi? Kama unafanya hupati Pesa? Embu Acha Ubwege.

Oooh! Mimi nataka MKE na Familia. Ni Sawa lakini ndio ugeuzwe Bwege? Familia ni muhimu ikiwa Protocols zote zinafuatwa, heshima na nidhamu Kwa MKE zinazingatiwa. Lakini sio tunakuona unakonda, Unalalamika unanyimwa sijui unanuniwa, ujingaujinga tuu.

Kama hawezi kukupa mwambie afutike, kama hawezi kuishi Kwa kutabasamu Aende kwao akanunie Ndugu zake Huko.
Sio kuendekeza ujinga.

Yaani unahangaika kwaajili ya familia, bado jitu linakuhangaisha, linakutesa.
Ati kuna wengine anajiamualia tuu vyovyote anavyotaka, sijui nataka mtoto wangu asomee shule Fulani alafu Mwanamke Mwenyewe anayesema Hana kazi, alafu anajua kabisa mumewe kipato kidogo alafu nawe Kwa Ubwege wako unateseka, hao Wanawake tuleteeni Sisi huku alafu watarudi Huko kuwapigia magoti. Kumbavu!

Acha nipumzike maana ninahasira Sana. Wadogo zangu, acheni upuuzi! Kuweni Wanaume.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Wanawake daima wanakuhangaisha wakisha jua udhaifu juu yake.....na udhaifu unaonekana pale mwanzo wa mahusiano kwenye Yale unayoita mahaba......

Mwanamke anatakiwa uishi naye huku akijua mipaka yake na akivuka mipaka ni kumuonesha kuwa wewe ni mwanaume kamili...Kwa kufanya maamuzi magumu..........

Ukiwa na uwezo wa kustahimili maumivu ya kuachana na mwanamke basi wewe hakuna mwanamke Duniani atakufanya bwege......

Ishi na mwanamke kwa wema lakini mfanye ajue kuwa unaweza kuacha naye muda wowote akitoka nje ya mstari......
 
Wanawake daima wanakuhangaisha wakisha jua udhaifu juu yake.....na udhaifu unaonekana pale mwanzo wa mahusiano kwenye Yale unayoita mahaba......

Mwanamke anatakiwa uishi naye huku akijua mipaka yake na akivuka mipaka ni kumuonesha kuwa wewe ni mwanaume kamili...Kwa kufanya maamuzi magumu..........

Ukiwa na uwezo wa kustahimili maumivu ya kuachana na mwanamke basi wewe hakuna mwanamke Duniani atakufanya bwege......

Ishi na mwanamke kwa wema lakini mfanye ajue kuwa unaweza kuacha naye muda wowote akitoka nje ya mstari......

Umesema kweli yote.
Wema ni pamoja na kuhakikisha MKE havuki mipaka yake
 
Ukiwa Huna hela lazima uchekechwe tuu , Ila kama hela ipo wanawake utawaogelea Sana , huwezi kumzingua pisi kali kama huna hela ni ngumu Sana mana kuna wahuni wenye shekeli watakuwa wanampa kiburi na atakuwa anawanyenyenyekea kinyama Ila wewe unapelekwa mwendo wa ngiri mkia juu😁😁😁
 
Back
Top Bottom