Caroline Danzi ni nyie wenyewe mnawaendekekeza, ni kwa sababu wameona kwamba inawezekana kupata jimama la kumlea kwa malipo ya ngono na ndio sababu ya kila kijana mvivu analala akiota zali la mentali......
Na hiyo iko kote kote maana pia vipo vibinti hufukuzia wazee waume za watu kwa ajili ya kujikwamua kimaisha na yote hiyo ni kutotaka kuwajibika kwa maisha yao.
Kuna haja ya kuanzisha darasa la ujasiriamali humu ili kila mtu ajitegemee.
Kuna malalamiko mengi humu ya wanaume wakidai kuwa wake zao wanafanya kazi lakini hawako tayari kuchangia matumizi ya nyumbani hilo nalo pia ni tatizo, na wanawake wanahalalisha kabisa kwamba hilo sio jukumu lao.
Lakini unadhani hilo limetokana na nini?
Ni malezi tu, na ndio maana inashauriwa kama unampata mwenza kuna haja ya kuchunguza familia atokako. Kwani malezi ya wazazi yana mchango mkubwa wa kuathiri tabia na mienendo yetu...
Nitazungumzia jambo hili kesho....................