Wanawake walio wengi huvutiwa na wanaume walio warefu. Achilia mbali vitu kama Mshiko(ATM) nk ambavyo vinachangia lakini huwa wanajisikia fahari kuwa na mwanaume mrefu.
Wakuu ktk pitapita zangu za kila siku nakutana na minong'ono kuwa wanaume warefu wana mvuto mkubwa kwa wanawake tofauti na wenzao wafupi.
Hii nimeisikia kwa baadhi ya wanaume wakikiri kuwa wanaume warefu wanakubalika kirahisi kwa wanawake, basi nikajaribu upande wa pili nisikie wenyewe wanachosema, wengi wamekiri kuwa wanaume warefu wana mvuto sana ila tatizo ni mila na desturi za kwetu haziruhusu mwanamke kumtongoza mwanaume.
Mwingine akaniambia kuwa wanaume warefu wengi wao wana confidence na wanajikubali sana, wapo wengi tu wanaokubali kuwa wanaume warefu wanakuwa ni wenye mvuto, sasa wanawake wa JF na nyie mnasemaje?