Wanawake tuna maneno

Wanawake tuna maneno

Mi kuna mmoja aliniharibia Mahusiano yangu ya kimapenzi...

Halafu akawa anamtongoza huyo mwanaume...

Tokea hapo wanawake niliwavulia kofia
Ndio tabia zetu. Na ukute kukuharibia kote hata kudumu naye hajadumu naye.
 
10810040_1504226659850615_1023255191_n(1).jpg
 
Pole sana.. Kwani wewe ni mzuri? Kama wewe ni mzuri wanawake wenzako hawataacha kukuletea maneno...
 
Hivi sisi hatuwezi kuwa marafiki mpaka tusemane vibaya, yani usipomsema mwenzio unaona siku haiendi au inakuwaje, unakuta unakuwa na rafiki mnasaidiana kwa hali na mali lakini au akiwa na shida unamsaidia tena vya kwake mchoyo kweli, unajitoa kwa kila kitu lakini utakuta linakusema vibaya sijui ni wivu, chuki hata sielewi aisee!

Hii tabia tunayo sana wanawake tubadilike jamani, maisha yashakuwa magumu maneno ya nini, mimi nishaamua sasa niwe mwenyewe tu sitaki marafiki maana ukigeuza tu mgongo wauaji, halafu ukitaka kukumbuka kitu ambacho umemuudhi huoni au ukimuuliza anasema hakuna kitu yaishe tu nisamehe.

Au wengine bila kusema wenzao siku haziendi vizuri "lazima tuji control "
Yaani nishaamua toka mwaka jana hakuna rafiki yeyote kushika simu yangu, wala kujua password, misele yangu napiga kimya kimya, sitambulishi mpenzi wangu tuonane wenyewe tu. Maana maneno mengi mpaka unachoka.

Wanawake sisi ni kibokooo

Mara hii mshatibuana na Rukia?

Au Pendo ndo kakukwaza?
 
Pole sana.. Kwani wewe ni mzuri? Kama wewe ni mzuri wanawake wenzako hawataacha kukuletea maneno...
ilo nalo neno maana ukiwa mzuri unaringa ukiwazidi kidogo tu unaringa na hela sijui anapata wapi basi tabu tupu...
Tungekua tunapendana kweli kweli na kushikamana kusaidiana km ilivyo kwa me tungekua mbali
 
Back
Top Bottom