Wanawake tulieni kwenye ndoa zenu

Wanawake tulieni kwenye ndoa zenu

Watangazaji,wakina Mama wanaoalikwa na motivational speakers wa kwenye tv na redio ni kirusi kingine Cha ndoa.

Ukimuona mkeo anafuatilia hivyo vipindi jua ndoa yenu iko mashakani au soon itaingia migogoro.
Na akianza kufuatilia tu ujue
Hapo kuna shida hyo ndoa haimaliza
Miez kwakweli utaanza kuona challenges nyingi sana
 
Juzi naona Carol Ndossi anasema mwenza kushika simu ya mwenzie ni kosa kisheria hata sijui sheria yenyewe kaitoa wapi, madanga na malaya wakashangilia sana.

Btw watu wamekua sio waaminifu tena uzinzi umetawala kila kona na hawa motivation speaker kwa kutaka ku-gain followers na kupiga pesa wamekua wakiwahadaa kwa maneno ya negative ili wawasapoti.

Mwingine utasikia anawaambia mwanamke tafuta pesa yako ili mwanaume asikunyanyase, najiuliza kwanini wasitafute chanzo cha manyayaso, ama wasitoe darasa kwa hao wanaume wanaoona wa awanyanyasa wake zao.

So wanawa-motivate wanawake watafute pesa then wawe wababe
Ushauri wao hauendani na mazingira. Haya ndiyo madhara ya copy and paste vitu vya Ulaya. Hata Ulaya kwenyewe mambo hayako kama hao ''washauri'' wetu wanavyosema. Mimi nadhani ndoa iliyotulia issue ya kushika simu ya mpenzi wako siyo jambo la kujadili wala kuweka maamuzi. Ni kitu mnajikuta mnakifanya naturally i.e. hamviziani wala hamhisiani wala hamfichani. Ukishaona kwenye ndoa wenza wanawekewana masharti kwenye kushika simu ya mwingine basi ujue tayari kuna tatizo. Na pia ukiona wenza wanavizia au wanapekuana kwenye simu bila sababu ya msingi basi ujue kuna tatizo. Inatakiwa mmoja anapoomba simu ya mwingine aombe kwa nia njema na siyo kupeleleza. Na mwenzake naye asiweke masharti ya simu yake kuchukuliwa.
 
Kwanza Kwa usaliti kwenye ndoa wanaoongoza ni wanaume Kwa wingi mkubwa!

Kwa hiyo acheni ubabe!
Mimi ni mwanaume na nakubaliana na wewe. Wanaume ndiyo wasaliti zaidi na wanakuwa wakali sana wanapogundua wenza wao nao wamechepuka. Kwa kifupi mila na desturi za kiafrika zinaona mwanaume kama ana haki ya kuchepuka lakini mwanamke hana.
 
Mie nipo upande wa wanaoliza chuma tu!

Jana nilisoma somewhere jamaa kaondoka na kichwa cha mkewe madai alikuwa anamsaliti na mwenye nyumba mganga.mtu anaulizwa kinachokupa jeuri si hii sura sasa ngoja nikuonyeshe,zinalia saba unadhani kuna kitakachosalia hapo?
 
Wanaume wanaisha wallah.....mnaogopa maumivu badala ya kuyakabili.

Unaua mwanamke ulizaliwa nae tumbo moma kusema huwezi kuishi mkitengana nae!? Mapacha tu wanatengana sembuse wewe na mkeo.

Na hapa sio suala la mke kuwa mkaidi, ni mwanaume kutafuta mke unayemmudu bila hivyo mtazidi kuoa wake wasio wenu kisha muue kila kukicha kwa kutokuamini mnachokiona
Na ww kwanini uolewe na mwanaume ambae
Unaona huyu atakusumbua

Ikiwa unaona huyu mwanaume sio msumbufu
Na ww tabia yako na yake hamuendan
Kwanini uolewe nae

Ujinga mmoja n mtu kuthan atambadilisha
Mwenzake wakiwa ndan ya ndoa kitu ambacho
Maranyingi kinashindikana
 
Ugali ulivyomtamu hivi ukiupatia mbona nzuri zilizoungwa nazi Kwa ugali ulosongwa ukasongeka eti uharibifu maisha yako kwaajili ya mwanamke?

Halafu sio kusema yuko peke yake huku Dunia la hasha wako wengi tu,

Mmnh hapana nakataaa mimi madhira!

Na Mwenyezi Mungu anisaidie siku zote subira na uwezo wa kustahamili mitihani na kuishinda!
Hivi Tanzania hakuna ile ndoa ambayo moja ya masharti yake ni kuwa wnandoa hakuna ku-share mali bali kila mtu anakuwa na hesabu yake?
 
Mi naona Kama ingekua vizuri Mwanamke ndiyo atafute Mume atake mmudu na atakae weza vumilia uzinzi wake, maana Wanaume wa hivyo pia wapo kibao, yaani hata Kama Mke wake asiporudi Nyumbani kwa siku tatu yeye atavumilia tu bila kinyongo!!!
Mwanaume WA hvo unless ampate shoga tu
 
Kuna ule ujnga WA kua unaona
Huwez kuish bila yeye huu ndo upuuz
Unaosababisha majanga yote

Mtu anaona anampenda mwenzie
Kias kwamba hawez kuish bila
Yeye na kumuacha hata

Kuuwana ndo kuana ndo kuaanzia hapa
 
Hivi Tanzania hakuna ile ndoa ambayo moja ya masharti yake ni kuwa wnandoa hakuna ku-share mali bali kila mtu anakuwa na hesabu yake?
This is Africa bro hili bara tunatambua
Mwanaume ndo kichwa cha familia
Ndo mwenye kusema
 
Unaeleza kabisa kuwa ulimpa ukizani mtaendelea kuishi pamoja Kwa kusikilizana lakini imekuwa kinyume hivyo nahitaji kurejeshea mali zangu na fedha zangu haraka kabla sijawaza na kufanya vibaya.
Ktk sheria hakuna kitu kama “nilidhani” sheria itataka kufahamu kama hivyo unavyodai ni vyako vimeandikwa jina la nani?na vitakuwa vya yule aliyeandikwa kama unavitaka utaambiwa mwambie akuuzie kama anauza.na hizo kauli sijui “sijawaza kufanya vibaya” ipo siku danga lake lingine litataka kumkomesha uonekane ni wewe maana ulishatoa vitisho hadharani.

Let say kitu kimeandikwa Akilinjema bin Fulani mimi leo nikaseme hapana ni changu nitaelewekaje?Haya,ulimpa onyesha maandishi mliposainiana huna utataka bado kusema mali ni zako?wasaliti acha wapunguzane.

Maisha na mali usichukulie ni vitu vyepesi kiasi hiko maana even yule anayetoa siyo kwamba anatoa ameridhika anazo nyingi hasha anatoa kwa sababu tu imebidi iwe hivyo.
 
You have two options dear brethren;
..USIOE au
..OA ZAIDI YA MKE MMOJA.

Ukifanya hayo utaishi na kuona vitukuu, short of that 50yrs ushazeeka au utakufa mapema.
 
Hizi nyakati ni moja kati ya nyakati mbaya sana kwa waungwana kuingia kwenye mahusiano au ndoa.....hizi ni nyakati ambazo ukimpenda mtu basi ndio umempatia ufunguo wa manyanyaso na mateso maishani mwako..........hakika utaijutia nafsi yako na utaulaumu moyo wako kwa kukushawishi kutumbukiza kwenye dimbwi la mateso badala ya raha.....
 
Mnaexaggrate mambo tu, hivo vitu vizito havijaanza leo vilikuwepo tangu enzi na enzi ni vile tu enzi hizo WANAUME WALIKUA NI WANAUME, walijua namna ya kutumia akili si ndio maana baba alikua akitoka safari anafikia kijiweni anampa mtoto koti apeleke home ye anakuja baadae....#ongeeninawazee

Anampa koti apeleke nyumbani ili mkewe kama alikuwa na hawara amwondoshe mapema, na ajue mkubwa wa kaya amewasili...lakini ole huyo hawara abainike bayana, atakatwa mtu nyeti...
 
Kuna article nilisoma, "as you educate and empower a girl child, don't forget that a boy child needs the same treatment. "

Nguvu kubwa sana inatumika kumuelimisha binti, inasahau kuwa kijana wa kiume nae anatakiwa kufundishwa jinsi ya kuishi na huyu binti. Tinajenga kizazi hovyo kabisa.
 
Anampa koti apeleke nyumbani ili mkewe kama alikuwa na hawara amwondoshe mapema, na ajue mkubwa wa kaya amewasili...lakini ole huyo hawara abainike bayana, atakatwa mtu nyeti...
Hamna cha kukatwa nyeti weye, wanaume hawakua maboya kama hizi new breeds, enzi hizo hata mama kuzaa watoto wa nje ilikua kawaida tu yani katika ya watoto 6 wa dingi unakuta wawili sio wa dingi na dingi anajua kabisa na maisha yanaendelea.....siku hizi ni kubana pua dieniei, #ongeeninawazee
 
Back
Top Bottom