Napinga kabisa suala la kupongeza wanawake wanapopata fursa za juu. Tuwapongeze wanapodeliver quality service kwa umma mpana wakishashika nafasi hizo. Nasema hivyo kwa sababu ya kinachotokea bungeni hivi sasa. Kama mnafuatilia bunge kwa makini, kama mnafahamu unyeti wa mswada wa Mabadiliko ya Katiba uliolazimishwa kusomwa bungeni kwa mara ya Pili badala ya mara ya Kwanza, na kama mmefuatilia na kuona mchango wa wanawake wengi tena wenye madaraka wanavyotumia nafasi zao hizo kukandamiza sauti na matakwa ya wananchi, basi utaungana nami kwamba badala ya kuwapongeza wanawake hao watatu, tujitokeze hadharani kusema wazi kuwa wanawake walioko bungeni tuliodhania watasimama kulivusha taifa, wanaliangusha taifa!