Wanawake nyie endeleeni kuringa tu

Wanawake nyie endeleeni kuringa tu

Msichana ana miaka 22, anafuatwa na mvulana na kuambiwa kwamba anataka kuolewa, mvulana yupo kamili kajiandaa na anamaanisha, msichana anakataa kwa visingizio vya kipumbavu mvulana anaachana nae.

Anachokifanya ni kumfuata mvulana ambaye hana mpango wa kumuoa kisa gari kisa fedha anataka kuitwa mpenzi na mambo kuishia kitandani anavuliwa pichu.Haiishii hapo anapofika miaka 23, 24, 25, 26 hali inakuwa hivyo hivyo kwake anajiona hana haja ya kuolewa anaamua kuwa na mpenzi tu, leo huyu kesho huyu na keshokutwa yule.

Siku hazimsubiri miaka 27, 28, 29 na 30 inaingia hapo ndipo anashtuka kwamba kapoteza muda na anatakiwa kuolewa.Hahaha! Mungu sio chizi aliyajua maisha yako ya mbele ndio akakuletea wanaume mbalimbali wa kutaka kukuoa lakini ukakataa kwasababu zisizo na mantiki.

Mwenyewe unaona muda wa wewe kuolewa umefika lakini hauolewi unaanza kuangaika huku na kule kila mwanaume kwako anaonekana kuwa muhimu. Yaani wakati ambao haukuuhitaji ndoa, ndoa ilikuhitaji na wakati ambao unaihitaji ndoa wanaume wana-HIT & ku-RUN.

Kwa mahesabu kama una miaka 30 inakupasa kuolewa na mwanaume mwenye angalau miaka 33 au 35. Je kuna mwanaume mwenye umri huo ambaye yupo tayari kuoa? Mwanaume hataki kuitwa babu na mtoto wake anataka kuitwa baba. Mwanaume anapofikisha umri wa miaka 30 anaweka jiko ndani lenye miaka chini ya 25.

Sasa kama kipindi alichokuwa na miaka 30 ukamkataa, wewe ukiwa na miaka 30 mwenzako ana 35 kashaoa kitambo na kama MUNGU kamjalia ana watoto wawili.Sikulazimishi uolewe ila unapopata mwanaume aliye tayari kukuoa kubali tu, ndoa ni bahati kuna wanawake wanafikisha miaka 40 na bado hawajaolewa na kila siku wanatamani kuolewa.

Unapoipata bahati fanya mambo.Siku zote mwanaume anapokwambia kwamba anataka kukuoa ukaleta pozi weeeeee, akija kwa mara ya pili huyo si muoaji, atakuja akuchezee na kukuacha kwani anajua pia we haupo tayari kwa kuwa alishakupa nafasi ukailetea pozi.

WANAWAKE WAPO MILIONI 29 TANZANIA NA WANAUME MILIONI 25. HALAFU WEWE UNALETA POZI.HAYA, TUTAONA MWISHO WAKE.
umenivunja mbav kwmb wao wapo mil29 na ss tupo mil25 alafu wanaleta poz.
 
Kama vile unanisema mimi, niliwahi kupendwa na wanawake si chini ya wanne, walikuwa wakijilengesha na kujitongozesha kwa kweli ilibidi niwakubalie tu shingo upande, walikuwa wazuri kiasi na wengine wazuri sana, pamoja na kuwa walinipenda sana kila mtu kwa nafasi yake, walinithamini sana lkn mimi ile feeling ya kutoka moyoni kabisa haikuwepo nilibaki kuzuga tu.

Tulikuwa tunagegedana tu utamu tunapata lkn love hakuna.

Wengine walinifanyia mambo makubwa na zawadi kedekede lkn wapi.

Na niliishia kuwatupa tu.

Haya uyasemayo ndivyo yalivyo, mwanadada epuka wakati huu usikufikie ni nyakati mbaya sana kuwahi kukutokea maishani.

nb: kupendwa raha bhana.
 
Kuolewa sio lazima..
Ila kwa mazingira yetu kibongobongo wanawake wengi hawajishughulishi wenyewe wengi wanategemea neema toka kwa mwanaume (siungi mkono swala hili)..
Kwahio kwa kukosa kitu mwanamke anaona ulazima wa yeye kuolewa..
Matokeo yake mwanaume akija na gear ya kuoa tu anakubaliwa..

Wanawake mjishughulishe ili mjikomboe kiuchumi
Hamtokuwa tegemezi kwa mwanaume tena and your struggle for gender equality will make sense even more..
 
Msiwape watu stress, kama hajakupenda basi kubali haujapendwa...sio sababu una ahaidi ndoa ndo ajilazimishe kuolewa na wewe. Unajuaje na huyo mwingine hajamwambia anataka kumuoa kama wewe unavyosema.
They will marry when and who they want.
Hizi topic mkawaambie dada zenu nadhani ndo hawana haki ya kupenda au kuchagua wanachopenda.
Basi ameona Ahadi yake ya ndoa ni jambo la maana. Kila mtu ana priorities zake bwana. Wasiwachoshe wasichana wa watu.
 
Aaahhaaaaa... Asante kwa lesson.. There are some people are married at 18 years old while are going to school ( College or University) ... And life moves on smooth... Thanks..
Haya ni maisha, sidhani kama kuna formula katika kuyaishi, maisha yako si ya mwingine and vice versa, kila mtu ataishi atakavyo. Relax.
 
Hakuna heshima ya mwanamke hata aweje kama hajaolewa, hata awe na miaka 45 hajaolewa na bint Ana 22 kaolewa basi jamii inampa heshima zaidi bint wa 22 kuzidi huyu mwenye 45 Ndio inaheshima yake bwana
 
Mwanamke unatakiwa utulie upendwe halafu wewe ndo upende, Mwanaume ukianza kumpenda huwa yanatokea yafuatayo:
1)Hata uwe mzuri kiasi gani au uwe na tabia njema kiasi gani atakukubalia haraka haraka ila moyoni anakuwa anakuzarau sana so anakutumia kwa madharau excessively then anakudump, anaweza hata akataka tigo!!!
2)Ukianza kumpenda mwanaume huwa anachukulia kuwa unajipendekeza na ni dharau!
3)Mwanaume hata umpendeje kama hakupendi hawezi kubadilika akupende kamwe na ataishia kuchepuka!
Have you ever being a woman even for five seconds! ? Unapata wapi ujasiri wa kutuongelea as if your into Us, yaani unamaanisha tuchukuliwe tu tutapenda mbele kwa mbele? Hivi kuna kitu kinaitwa "kujifunza kupenda" au it's just a myth mi nadhani kuna "kumzoea" mtu na kukubali hali .
Hivi wanaume mnajua how miserable kulalwa na mtu usiyekuwa na hisia naye hasa kama hujawahi kuwa "kahaba".
 
Wengi humu kwenye huu uzi hawajaolewa na wengine inaonesha wamezalishwa tuuuuu
Hivi mnajiskiaje mnapoulizwa baba yake huyu ni nani? Mbona hatujawahi mwona?
Au mtoto shuleni akiambiwa amlete baba yake inakuwaje?

Oleweni tu
Eti mnapenda watoto tu nyau nyie
 
Binti, kubali any marriage proposal ya kwanza unayoipata... hiyo ni bahati imekudondokea, la sivyo utakoma baadaye.

Binti, ukimaliza tu form six au hata form four, anza tu kuwaza ndoa...maana ukifika 30 yrs old hujaolewa, hamna namna tena, wewe umekwishaaaa

Mwanamke, unashauriwa hapa kuolewa mara tu chance inapojitokeza, hata kama ni mtu ambaye hujampenda, (take risk), utaenda kumpendea mbele ya safari... (na kama usipofanikiwa kumpenda...well, labda thread nyingine itaanzishwa kuhusu hilo)

Binti/mwanamke, Moyo wako ukimpenda mwanamme kabla ya yeye hajajua unampenda, uzuiye huo moyo kabisa, usithubutu kumwambia huyo mwanamme, vumulia mpaka atakapokupenda yeye kwanza, la sivyo atakudharau mama.

Binti, wewe ni mwanamke, siku zote inatakiwa utulie tuliiii upendwe kwanza, alafu wewe ndo uanze kuufundisha moyo wako kupenda. Usitake kuleta fyokofyoko za kuanza kupenda ile jinsia nyingine kabla wao hawajakupenda.

Mwanamke, na utakapofika 30yrs old bado hujaolewa, usilete ushetani wako wa kuwalaghai "innocent married men", wao wametulia ndani na wake zao, nyie mnaenda kuwashikia bunduki mzae nao, acheni hizooo, nyie si msilikataa kuolewa mkiwa chuo?

Salamu zimfikie besti wangu housegirl
 
Hahaha what an artist you are!!

You've summarised everything perfectly.

Nashangaa mabinti wanavyojitia kiherehere kupenda.

Nimekumbuka kitabu Three Suitors One Husband, binti anamuambia bibi amepata mwanaume aliyempenda, hao watatu waliojitokeza kutoa mahari hawataki. Bibi akauliza "Nani kakuruhusu kupenda??"

Poleni wanawake. You've a long way to go.

KayScarpetta
 
housegirl, Hello besti!
Mhhhh...mwenzio hapa napachungulia kwa uoga uoga...mhhhh...what with being diaognosed with a psychological disorder...mweee...this region is still largely a mans world besti.
Kwa fikra za aina hii hata hayo mapinduzi ya kiuchumi kwenye hili taifa hatutafika leo... Kule kwenye lile jukwaa letu lingine la kupigania taifa, wanasiasa (of which the majority are men, offcourse), hawana fikra tofauti na fikra zilizoko kwenye huu uzi besti.

Nasema hivyo kwanini? Huu uzi una viashiria vinavoonyesha kwamba wanaume wengi wanao-support hii post, wanaogopa mapinduzi ya kifikra ya mwanamke wa leo. Na wale wanasiasa wa kule (wengi wao wanaume), nao pia wanaogopa mapinduzi ya kifikra yanayoikumba hii dunia, kwasababu, wanafanya kwa makusudi kabisa mambo yanayoturudisha nyuma enzi za ujima, hawataki kabisa wananchi wa hili taifa 'waerevuke'. Wanataka wananchi waendelee kuwa gizani ili wao wapate chance ya kuendelea kuwatawala... do you see the similarities?

Mapinduzi ya kiuchumi besti, lazima yaende parallel na mapinduzi ya kifikra. It is very simple, huwezi kupigia debe swala la kujikomboa kiuchumi while at the same time, unapigia debe swala la kumuoa binti akiwa 20yrs old bado hajajitambua na bado yuko kwenye harakati za kujiendeleza kielimu na kiuchumi, eti tu kwasababu wewe ni mwanamme utamtimizia kila kitu. Huwezi kuwa mwanaharakati wa maendeleo kama bado unafikra kwamba eti mwanamke akiwa 30yrs old, eti amechoka, amezeeka, eti ameshapigwa pum*****u sana kwa hiyo amekwisha.

It is still a mans world besti...but it would be nothing, nothing without a woman...hahahaha...and we women, will deal with them accordingly... teh teh teh...
 
Ingekuwa Kuolewa ni kama kuku basi wasichana tungeolewa sana. basi hamna haja ya kupenda,mtu akikutamkia tu unaolewa.duuuu wanaume mnachonga sana.mkikataliwa tu mnakuja kulialia humu.
 
Binti, kubali any marriage proposal ya kwanza unayoipata... hiyo ni bahati imekudondokea, la sivyo utakoma baadaye.

Binti, ukimaliza tu form six au hata form four, anza tu kuwaza ndoa...maana ukifika 30 yrs old hujaolewa, hamna namna tena, wewe umekwishaaaa

Mwanamke, unashauriwa hapa kuolewa mara tu chance inapojitokeza, hata kama ni mtu ambaye hujampenda, (take risk), utaenda kumpendea mbele ya safari... (na kama usipofanikiwa kumpenda...well, labda thread nyingine itaanzishwa kuhusu hilo)

Binti/mwanamke, Moyo wako ukimpenda mwanamme kabla ya yeye hajajua unampenda, uzuiye huo moyo kabisa, usithubutu kumwambia huyo mwanamme, vumulia mpaka atakapokupenda yeye kwanza, la sivyo atakudharau mama.

Binti, wewe ni mwanamke, siku zote inatakiwa utulie tuliiii upendwe kwanza, alafu wewe ndo uanze kuufundisha moyo wako kupenda. Usitake kuleta fyokofyoko za kuanza kupenda ile jinsia nyingine kabla wao hawajakupenda.

Mwanamke, na utakapofika 30yrs old bado hujaolewa, usilete ushetani wako wa kuwalaghai "innocent married men", wao wametulia ndani na wake zao, nyie mnaenda kuwashikia bunduki mzae nao, acheni hizooo, nyie si msilikataa kuolewa mkiwa chuo?

Salamu zimfikie besti wangu housegirl
Kwa nini ubakwe eti kuiogopa miaka 30? Huko ni kubakwa hakuna upendo wa mbele kwa mbele
 
loading error..................................
 
Back
Top Bottom