Wanawake na mauongo yao ya saluni haya hapa….!

Wanawake na mauongo yao ya saluni haya hapa….!

wedd9.jpg


hair-salon.jpg


Kwenye
Saluni nyingi za wanawake, mazungumzo mengi yanahusu maisha ya watu na
hasa kuhusu mapenzi na kipato, kashfa na saikolojia zisizo rasmi kuhusu
ndoa na uhusiano. Kuna mazungumzao ya kukatishana tamaa na kuumizana
zaidi, kwa sababu kila mmoja anajaribu kuonyesha kwamba ana nafuu
fulani.

Lakini mbaya zaidi ni kwamba, saluni za wanawake hutumiwa na wanawake
hao kama maeneo ya kusemea hisia zao chungu na kutoa jumuisho kuhusu
wanaume na uhusiano. Huko saluni hakuna wataalamu, bali kuna
wazungumzaji ambao wanaamini wao ni wataalamu, na wengine kwa sababu ya
kuzidiwa na mzigo wa matatizo hasa ya uhusiano na pengine ya kipato,
huwaaamini hao wataalamu wasio rasmi.

Huko saluni ndiko ambako wanawake wanaambiana`kwamba, mwanaume akiacha
kufanya tendo la ndoa kwa wiki moja na mpenzi wake, ni lazima mwanaume
huyo atakuwa na ‘nyumba ndogo.’ Ndiko ambako wanafundishana kwamba,
ukipata Mganga wa nguvu unaweza kumshika mwanaume. Ndiko huko ambako
hutajwa orodha ya wanawake ambao wamewashika waume zao kupitia kwa
waganga. Ndiko huko ambako majina ya waganga maarufu hutajwa.

Lakini ndiko huko saluni ambako, wanawake hutaja orodha ya wanawake
wenzao waliopata mali kupitia ‘mabuzi,’ ambao huwapa mitaji ya biashara
inayowawezesha kusafiri hadi Uchina. Pia hutajwa majina ya wanaume
wanaohonga sana. Ni saluni ambako wataalamu wasio rasmi hutoa suluhu ya
matatizo ya ndoa. Ndiko ambako wataalamu hao huwaambia wanawake wenzao
kwamba, ukimuonyesha mwanaume kwamba unampenda sana, atakudharau na
kukuacha.

Kwa hiyo mwanamke akitoka saluni anakuwa ametoka shule anayoiamini .
ambapo huacha kumwonesha mumewe kwamba, anampenda. Ni wazi shule hii ya
saluni haijui kwamba, unapoonesha kutokupenda, nawe utaoneshwa
kutokupendwa. Kwani unachopanda ndicho unachovuna. Wakati mwingine
shule hii inajua jambo hilo, isipokuwa inataka waliopotea na
kuharibikiwa wawe wengi.

Ni huko saluni ambako utasikia wanawake wakifundishana namna ya
kuwadanganya wanaume zao. Hufundishana namna ya kujenga nyumba bila
kunaswa na mume, kwani wanaume hawaaminiki, huwezi kuacha kujiandaa.
Lakini shule hii haijui kuwa, hiyo ni sumu kubwa kuliko sumu nyingine
kwenye ndoa, kutafuta mali na kujenga msingi wa kipato kwa siri.

Ni hukohuko saluni ambako wanawake huambiana uongo kuhusu wakwe,
watoto wa kambo, na mawifi. Hufundishana kwamba, kumpenda mama mkwe au
wifi ama mtoto wa kambo ni kutafuta muhali. Haiishia hapo huendelea
kufundishana hata namna ya kuwachukia watu hao.

Mwanaume, kama ukiona mwenzi wako anakwenda saluni na akitoka
huko amekuwa mtu mwingine kabisa, unapaswa kujua kwamba, huenda amepata
‘dozi’ ya wataalamu hao.

Wanawake, nawashauri jihadharini sana na maneno ya saluni. Kwani
katika kila maneno mia moja, ni moja tu linalokaribia ukweli. Kumbuka,
linalokaribia ukweli . siyo kuwa ni la kweli……

the same apply kwa wanaume wakikaa vijiweni na bar wanadanganyana wake zetu hawacheat sisi ndio tumeumbwa na uwezo wa kucheat ooh! usimwambie mke wako unapata mshahara kiasi gani! akirudi nyumbani amebeba ujinga wote wa bar na vijiweni!
 
mia baba am on fight na ma wife becoz of that kaenda kujazwa maneno huko then anakuja kunishurutisha vitu nje ya uwezo wangu eti kisa flan kasema ni kizur huko saluni. Sheeeeeeeeeezy typ natan nimpige sema bac tu
 
wengine tukinyoa tutarudishwa grade one.... bora nywele zinatukomaza.
best kumbe unazo, umeweza afford lace wig?
mi bora niende local tu........
ukipiga gharama za rejareja saluni kwa miezi kadhaa tu una lace wig yako ujue
just imabine manicure na pedicure 15000 kope 25000 kuosha 4000 steaming assume the best profective sijui 12000 ukiritachi 12000 kusuka suka mara yebo 20000 mara weaving sometimes local anzia kulinunua 35000 huo ni mwenzi mmoja ;kwa mwezi hata laki inaishia saloni si bora ununue lace yako mara moja tu utulizane
 
ukipiga gharama za rejareja saluni kwa miezi kadhaa tu una lace wig yako ujue
just imabine manicure na pedicure 15000 kope 25000 kuosha 4000 steaming assume the best profective sijui 12000 ukiritachi 12000 kusuka suka mara yebo 20000 mara weaving sometimes local anzia kulinunua 35000 huo ni mwenzi mmoja ;kwa mwezi hata laki inaishia saloni si bora ununue lace yako mara moja tu utulizane
mimi huko siendi, nina kipilipili changu....
nimejifunza kusuka uzi usiku nafumua asubuhi nachana kwenda job, kama nime-blow dry...... utanitaka
kucha mwenzangu ni natural, sana sana nikitaka naweza weka hena home mara moja moja.....
kope hizo naogopa sana ku-risk macho yangu.
kama kuna vitu naogopa ni kuweka kitu machoni
 
  • Thanks
Reactions: BAK
aahhh binamu hapo umenena huo ni mfano wa kuigwa, hizi saluni siku hizi kwa asilimia kubwa zimekuwa kama magulio hasa za Sinza... bora wangekuwa wanapiga umbea tu... afadhali lakini ukijua ya nyuma ya pazia lol.... chichemi[/QUOTE
angalia usijenitusi nduguyo atiii!

aahh asilani hilo siwezi fanya hata siku moja...
 
mimi huko siendi, nina kipilipili changu....
nimejifunza kusuka uzi usiku nafumua asubuhi nachana kwenda job, kama nime-blow dry...... utanitaka
kucha mwenzangu ni natural, sana sana nikitaka naweza weka hena home mara moja moja.....
kope hizo naogopa sana ku-risk macho yangu.
kama kuna vitu naogopa ni kuweka kitu machoni
ahahaaa mambo ya uzi unywele unanyooka balaaa. kipindi nasoma bana kuna mama jirani alikuwa msusi ili akusuke anakupa mikazi yake ya home ...uoshe vyombo.udeki ..mshike mtoto nk sasa mimi nilikuwa na sister angu alikuwa anapenda kusuka kweli so yeye alikuwa anavumilia mimi nilikuwa namuomba tui maza anipige uzi asubuhi tunachana..halafu uzi unarefusha kweli kweli
 
ahahaaa mambo ya uzi unywele unanyooka balaaa. kipindi nasoma bana kuna mama jirani alikuwa msusi ili akusuke anakupa mikazi yake ya home ...uoshe vyombo.udeki ..mshike mtoto nk sasa mimi nilikuwa na sister angu alikuwa anapenda kusuka kweli so yeye alikuwa anavumilia mimi nilikuwa namuomba tui maza anipige uzi asubuhi tunachana..halafu uzi unarefusha kweli kweli
umeona eeehhhh!
ukiniona kama muhindi na unywele wangu..... nini salon banaaa
 
umeona eeehhhh!
ukiniona kama muhindi na unywele wangu..... nini salon banaaa
ngoja nikianza kusuka tena nianze kupractice zamani..mi nilinyoa si unajua nilifiwa na mother!basi nikibeba kibegi changu cha laptop ofsini watu wanauliza we dogo unaenda twisheni ama..nywele zinafanya mtu unakuwa mtu mzima jamani kunyoa sio kabisa
 
ngoja nikianza kusuka tena nianze kupractice zamani..mi nilinyoa si unajua nilifiwa na mother!basi nikibeba kibegi changu cha laptop ofsini watu wanauliza we dogo unaenda twisheni ama..nywele zinafanya mtu unakuwa mtu mzima jamani kunyoa sio kabisa
nakumbuka Smile,
pole tena.... ile namba ndo uliitupa kabisa? lol!
ingekuwa maeneo ningekutaniaje? ila sasa hapana......., ngoja niishie hapa
 
Last edited by a moderator:
mmama ndo nini!? lol!! 😛layball:

Kiukweli mimi ni mmama lakini sipendi kabisa kwenda saluni......
Najitahidi nakuwa na kila kitu changu nyumbani kwa ajili ya kuhudumia nywele zangu. naosha, steaming, nk mwenyewe. Nikitaka kusuka huwa nina mtu anakuja kunisuka nyumbani kwangu. Saluni naenda tu kama nina dharura.
 
aahhh binamu hapo umenena huo ni mfano wa kuigwa, hizi saluni siku hizi kwa asilimia kubwa zimekuwa kama magulio hasa za Sinza... bora wangekuwa wanapiga umbea tu... afadhali lakini ukijua ya nyuma ya pazia lol.... chichemi
Huko nyuma ya pazia kuna nn? maana sisi wengine tuwekewa muda wa kutoka mpk kurudi kutoka saloon, so ili nisichelewe naenda nikiwa nimeshaziosha kabisaaa, ili nisichelewe kurudi, nikaulizwa maswali mengi. Na ukichelewa kutoka kwenda imekula kwako.
 
Bora mie na kipilipili changu wala sina haja na salon.... I like my kipilipili original!!!!

natural.jpg
 
Husninyo.. ni wale toka nchi jirani kwa papaa muyoi toka pande ya mbujimai.. au hawa wa kwetu ambao wengi (kama sio wote) inasemekana ni mishumaa..?

ni hawa hawa wa kwetu yaani hata kama umeenda na umbea wako utauacha mlangoni ukitoka unaondoka nao
 
Huko nyuma ya pazia kuna nn? maana sisi wengine tuwekewa muda wa kutoka mpk kurudi kutoka saloon, so ili nisichelewe naenda nikiwa nimeshaziosha kabisaaa, ili nisichelewe kurudi, nikaulizwa maswali mengi. Na ukichelewa kutoka kwenda imekula kwako.

nyuma ya pazia kuna wanaokwenda salon wakifika tu wanatoka kwenda kwenye mambo yao wakimaliza ndio wanarudi salon mr akimpitia anamkuta pale pale anajua mke alikuwa salon kumbee.............!!!
 
Umeona hizo eyebrows... ....nani hapo Mpwapwa anaweza kunifanyia threading......nataka arch shape.......zangu ukiziona utadhani brush lililoisha.......nipo njiani nakuja huko.....
mi mwenyewe noumer katika threading, we njo vitendea kazi utavikuta huku huku. mzima wewe?
 
Back
Top Bottom