Choosen85
JF-Expert Member
- Jun 22, 2022
- 2,304
- 5,569
Alooo nimekuwa nikipata bahati kidogo ya kuwasikiliza hawa wachungaji wanawake huku makanisani ninasikitika sana kwamba wengi wao mahubiri yao yamejaa chuki, visa na visasi, uanaharakati dhidi ya mwanaume.
Wanawafundisha wenzao ni kwa namna gani mwanaume alivyo mtu mbaya sana asiyefaa.
Lakini wanawafundisha kwamba hata bila mwanaume wao wanaweza hivyo wasibabaishwe na mwanaume.
Haya mambo yapo mpk kwenye semina zao wanazoenda huko. Maswali yangu ni haya
Moja je hawa wachungaji wanawake hawa wameolewa na kama wameolewa huko kwenye ndoa zao amani ipo?
Pili ni kwanini wanafundishana kwamba mwanaume ndiye mbaya tu wao wamekamilika, je hakuna jambo jema ambalo wanaweza fundisha kuhusu ndoa na mahusiano ya mke na mume?
Wakuu hebu na ninyi toeni mitazamo yenu najua wapo ambao pia mmewahi sikia mahubiri ya hao wachungaji kama rose shaboka nk......