Wanawake na mauongo yao ya saluni haya hapa….!

Wanawake na mauongo yao ya saluni haya hapa….!

.............mie style yangu hii mimi mwenyewe ndio hairdresser wangu na napendeza vilevile.....

images
nikitaka kuweka rangi my babe sosoliso ananiweka basi inapendezaaaa
images

nakupendaje mahabuba wangu Paloma..
 
Last edited by a moderator:
Umeona hizo eyebrows... ....nani hapo Mpwapwa anaweza kunifanyia threading......nataka arch shape.......zangu ukiziona utadhani brush lililoisha.......nipo njiani nakuja huko.....


mamito..ukikgoogle unapata video clips za kiiiiiiila kitu hadi za kubandika kope!!!
 
Mbaya zaidi unakuta wanaanza kumuongelea mwanaume, na wanaweza kutoa data jinsi anavyochukua na kuhonga mademu, kumbe unakuta wakati wakisema hayo mke wa mhusika naye yupo hapo saluni, ila hawamjui...
 
ila wanopiga domo ni kina
nani?wamiliki wa saluni au
wafanyakazi?maana duuuh
umbea sinaga wala
kampani ya kike sina!
salun naenda na 50 zangu bana!

 
Mtabumbuzi umenena kweli tupu mwanawane mazungumzo mabaya huharibu tabia njema.....Mama Ngina ukiona anarudi huko katabia kamebadilika ni kusogeza kamkasi karibu unamtengeneza kama tunavyofanya kwetu umasaini.
 
hivi salon za kiume nazo kuna issue gani wanazoongelea!
 
Nyongeza ya hapo ndio wanakojulishiana mwanaume gani anamfikisha kunako wakati wa majamboz!
 
yaani heading tu imenifanya nivunjike mbavu kabla ya kusoma content.

Na umenikumbusha the last time l was at the salon na story zilizokuwa zinapigwa. LOL
halafu ujue kuna wanaume siku hizi, kuna Mr. Kucha na mchanaji wa kikongo, possibly na msusi wa kimasai!
 
kuna saluni moja nilikuwa naenda k'ndoni,mmh,visichana viongo.ila wafanyakazi wa saluni wanasema wameshayazoea.mara utasikia,nina haraha saa 10 natakiwa kupanda ndege,na wengine hujifanya kiswahili hawajui ka mmh sina nafasibisa.kuna muimbaji mmoja aliingia,mara simu ikaita.nikamsikia anasema hana nafasi amealikwa sweden,uk na marekani.wengi wao ni kujifanya wako juu
 
Mpwa Elli naona na wewe unaunga mkono mada.

Vipi kuhusu mafundi viatu(shoe shine) kuwa sehemu ya kupigia domo?
mara nyingi wale ndio wauza unga na bangi na dili zote kubwa na ndogo hufanyikia pale, nakumbuka kuna ishu fulani nilikua naitafauta kariakoo basi yule jamaa akanipeleka kwa shoe shiner mmmoja na yeye ndio akatuelekeza kwa mtu, at the end niliamua ku-drop hio dili but kila kitu kilienda swaaafi kabisa....so hawa ni watu wa dili zaidi ili watoto wale, yaani ukiskia wale madeshee wa tauni au misheni tauni ndio hao, asubuhi anaenda job kumbe anaenda kuzuga kwa fundi viatu halafu dili zote za kuuza nyumba, viwanja, magari, mali za wizi, kuchonga mihuri na vyeti bandia zote huishia hapo, take my word
 
Gharama pia zimepanda sana....... mi zimeshanishinda
najinunulia shampoo yangu, drier jua
mi nimenyoa best ..sitaki shida nikiamua kutokelezea napiga lace wigi langu ahaaa siku inaisha
 
mi nimenyoa best ..sitaki shida nikiamua kutokelezea napiga lace wigi langu ahaaa siku inaisha
wengine tukinyoa tutarudishwa grade one.... bora nywele zinatukomaza.
best kumbe unazo, umeweza afford lace wig?
mi bora niende local tu........
 
Ila kweli saluni kuna mambo. Ukiendekeza story za saluni kuna risk utabadilika uwe mtu tofauti. Utaanza kutoa maneno ya ndani mwako etc etc. Mie sipendi salon kwa kweli. Naendaga ku retouch, steaming nafanyaga mwenyewe home na kusuka pia. Kutinda nyusi naendaga Mwenge specifically kwa kazi hiyo tu. Nikitindwa kwingine matokeo yake nakuwa kama popo.
 
Back
Top Bottom