Wanawake, Mkijipodoa sana mnatutisha... Ebo!

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,806
15,379
Imebainika kwamba wanawake wanaojiremba sana usoni kwa rangi za midomo zenye kuonekana sana, na vipodozi vingine vikiwemo vile vya kope za macho, huwatisha wanaume badala ya kuwafurahisha au kuwavutia.

Katika tafiti nyingi zilizofanywa kwenye jamii mbalimbalina hasa mijini imebainika kwamba, wanaume saba kati ya kila kumi hupenda nyuso za wanawake zilizowekwa vipodozi kidogo sana. Wale wanawake ambao nyuso zao zimekolezwa vipodozi vingi badala ya kuwafurahisha au kuwavuta wanaume, huwakera na kuwatisha.

Zaidi ya wanaume 6,800 kati ya 10,000 walioshiriki kwenye tafiti hizi, walikiri kwamba, hupenda nyuso za wanawake ambazo ni safi na nyororo, ambazo hazijakandwa tope la vipodozi.
Kuna wanawake ambao hutumia mchanganyiko mkubwa sana wa vipodozi unaofikia aina 20 kwa siku. Nyuso za wanawake hawa zimeelezwa kwamba, huchusha kuliko kuvutia.

Tatizo la wanawake kujipodoa sana usoni linatokana na kutojiamini kwa wanawake hao. Wao wanadhani kujipodoa sana, kutawafanya wawavutie wanaume na hiyo itawafanya wasione udhaifu wao kwenye maeneo mengine ya mwili au tabia zao. Jambo ambalo halina ukweli.
 
Mi namshangaa zaidi mwanaume anayeweza kutoka/kuongozana na mwanamke ambaye amejisiliba kupita kiasi. Sijui inabidi mtu alewe kwanza...
 
Kukutisheni ndio lengo letu!
Kaunga umenichekesha afu utashangaa wanapanga foleni kwa wanaojipodoa sana.

nakumbuka kuna wakati nliwahiandika kuwa mambo mengi ya urembo wayafanyayo wanawake huwa yanakuwaga influenced na mitazamo ya wanaume. Mf.
Wanaume wanapopendelea viportable basi wadada watashinda wakipigana vikumbo gym kupata that portable figure.
2. Wanaume wanalipoanza kupendelea light skinned women, wadada tukaamini kuwa uzuri ni rangi, tukaikimbilia mikorogo
3. Wanaume ukipita na furushi lako ulilojaaliwa basi utasalimiwa wewe, utapigiwa miluzi wewe na salamu kede kede, wadada tukadanganyika tukawatafuta wachina walipo.....mwe!!

Kaazi kweli kweli
 
hiyo ndio confidence yao,kama wengine wanatishika,wengine bila make up hajiamini mpaka ajipodoe.muhimu kwake yeye kama anajiona amependeza inatosha.dunia ya leo utawaridhisha wangapi?
 
Uko right Mwanajamii ukiwaendekeza hawa viumbe utakuwa kichaa! Nafikiri ni muda muafaka mwanamke kufanya vitu kwa ajili yako mwenyewe (be urself), utashangaa sana ukiwa hivyo unakuwa more attractive!
Ukiwaendekeza sana hawa viumbe, nmh hawaridhiki siku zote!

Siri moja ni kwamba wanavalue sana kitu wanachokihangaikia, ukiwaplease sana they get bored easily fast! If u feel like kujipodoa, do it for urself msimamo wako is more attractive to them kuliko unatural wako! Wakigundua u do everything for them, u cease to be a challenge na watakutake for granted!

Ni mtizamo ulikuwa so much influenced by my experience!
 
Hawa unaokutana nao wanatisha sijui wa aina gani Mtambuzi.... Dah! wengine hupendeza mno, kiasi kwamba ukimkuta bila makeup utamsahau...

@AshaDii........ Siku ukisikia kuna Shajara za Ulimbwende, nakuomba uende ukaangalie jinsi Wanyange walivyojisiriba vipodozi na Lebasi mwili mzima, yaani utadhani ni waganga wa Maruhani...............
 
Kaunga umenichekesha afu utashangaa wanapanga foleni kwa wanaojipodoa sana.

nakumbuka kuna wakati nliwahiandika kuwa mambo mengi ya urembo wayafanyayo wanawake huwa yanakuwaga influenced na mitazamo ya wanaume. Mf.
Wanaume wanapopendelea viportable basi wadada watashinda wakipigana vikumbo gym kupata that portable figure.
2. Wanaume wanalipoanza kupendelea light skinned women, wadada tukaamini kuwa uzuri ni rangi, tukaikimbilia mikorogo
3. Wanaume ukipita na furushi lako ulilojaaliwa basi utasalimiwa wewe, utapigiwa miluzi wewe na salamu kede kede, wadada tukadanganyika tukawatafuta wachina walipo.....mwe!!

Kaazi kweli kweli

Nimeyampenda sana haya maneno yako:-
......Marriage is like a Dance, No matter how the Music changes you keep on Dancing... 2011
 
@AshaDii........ Siku ukisikia kuna Shajara za Ulimbwende, nakuomba uende ukaangalie jinsi Wanyange walivyojisiriba vipodozi na Lebasi mwili mzima, yaani utadhani ni waganga wa Maruhani...............


Imenibidi tu nicheke..... Khaa! Yaani Mtambuzi wewee.....
 
Hawa unaokutana nao wanatisha sijui wa aina gani Mtambuzi.... Dah! wengine hupendeza mno, kiasi kwamba ukimkuta bila makeup utamsahau...
<br />
<br />
umeona eeh! Mwanamke kujipodoa, kujiremba. Lol!
 
wale nao wana watu wao waliowapenda wakiwa vile na wakiacha wataulizwa
 
Kwa mfano alotoa... naacha kujipodoa hata kwenye mtoko....lol

@AshaDii..... Hujanielewa, nimesema kujipodoa sana ndio tatizo kwani mtu anakuwa kama kinyamkera...........Ni vyema wanawake wakajipodoa kiasi yaani kama vile una mafuta yako ya Lady Gay au Yolanda na cream yako ya Carolite. na Wanja wa Kipemba na kisha lip shine ya mafuta ya nazi halafu unamalizia na uturi wa kufukiza kwa chetezo kutoka Zanzibar au Tanga............. hivyo tu inatosha, sio kujisiriba mavipodozi mpaka unatisha.........
 
tatizo ni kutokujiamini mtu anahisi without make up hawez kudrow tension za watu na ikumbukwe kuwa kunawatu wanaishi kwa kuangalia wanaume wengi wanavutiwa na nini kujiamini ziro ni wanawake wachache wanaojikubali too bad
 
kuna vile virangi vyao wanapaka mdomoni utadhani ametoka kula nyama za watu.yaani siwezi thubutu kumsogelea anibusu.halafu nyusi wazinyoa harafu wanapaka midude ya rangi tofauti ka ma** ya kuku.mwingine unakuta mashavu mekunduu yameiva ka jipu linalokalibia kupasuka sijui wenyewe wanakuwa wamepaka nini.halafu mwenyewee ndo anaona kapendezaa.tpuuuu...!!.mia
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom