Hivi na hili tuliliongelea kule?
Wametoka mbali na mkewe, wametoka ktk zama za dhiki, wakiwa hawajui kesho yao, wametoka kwenye kununua gengeni ama dukani kwa mpemba mpaka kununua nyanya na vitunguu SHOPRITE, ...
Sawa na kununua samaki wa maboksi kutoka South Africa badala ya samaki freshi wa pale Magogoni
Jamaa anasema shemeji (shemeji kakiri kwangu kutamka kauli hizi) amemwambia kauli hizi:
- "Bora hata penzi la Mzee, (jamaa anasema Mzee ni jina la BF wa mwisho wa mkewe kabla ya yeye kumuoa)"
Lakini si anadai wametoka mbali na mkewe. Huyo ex wa mkewe kaibukia wapi tena?
2. "Mwanaume utakuwa wewe, mwanaume unapiga bao 1 tu, hoi!"
Walipokuwa wananunua nyanya na vitunguu gengeni mwanaume alikuwa anapiga zaidi ya bao moja?
Kwama amenza kupiga bao moja baada ya kuanza kununua nyanya na vitunguu SHOPRITE?
Shemeji ameifafanua kauli ya kwanza (utetezi wake), anasema alimaanisha bora aolewe na Mzee kwa maana ya Kikongwe kuliko akina sie vijana, anasema tunawapa stress sana, wazee hawana mambo mengi!
Probably, she may be right.
Wanawake: hapa huwa mnatukosea sana.
- Tumetoka wote ktk dhiki, tumeingia wote katika mafanikio, hii haitoshi kuwa hoja ya kuthibitisha Uanaume wangu?
- Tumebarikiwa watoto wawili, hii haitoshi kuwa hoja ya kuthibitisha Uanaume wangu?
- Tunasomesha watoto shule nzuri, hii haitoshi kuwa hoja ya kuthibitisha Uanaume wangu?
- Tunamiliki vigari viwili, mke anadrive, mume anadrive, hii haitoshi kuwa hoja ya kuthibitisha Uanaume wangu?
Hayo yote hayatoshi kudhibitisha uanamume wako. Kwa wanawake, uanaume siyo kuwa na mafanikio, watoto, kusomesha watoto au kumiliki magari. Of course, wako baadhi ya wanawake huwa wanaagalia hayo.
Tatizo lako unadhani kuwa wanawake wamekuwa programmed kufikiria au kutaka yale ambayo wanaume wanafikiria au kuyataka. Baadhi watakuja na kujigamba hapa, but deep inside their hearts, there is something they always want from a man.
Wanawake: hapa huwa mnatukosea sana! Hata kama kuna ukweli, bado naona shem alienda mbali sana, siri za kitandandi kuja nje, daaaah! najua shem alikuwa na hasira na huwa niko upande wake siku zote, hata jana katika usuluhishi, nilikuwa upande wa shem bila ya kuonyesha, na nilifanikiwa kumshawishi mshikaji aombe msamaha, na ikawa.
Inawezekana kuna sababu ambazo zimemfanya shemejio a-publicize siri za kitandani. Usisahau wanawake are very emotional, na zikipanda moyoni (siyo kichwani) they are very dangerous. So, bear with them.
Then, nikamsihi shemeji, pamoja na tofauti zao za kimaumbile (nikimlenga mshikaji), bado wao si wakutoleana aibu zao hadharani. Nimemsihi shemeji sifa yake kama mke mwema ni pamoja na kuvumilia ama kushirikiana na mshikaji kutatua kile kinachoonekana ni udhaifu wa mmojawapo. Nimemuomba mshikaji asijiskie vibaya kwa vile mafanikio ya mwanaume, ni kuanzisha, kuendeleza na kutunza familia yake na ndugu wanaowahusu, ni zaidi ya kitandani.
Ushauri mzuri, ila pia waongelee jinsi ya ku-improve kitandani hata kama ni kununua tena nyanya gengeni.
Kitanda! ama hata Magoli 7 kitandani, hayatalipa ada ya watoto! Hayatalipia mafuta ya gari, hayatalipia matibabu ya wanafamilia, hayatatoa msaada wa kifedha kwa wanandugu, hatajenga nyumba, hayatanunua mavazi, chakula, viatu, simu n.k!
Hii ni fikra ya kiume zaidi. Imekaa kimfumo dume. Kama wanaume wanafikiria hivyo, usidhani pia kuwa wanawake wote wanafikiria hivyo pia. Siyo wanawake wote ni wachaga kama
miss chagga. Wengine wanam-judge mwanaume kitandani kwanza, mengine ni bonus.
Kwa nini wanawake mnapenda kukimbilia siri za kitandani? Kitanda kina siri gani mpaka mfanye ni moja ya silaha yenu! Ni kweli inachoma mwanaume kuekewa aibu yake ya kitandani, lkn hili ni jambo kubwa sana ki hivo ama?
Labda wanakithamini kitanda zaidi kuliko sie wanaume? Ndo maana wao wanaotandika kitanda kila asubuhi, sie wanaume tukiamka tunatupa blanketi kule fasta town kutafuta pesa?
On the other hand, sidhani kama ni wanawake wote wanapenda kukimbilia siri za kitandani. Wanawake wana siri kubwa na kama wangeamua kuzitema pasingekalika hapa. In fact, inasemekana kuwa wanawake ndo wanajua ins and outs za mafisadi wote hapa Tanzania. Sie wanaume tuna-guess tuu, we simply know nothing unless wewe mwenyewe ni fisadi au umehusishwa kwenye ufisadi.
Nimefika ofisini, sms ya kwanza leo kwa simu yangu ni ya mshikaji, kanitumia hizo statements 2 alizopewa an mkewe jana, yaani najua jamaa yangu imemuuma sana! Na hii itamuathiri utendaji wake wa kazi leo, tayari ameniomba tukutane lunch time maeneo ya leaders club Kinondoni, kuna kitu anataka nimshauri.
Mshauri kuwa mwanamke ni tofauti na mwanaume. Kuwa mahitaji ya mwanamke ni tofauti na yale ya mwanaume. Wanawake wanapenda mafanikio, watoto, watoto wao kusomeshwa shule nzuri, kumiliki mali, n.k, lakini hivi havimtoshi kudhibitisha uanaume wa mwanaume.
Na vitu ambavyo huwa wanavitaka ni vidogo sana kiasi kwamba they don't make sense to any man. Some of those things may look silly to men lakini they mean a lot to a woman. What a woman really wants is not what a man wants.
Jaribuni kutafuta kiabu cha Men are From Mars and Women from Venus mkisome wote kinaweza kukupa theoretical hints. Pia jaribuni kuangalia filamu ya What Women Want au filamu ya Casino ya mwaka 1995 ambayo ni true story halafu mwangalieni mke wa Roberto De Nero aliyokuwa anayafanya pamoja na kuwa jamaa alikuwa na pesa yake.