Wanaume walio ndoani na "holiday ukweni"

Wanaume walio ndoani na "holiday ukweni"

Napendelea kwenda mwisho wa mwaka almost one week naenda tarehe 24. 12 had tarehe 3. January

Ila inabidi bafuni uende umevaa surual[emoji1] [emoji1] [emoji1] na usiku
How does that feel kiongozi?[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
 
Tatizo ukioa ukweni ambako wanaongea-ongea ovyo kama WAMACHAME. Wanafiki sana, wanakuchekea huku wanakung'ong'a.
Kimachame hairuhusiwi kabisa kulala ukweni hata usiku mmoja… yaani asubuhi baba mkwe kafunga taulo kiunoni na kidume umefunga taulo kiunoni?…ukifanya hii kitu unaonekana umefanya ukumbafu wa hali ya juu sana uchagani
 
Kama Dada ako kashindwa kumshawishi Shemeji yako kuja kukaa kwenu Kula sikukuu, ujue Huyo Sio Mtamu... hajamkoleza shemeji yako..
 
Nimecheka jamani,eti nawaachia nafasi na mwanae waniseme
Ni kweli, hapo lazima mama na binti wakuchambue mwanzo mwisho. Siku hizi haya mambo hata mama na mtoto wa kiume wakikaa ni kumsema mwali tu.
 
Very nice Dorrlyn. Utaratibu mzuri sana. Na wewe kwenda kuuweka kwa mama mkwe wako, hii imekaaje?

Mimi sijaweka utaratibu wowote kwa mama mkwe. Mama mkwe huwa hapendi vijana wake na wake zao walale nae in the same roof. So we mletee wajukuu nyie mtafute pa kulala. Nikienda mwenyewe Na watt ananiruhusu kulala kwake.
 
Mimi nimelala kwa mkwe na nimepiga bao kwa roof hiyo hiyo. [emoji23][emoji23][emoji23]

Angalizo: Mkwe sio mswahili.
 
sikumbuki hata kama nimewahi kulala ukweni kwa siku moja tu...
 
Kama hamna tatizo au sherehe siwezi kwenda ukweni zaidi ys siku 1 na sijawahi kulala ukweni nashangaa sana ndugu zangu waliooa migombani wanavyoenda Xmas na mwaka mpya ukweni! Kuna wanaume wanastahili viboko
[emoji23] [emoji23]
 
Happy 2018!!

Nina swali dogo lakini laweza kuwa muhimu, hasa kwa jamaa zangu wa kiumeni waliopo ndoani. Fikiria ni holiday time, wale ndugu zangu wenye desturi ya kurejea kwao/kwa wazazi wanajiandaa kwenda kufurahi na ndugu, marafiki na majirani.

Wakati huo mke anakwambia "hubby naomba likizo/sikukuu hii tuitumie kwa wazazi wangu", tuseme kuanzia tar. 20 Dec hadi tar. 7 Jan. Nawe mwanaume unakubali kwa sababu ni ukweli kuwa wazazi wa mke ni wazazi wako pia.

Swali langu hapa;
*Je utaweza kukaa kwa wakwe kuanzia 20th hadi 7th?

*Ni sahihi (kwa mtizamo wako) kukaa kwa wakwe kwa mda mrefu kama wiki na zaidi?

*Mila zetu zinasemaje kuhusu mwanaume 'kupiga kambi' ukweni?

Again, happy 2018 MMU family.
Je,ni sahh kwa mwanamke kwenda ukwen na kukaa muda mrefu?
 
holiday ni muda wa kwenda kujifunza na kuona fursa sehemu mbvali mbali sio kubweteka sehemu moja .kwetu nna nyumba yangu na huwa sikai sana unless kuna la ulazima.ukweni si pa kukaa kuliko kwenu,kwa wanaotaraji kuoa km kwenu unakaa wiki maximum ukweni inatakiwa maximu 3 days
kwa mimi ukweni siwezi kuwa na madaraka hivyo sipendi kukaa hata kwa wazaz wangu still si kwangu.hulka ya baba wa familia ni madaraka kamili.
 
Back
Top Bottom