Wanaume walio ndoani na "holiday ukweni"

Wanaume walio ndoani na "holiday ukweni"

Happy 2018!!

Nina swali dogo lakini laweza kuwa muhimu, hasa kwa jamaa zangu wa kiumeni waliopo ndoani. Fikiria ni holiday time, wale ndugu zangu wenye desturi ya kurejea kwao/kwa wazazi wanajiandaa kwenda kufurahi na ndugu, marafiki na majirani.

Wakati huo mke anakwambia "hubby naomba likizo/sikukuu hii tuitumie kwa wazazi wangu", tuseme kuanzia tar. 20 Dec hadi tar. 7 Jan. Nawe mwanaume unakubali kwa sababu ni ukweli kuwa wazazi wa mke ni wazazi wako pia.

Swali langu hapa;
*Je utaweza kukaa kwa wakwe kuanzia 20th hadi 7th?

*Ni sahihi (kwa mtizamo wako) kukaa kwa wakwe kwa mda mrefu kama wiki na zaidi?

*Mila zetu zinasemaje kuhusu mwanaume 'kupiga kambi' ukweni?

Again, happy 2018 MMU family.
Ni mtoto wetu Na hapa ni kwao. Kwa kupata Na mwanetu wamefanyika kuwa mwili mmoja
 
Siku tatu mwisho ukweni si kwa kuzoea zoea kwenda kukaa.
 
Mada fikirishi sana hii. Mimi nina miaka 16 ya ndoa na sijawahi kulala ukweni hata kwa siku moja. Sijawahi kukatazwa ila naamini sitakuwa na amani... Japo ukweni kuna chumba cha kulala wageni ... mimi huwa nalala lodge ya karibu.

Asubuhi nawahi kifungua kunywa... napiga stori kidogo then nasepa kitaa... mchana nakuja kugonga lunch na story nyingi then nasepa. Usiku nakuja kugonga dinner.... story nyingi sana then naenda zangu lodge kulala.... wife analala kwao. (Angalizo sitafuti mchepuko)

Maximum kukaa ukweni ni siku tatu kama kuna msiba wa karibu sana. Kusalimia.... nikifika leo keshokutwa mapema sana kabla jogoo hajawika mi huyoooo nshasepa zangu. Wife tutakutana mbele ya safari au jijini Daslam

Mpaka sasa sijajua kwanini....
Mkuu, lazima tuwafunze vijana mambo kama haya. Japo umesema hujawahi kufikiria hili, ila unaona mwenyewe hujawahi kulala ukweni.

Asante kwa mchango makini kiongozi. Je, mila za kwenu zinasemaje kuhusu mwanaume kuweka kambi ukweni kwa muda mrefu?
 
Ukiwazoea ukweni ipo siku watakutuma ukawanunulie pedi dukani. Hao watu nadhani ni wa kukutana nao kwenye events tu (Sherehe na Misiba). Mengine ni wewe na familia yako tu.
 
Mi ni mwanamke Niko kwa ndoa zaidi ya miaka 15 huwa tunautaratibu wa kwenda holiday Xmas kwa mama mkwe Na New year kwetu ila si Mara zote new year Mme wangu anakuja kwetu. Tukiendq nae huwa tunalala hotel iliyo karibu Na kwetu ila watoto tunawaacha kwa bibi Na babu halafu pia wale waliooa Dada zangu Na pia kaka Na mabinamu zangu ndio wakati wetu muafaka wa kukutana Na watoto wetu kujuana so Mara nyingi tunakula kwa wazazi au ndugu wengine Na pia kula bata na San Na kulala ni hotelini.
Kwa hiyo hata nyie(wewe+mume wako) hamlali kwenu. Sasa kwa nini wewe usilale kwa wazazi, au hutaki kumuacha hubby wako aende hoteli peke yake?

Mila zenu/za mume hazuruhusu yeye kulala ukweni? Nyie mnalionaje hilo la ku-spend holiday kwa wakwe?
 
Mimi nimeoa mnyiramba, ase nikienda kule nakaribishwa kama nfalime

Mama mkwe hudeki chumba mwenyewe siku ya kwanza
Ananyunyizia urashii
Mwendo wa kula kuku tu

Ila Sasa misumari kutoka kwa mashemeji na wajomba Ni shida

Mama mkwe hajawahi kuniomba pesa direct huwa anaomba kupitia wife ananiheshim sana

Wajomba na mashemeji wa kinyramba Ni pasua kichwa

Wanafika saa mbili asubuh kuja kusalimia, wananisubiria nakunywa Chai naoga afu wanasema twende tukakutenbeze
Wananpitisha kwa ndugu moja then break ya pili utasikia shem makoo yanawasha tukajipooze kwanza buana

Nawapenda sana so charming Sema vyuma vimekaza

Siku unasepa unapewa kuku, mahind, mlenda wa kukausha, nk

Ukisikia Mayo ujue upo kwa wanyiramba
 
Mimi nimeoa mnyiramba, ase nikienda kule nakaribishwa kama nfalime

Mama mkwe hudeki chumba mwenyewe siku ya kwanza
Ananyunyizia urashii
Mwendo wa kula kuku tu

Ila Sasa misumari kutoka kwa mashemeji na wajomba Ni shida

Mama mkwe hajawahi kuniomba pesa direct huwa anaomba kupitia wife ananiheshim sana

Wajomba na mashemeji wa kinyramba Ni pasua kichwa

Wanafika saa mbili asubuh kuja kusalimia, wananisubiria nakunywa Chai naoga afu wanasema twende tukakutenbeze
Wananpitisha kwa ndugu moja then break ya pili utasikia shem makoo yanawasha tukajipooze kwanza buana

Nawapenda sana so charming Sema vyuma vimekaza

Siku unasepa unapewa kuku, mahind, mlenda wa kukausha, nk

Ukisikia Mayo ujue upo kwa wanyiramba
@victor wa happy, ni mda gani huwa unakaa huko kwa wanyiramba/wakwe zako? Je, ni siku kadhaa, wiki au hata mwezi?
 
Sidhani kama kukaa ukweli kwa siku zote hzo ni jambo zuri. Ukweni ni sehemu ya kukaa siku moja mbili ya tatu unaondoka. Imagine wazazi wanapata picha gani pale unapowatakia usiku mwema? wanajua daaah!! jamaa linaenda kumuumiza binti yetu. si picha nzuri kwakweli. Tusikae sana ukweni
Naamini upo sahihi kiongozi. Je, ni mila zetu zinazuia au ni kanuni tumejiwekea?
 
Kuna kaugumu fulani hivi, sie tukienda home tunashinda kwa mama ila kulala tunaenda kwa dada, hata mi sijui kwanini.
Umeita wanaume sorry nmekuja kumuwakilisha mwanaume wangu .
Wewe ungejisikia vipi my hubby wako akipendekeza mkaspend holiday yote kwa wazazi wako, kula na kulala kwa wiki mbili?
 
Why not? Ushaasema ""holiday". Wakwe ni wazazi kwa mke wako na kwako kama wa kwako walivyo kwako na kwa mkeo. Hapo kwenye "mila zetu" fafanua maana kila kabila lina mila zake. Kwa jamii yangu ya kimachame wakioana wamachame kwa wamachame wanajua mila inasema mwanaume hawezi kulala kwa wazazi wa mwanamke na hata mwanamke hawezi kulala kwa wazazi wake hata kama kuna msiba. Kama wameoana wenyewe kwa wenyewe ina maana wana miji yao hivyo hakutatokea haja ya mwanaume kulala kwa wakwe. Lakini mila zinasemaje kuhusu kuoa chasaka au mnyika? Makabila yote duniani yangependa watoto wao wasioe au kuolewa na kabila lingine lakini kwa wengi imeshindikana. Kwa hiyo mnyaturu akioa mchaga kuna siku tu atalala ukweni. Si ajabu wala hakuna ubaya.

Naona umejichanganya mwenyewe NANDERA, huku unasema 'why not', huku unafanya reference ya kabila lako ambalo halina utaratibu wa waume zenu 'kuuweka' kwenu kwa mda mrefu.
 
Back
Top Bottom