Wanaume walio ndoani na "holiday ukweni"

Wanaume walio ndoani na "holiday ukweni"

Kwa hiyo hata nyie(wewe+mume wako) hamlali kwenu. Sasa kwa nini wewe usilale kwa wazazi, au hutaki kumuacha hubby wako aende hoteli peke yake?

Mila zenu/za mume hazuruhusu yeye kulala ukweni? Nyie mnalionaje hilo la ku-spend holiday kwa wakwe?

Mimi hata mila zetu sizijui ila huu ndio wakat pekee wa mimi Na yeye kuwa pamoja peke yetu watoto wanabaki Na bibi Na babu huko tukiamua tunaenda beach kabisa. Hivyo ndivyo tulivyozoea hata kwa wakwe zangu huwa hatulali tukifika tunasalimia mama mkwe tunakula hapo tunamwachia wajukuu sisi tunaenda kwa nyumbani yetu ambapo haiko mbali sana Na ya mama mkwe.
 
Mimi hata mila zetu sizijui ila huu ndio wakat pekee wa mimi Na yeye kuwa pamoja peke yetu watoto wanabaki Na bibi Na babu huko tukiamua tunaenda beach kabisa. Hivyo ndivyo tulivyozoea hata kwa wakwe zangu huwa hatulali tukifika tunasalimia mama mkwe tunakula hapo tunamwachia wajukuu sisi tunaenda kwa nyumbani yetu ambapo haiko mbali sana Na ya mama mkwe.
Very nice Dorrlyn. Utaratibu mzuri sana. Na wewe kwenda kuuweka kwa mama mkwe wako, hii imekaaje?
 
Mkuu, lazima tuwafunze vijana mambo kama haya. Japo umesema hujawahi kufikiria hili, ila unaona mwenyewe hujawahi kulala ukweni.

Asante kwa mchango makini kiongozi. Je, mila za kwenu zinasemaje kuhusu mwanaume kuweka kambi ukweni kwa muda mrefu?
Sijawahi kuona baba yangu akilala ukweni. Mimi pia sijawahi kulala ukweni. Sina mtoto wa kiume... ningemshauri asilale ukweni...

Hawa mabinti zangu wakiolewa afu waume zao waje walale kwangu nitawashangaa na nitawasikitikia sana mabinti zangu...

Sina sababu ya msingi ila sioni kama ni sahihi kufunga taulo kwenda kuoga ukweni... sembuse kulala...?
 
Ulivyofunga ndoa iliambiwaje kuhusu wazazi wa pande zote mbili. Hakuna tatizo unaweza mwaka huu ukaenda ukweni na mwaka mwingine kwenu. Hizo ni familia moja. Kumbuka watoto wanatakiwa kuwaona babu na bibi wote. Ila sio lazima we na mkeo ama mumeo kulala kwenye mji wa wazazi mnaweza kulala hotelini lakini watoto ni muhimu kuzoea mazingira ya asili ya wazazi.
 
Sijawahi kuona baba yangu akilala ukweni. Mimi pia sijawahi kulala ukweni. Sina mtoto wa kiume... ningemshauri asilale ukweni...

Hawa mabinti zangu wakiolewa afu waume zao waje walale kwangu nitawashangaa na nitawasikitikia sana mabinti zangu...

Sina sababu ya msingi ila sioni kama ni sahihi kufunga taulo kwenda kuoga ukweni... sembuse kulala...?
Wapo vijana wana mahusiano na wakwe zao (achilia mbali kulala ukweni). Tena mechi inapigwa hapo hapo ukweni hilo unalizungumziaje?
 
Mimi nimeoa mnyiramba, ase nikienda kule nakaribishwa kama nfalime

Mama mkwe hudeki chumba mwenyewe siku ya kwanza
Ananyunyizia urashii
Mwendo wa kula kuku tu

Ila Sasa misumari kutoka kwa mashemeji na wajomba Ni shida

Mama mkwe hajawahi kuniomba pesa direct huwa anaomba kupitia wife ananiheshim sana

Wajomba na mashemeji wa kinyramba Ni pasua kichwa

Wanafika saa mbili asubuh kuja kusalimia, wananisubiria nakunywa Chai naoga afu wanasema twende tukakutenbeze
Wananpitisha kwa ndugu moja then break ya pili utasikia shem makoo yanawasha tukajipooze kwanza buana

Nawapenda sana so charming Sema vyuma vimekaza

Siku unasepa unapewa kuku, mahind, mlenda wa kukausha, nk

Ukisikia Mayo ujue upo kwa wanyiramba
[emoji23][emoji23]mimi home nikienda cwezi kukaa zaidi ya cku tatu ni gharama wageni wanakuja kuanzia asubuhi kusalimia (hapo akitaka kuondoka atakuaga kila saa mpk umwache na chochote)bado ndugu hao hua wanaomba kabisa hela[emoji23][emoji23]
 
Sidhani kama kukaa ukweli kwa siku zote hzo ni jambo zuri. Ukweni ni sehemu ya kukaa siku moja mbili ya tatu unaondoka. Imagine wazazi wanapata picha gani pale unapowatakia usiku mwema? wanajua daaah!! jamaa linaenda kumuumiza binti yetu. si picha nzuri kwakweli. Tusikae sana ukweni
[emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1]
 
Me ukweni nadamkia komboraa nikijitahid saaanaaa nmekaa mpakaa kumi na moja jion nmegeuzaa malapaa japo sio mbali 150 km kwenda tuu

Wife akisema anabaki kwao hatakiwi kuzidisha siku 3 sijawahi kufikiria kulala ukwenii hataa kwa pesaa
 
Muda wote huo unafanya nn mwanaume??Salimia nenda kwenu mwache mke hapo..awe huru...afurahi maisha na ndugu zake...
 
Naamini upo sahihi kiongozi. Je, ni mila zetu zinazuia au ni kanuni tumejiwekea?
Nafikir kuna vitu vinakuja moja kwa moja tu...hivi mm niende kwetu na mke wangu then na dada angu nae aje na shemeji yangu..then huyu shemeji akae sijui siku saba....nikijua tu wanakaa muda wote huo..natengeneza safari...namuacha wife....haha
 
Ulivyofunga ndoa iliambiwaje kuhusu wazazi wa pande zote mbili. Hakuna tatizo unaweza mwaka huu ukaenda ukweni na mwaka mwingine kwenu. Hizo ni familia moja. Kumbuka watoto wanatakiwa kuwaona babu na bibi wote. Ila sio lazima we na mkeo ama mumeo kulala kwenye mji wa wazazi mnaweza kulala hotelini lakini watoto ni muhimu kuzoea mazingira ya asili ya wazazi.
Mkuu, hoja yangu sio kwa wajukuu kwenda kukaa na babu na bibi, nisome tena.
 
Sijawahi kuona baba yangu akilala ukweni. Mimi pia sijawahi kulala ukweni. Sina mtoto wa kiume... ningemshauri asilale ukweni...

Hawa mabinti zangu wakiolewa afu waume zao waje walale kwangu nitawashangaa na nitawasikitikia sana mabinti zangu...

Sina sababu ya msingi ila sioni kama ni sahihi kufunga taulo kwenda kuoga ukweni... sembuse kulala...?
[emoji122][emoji106][emoji122]
 
Back
Top Bottom