Kutongoza hakuna njia maalumu eti lazima ufanye hivi ndiyo itaitwa unajua kutongoza, kila mtu ana mbinu yake cha muhimu anaetongozwa, ajue kinachoeendelea mwanamme anataka nini. Wapo waliotongoza kwa kuwapokea tu mzigo wa kuni mpenzi/ mke mtarajiwa, leo ni wapenzi au wameoana kabisa. Mimi enzi hizo nilikua mpiga picha siku moja nikawapiga picha akina Dada waliokua wamekaa kikundi, nikijua picha zikitoka sitokosa wakuipenda na akailipia. Siku nimepeleka ile picha nikaitwa na kijana mmoja pale, akaniambia kuna Dada yuko hivi siku ilivowapiga picha alikupenda sana uchangamvu wako amenituma nikuambie. Siku hawajakuambia uwapige picha ukawapiga anataka akupe penzi. Sasa hebu ona kumbe nilimtongoza kwa uchangumvu tu, nina mifano mingi sana jinsi watu walifowapata wapenzi wao ambao wengine hivi sasa ni wanandoa ila haitoshi kuandika hapa.