WANAUME: Nimewainulia mikono!!

WANAUME: Nimewainulia mikono!!

Okay, now let me say this,

Kawaida kwa mazingira ya kiafrika hasa, kuolewa kwa mwanamke ni prestige na heshima kwake mwenyewe na kwa familia yake (Mama hufurahi zaidi binti yake anapoolewa nadhani hata kumzidi baba) Hii inatokana hasa na mazingira tunayoishi ambayo msichana asiyeolewa mpaka kufikia umri wa miaka 30 na kuendelea huonekana ana kasoro fulani au kuchukuliwa kama mtovu wa heshima (nachelea kutumia neno malaya)

Sasa, hali hii imewafanya wanawake wengi kuwa na destiny ya kuwa wake za watu kwenye akili zao (Ingawa notion hii imeanza kubadilishwa na baadhi ya wasichana wa kisasa ambao either huamua kuishi maisha yao au kuamua kuwa na watoto tu bila kuolewa. Hata hivyo pia perception ya jamii kwa kiasi kikubwa humchukulia kama malaya au mtovu wa heshima.

Kwa sababu hizo hapo juu na zile za kutaka kufanya harusi kama ya fulani, hupelekea wengi wao kutaka kufunga ndoa na kuwa tayari kumuachia mtu yoyote ambaye atakuwa tayari kuwaoa. Wakati mwingine bila kuangalia mambo mengine tangulizi kabla ya ndoa ambayo huenda yanapelekea wapenzi wao wa muda mrefu (kwa kesi ya huyo rafiki yako) kuchelewa au kuonekana kama hawana mpango wa kufikia hatua ya ndoa.

Sasa labda niongelee kidogo for the case of vijana wa kiume wa siku hizi. Wengi wao wana hofu ya kuingia kwenye ndoa kwasababu wanaangalia zaidi vitu vifuatavyo;
  1. Uwezo wa kuwa na mke hasa kumuhudumia (Hapa mara nyingi wanaangalia kama wasipoweza kuwapa kila wake zao wanachokihitaji je hawatawasaliti na wanaume wengine?)
  2. Namna gani wataweza kufanya harusi kubwa kama ya fulani ili wasiingie aibu ya harusi yao kuwa ya kawaida bila kuangalia hasa maana ya ndoa na essence ya sherehe kwenye ndoa.
  3. Kutoaminiana (Hii ina apply kwa pande zote mbili) hasa kwa siku hizi ambapo uaminifu umekwisha kabisa kwa pande zote mbili.
  4. Mahari, this is an issue ingawa pia nyingine ni woga tu kwa hadithi wanazosikia vijiweni.
Sasa ukiangalia hizi utagundua kwamba kuna pande mbili zenye a very different move, wakati mwanamke anataka kuingia kwenye ndoa mwanaume yeye hasa mwenye nia ya dhati anakuwa anaogopa kuingia kwenye ndoa kwa kuangalia sababu hasa nilizozitaja hapo juu. Na ndipo hapo unakutana na majitu yanayotumia weakness ya wanawake kama huyo rafiki yako kutimiza azma yao.

charminglady, tafuta novel moja inaitwa Nothing Lasts Forever ya Sydney Sheldon ina story fulani kama inaendana na hiyo ya rafiki yako.

Nipo mkuu angalau hata nisipocomment huwa nasoma na kutabasamu mwenyewe pale ninapokuwa nimebanwa na majukumu.

nashukuru kwa mchango wako mkuu... Nitajitahidi kusaka hiyo novel!!!! :clap_2:
 
besti nimependa sana hadithi yako imenipa fundisho na somo pia hasa sisi wadada tuwe amakini na hawa makaka uchwara jamani ila hujamalizia unataka kuwa kama akina Mtambuzi wasiomalizia mada zao
 
Last edited by a moderator:
Hope weekend ilikuwa poaaaaaa........!

Kuna dada mmoja alikuwa anafanya kazi ofisi moja ya Serikali Mkoani Mtwara ila ni mwenyeji wa Mwanza, (Majina, kabila na mahali sio halisi tafadhali) Huyo dada alikuwa mrembo kweli, basi akapata boyfriend wa Kimakonde hapo Mtwara (Tumuite Maneno) Wakapenda hakuna mfano, yaan ukienda ofisini hapo hutochukua muda kusikia habari za mapenzi yake na huyo Boyfee wake, kila mtu alikuwa anatamani kuwa na mahusiano kama ya yule dada.....

Basi kaka mmoja mwenye pesa zake (Tumuite Aman) akawa anamtaka yule dada (Tumuite Tumain) Tumain alimpa za uso, "Ooh mie nina mchumbaangu, tunapendana saaaana na tutaoana siku si nyingi" Aman hakukata tamaa, kila apatapo nafasi ya kuonana na Tumain alikuwa akimkumbusha ombi lake. Kumbuka Maneno hakuwa na pesa kama Aman..... Miaka ikasonga hakuna dalili ya ndoa kati ya Mrembo Tumain na Kaka Maneno, Hatimaye akawa anakumbuka kuwa kuna mkaka anamsumbua sumbua huenda akawa ana lengo la kumuoa.....

Mrembo Tumain akatafuta ni jinsi gani atampata Aman bila Aman kumstukia, kama bahati vile wakati anafikiria Aman naye akawa anarudi kujaribu bahati yake, Ndipo Mrembo Tumain akajaribu kufungua moyo ya kumsikiza Aman..... Aman akaanza na gia ya Ndoa, dah kumbe hapooooo ndipo alipokuwa anapatamani Mrembo Tumain........

Basi Mrembo Tumain akamwambia Aman iwapo wataka kunioa hakuna kufanya mapenzi mpaka siku ya Ndoa... Aman alikubali bila kinyongo akijua kuna mahali ambapo atamkamatia tu..... KIMSINGI AMAN HAKUWA NA NIA YA KUMUOA MREMBO TUMAIN BALI ALITAKA KUMKOMOA KWA KUFANYA NAYE MAPENZI TU KISHA KUMUACHA KWANI ALIKUWA AMARINGIA SAAAANA......

Basi bana, Mrembo Tumain akavunja uhusiano na Boyfee wake wa siku nyingi ambaye walikuwa wakipendana saaaana! Mara akaanza mahusiano na Aman kwa lengo la kutofanya mapenzi kabla ya ndoa. Haya haya ndoaaaaaaa hiyooooo yabisha hodi. Aman akamwambia jiandae twende nikajitambulishe kwenu Mwanza. Tumain akachukua likizo kwa ajili ya kwenda kumtambulisha Aman....

Mrembo Tumain huyoooo akawasiliana na familia yake huko Mwanza kwa ajili ya kwenda kumtambulisha Aman.. Siku ikawadia safari ikaanza Mrembo Tumain na Aman haoooo wakaanza safari kupitia Dar es salaam... Kufika Dar wakachukua chumba, wakalala. Aman akamwambia Tuma mie ndie mumeo mtarajiwa na sasa tunakwenda kwenu kwa ajili ya utambulisho je bado huna imani nami?? Tuma kuambiwa hivyo akaona ni kweli... Wakafanya mapenzi, siku ya kwanza hiyo ikapita, siku ya pili hiyo ikapita na siku ya tatu ndipo wakaanza safari toka DSM kwenda Mwanza. Hapo familia ya Tumain inangoja ugeni wa Mkwe, Basi kufika Shinyanga ile wameteremka kuchimba dawa ndipo mambo yalipoharibika............

Aman na baadhi ya waliteremka kuchimba dawa na kumuacha Tumain ndani ya gari, baada ya muda watu wote walirudi ndani ya gari lakini Aman hakurudi mpaka gari liakaanza kuondoka. Tuma akaingiwa na wasiwasi akaanza kumpigia Aman simu "mbona hurudi na gari linaanza kuondoka??" Aman akamjibu nimepata dharura ila tangulia nakuja na gari litakalo fuata. basi Tuma akaruhusu gari kuondoka... haoooooooo mpaka Mwanza, kufika akakuta nduguze wanamsubiri stand ya Bus. wakamuuliza mbona ulisema unakuja na mgeni yu-wapi???? Tuma akawaambia "kapata dharura ila atakuja na mabasi yanayofatia" Tuma akafika kwao wakiwa na Matumani kuwa mgeni kapata dharua na akishindwa kufika siku hiyo anaweza akafika siku inayofuata asubuhi....

Kesho yake Tuma akampigia simu Aman... Kwani simu inapatikanaaaaaa...... Holaaaaa... piga piga na wewe simu haipatikani, basi Tuma akapiga kwa rafikize Aman, kuwauliza kama wana taarifa zozote, kumbe Aman aliwaeleza mchezo mzima na hao rafikize wakamwambia A-Z.... Tuma alilia sana na kujuta kumuacha mchumba wake kisa kukimbilia Ndoa hewa............. Mwisho wa siku akamaliza likizo akarudi kazini kwa aibu na fedheha sana kwani Aman alitangaza njia aliyotumia kumpata Tuma kiulainiiii tena siku tatu wanabanjuka tu bila tatizo!!!!!!!!

Mpaka wa leo Tumain hajaolewa ni zaidi ya miaka mitano imepita, hakuna hata mtu wa kumtania kuwa anataka ndoa. Boyfee wake wa zamani keshaoa na watoto juu!!!!!!!!!

SAMAHANI KWA KUWACHOSHA WAPENDWA.... HILI LIWE FUNDISHO KWA AKINA DADA.

ILA NA KWA WANAUME JAMANI MSIWE KAMA AMAN LOL!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Hili siyo fundisho kwa mtu yeyote isipokuwa ni ujinga, hata wewe uliyeleta thread hii kwa kudhani kuwa kuna fundisho hapa, wewe pia ni mjinga sana!
 
Hili siyo fundisho kwa mtu yeyote isipokuwa ni ujinga, hata wewe uliyeleta thread hii kwa kudhani kuwa kuna fundisho hapa, wewe pia ni mjinga sana!

Ni kweli mkuu, nakubali ila ipo siku ujinga utanitoka. Nashukuru kwa kuwa sio --------!
 
Bora ushukuru best kwani wengine hawajaelewa kwanini umetoa post hiyo
kwangu imenigusa sana tena sana na nimeifurahia toa post ingine zaidi ya hiyo
ni kweli mkuu, nakubali ila ipo siku ujinga utanitoka. Nashukuru kwa kuwa sio --------!
 
Bora ushukuru best kwani wengine hawajaelewa kwanini umetoa post hiyo
kwangu imenigusa sana tena sana na nimeifurahia toa post ingine zaidi ya hiyo

Usijali mamie... Nilifundwa nikafundika!
 
Back
Top Bottom