Dr. Mariposa
JF-Expert Member
- Dec 2, 2014
- 4,636
- 15,247
Najua haiwahusu ila nimeanza ufugaji wa kuku wa kienyeji sasa basi nina majike wanne na jogoo moja, nimeshtushwa sana jinsi jogoo anavyowajali wake zake,
Kwanza, jogoo hali mpaka majike wale, anawaitia chakula yeye anasimama pembeni,
Pili, anawapeleka sehemu ya kutagia yaani anatengeneza sehemu ya jike wake kua comfy wakitaga hadi kulalia,
Tatu, anaishi nao wote kwa upendo mkubwa, hawabagui, hawapigi
Nne, anawalinda dhidi ya maadui ukimsogolea jike wake anatishia kukurukia, na kwa watoto wakiwa wanawafukuza majike wake hata awe mbali vipi atakuja mbio na kutaka kupigana,
Sasa kilichonifanya nilete huu uzi ni baada ya kuona Jogoo anawashinda akili, maarifa na mapenzi wanaume wengi kwa wake zao,
Imagine janaume zima limejaza misuli kwenye mikono yake linampiga mwanamke kama linakanda maandazi,
Janaume zima linakataa kumpeleka mwanamke wake clinic wakati mimba waliitafuta wote, janaume zima lipo radhi kwenda kula mapocho pocho peke yake au na michepuko yake huku mke na watoto wanashindia andazi moja moja, yaani wanaume wa kitanzania wengi wenu mna ubinafsi sana, mwanamke aliyekutoa kwenye ukoko enzi hizo unavaa kandambili ukishazipata unaanza kumuona mluga luga hana hadhi hata ya kuongozana na wewe, mwanamke wako amekuzalia watoto wazuri, ameharibu shape yake mwisho wa siku unamuona mzee, kiroba ananuka maziwa, shame!
Kuna siku tumeenda clinic ya mtoto, akaja mwanamke mjamzito ameongozana na mwanaume wake basi lile janaume eti linajishtukia kuonekana kama yupo nae, muda wote kainama kwenye simu huku anatupiga kijicho cha pembeni, mwanamke wa watu anamsemesha jamaa hamjibu na akijibu anajibu kama anakereka, ikafika muda wakaitwa waingie kwa nurse khe jamaa asigome nini yule dada akamwambia kwa sauti ya chini lakini wakuda tukainasa, "baba T mbona unanitia aibu lakini sio vizuri" basi likageuka tena kutuangalia akatukuta tumemkodolea macho kama yote likamwambia "tangulia si nakuja bhana" baadae kwa kujivuta vuta sana likaingia, alivyoona warembo tumekaa tumetulia akaona mkewe anamchoresha duh! na limgongo lake lililopinda kama chura mzee, mxiiiiiiiiue
Kuna hawa wasiosaidia wake zao mizigo yaan unakuta wametoka shopping janaume lipo busy linachat mwanamke kaelemewa na mizigo, hua wananikera sana wakati mwingine huwaomba wawasaidie wakati mwingine naishia kusonya tu,
Haya nyie wanaume suruali ujumbe wenu ndio huo mjirekebishe, heshimuni wake zenu, wapendeni, wajalini, walindeni kama Jogoo anavyofanya kwa mke wake, mnaweza kufuga kuku pia ili mjifunze kwa jogoo 🤣🤣🤣
Tchaao.
Kwanza, jogoo hali mpaka majike wale, anawaitia chakula yeye anasimama pembeni,
Pili, anawapeleka sehemu ya kutagia yaani anatengeneza sehemu ya jike wake kua comfy wakitaga hadi kulalia,
Tatu, anaishi nao wote kwa upendo mkubwa, hawabagui, hawapigi
Nne, anawalinda dhidi ya maadui ukimsogolea jike wake anatishia kukurukia, na kwa watoto wakiwa wanawafukuza majike wake hata awe mbali vipi atakuja mbio na kutaka kupigana,
Sasa kilichonifanya nilete huu uzi ni baada ya kuona Jogoo anawashinda akili, maarifa na mapenzi wanaume wengi kwa wake zao,
Imagine janaume zima limejaza misuli kwenye mikono yake linampiga mwanamke kama linakanda maandazi,
Janaume zima linakataa kumpeleka mwanamke wake clinic wakati mimba waliitafuta wote, janaume zima lipo radhi kwenda kula mapocho pocho peke yake au na michepuko yake huku mke na watoto wanashindia andazi moja moja, yaani wanaume wa kitanzania wengi wenu mna ubinafsi sana, mwanamke aliyekutoa kwenye ukoko enzi hizo unavaa kandambili ukishazipata unaanza kumuona mluga luga hana hadhi hata ya kuongozana na wewe, mwanamke wako amekuzalia watoto wazuri, ameharibu shape yake mwisho wa siku unamuona mzee, kiroba ananuka maziwa, shame!
Kuna siku tumeenda clinic ya mtoto, akaja mwanamke mjamzito ameongozana na mwanaume wake basi lile janaume eti linajishtukia kuonekana kama yupo nae, muda wote kainama kwenye simu huku anatupiga kijicho cha pembeni, mwanamke wa watu anamsemesha jamaa hamjibu na akijibu anajibu kama anakereka, ikafika muda wakaitwa waingie kwa nurse khe jamaa asigome nini yule dada akamwambia kwa sauti ya chini lakini wakuda tukainasa, "baba T mbona unanitia aibu lakini sio vizuri" basi likageuka tena kutuangalia akatukuta tumemkodolea macho kama yote likamwambia "tangulia si nakuja bhana" baadae kwa kujivuta vuta sana likaingia, alivyoona warembo tumekaa tumetulia akaona mkewe anamchoresha duh! na limgongo lake lililopinda kama chura mzee, mxiiiiiiiiue
Kuna hawa wasiosaidia wake zao mizigo yaan unakuta wametoka shopping janaume lipo busy linachat mwanamke kaelemewa na mizigo, hua wananikera sana wakati mwingine huwaomba wawasaidie wakati mwingine naishia kusonya tu,
Haya nyie wanaume suruali ujumbe wenu ndio huo mjirekebishe, heshimuni wake zenu, wapendeni, wajalini, walindeni kama Jogoo anavyofanya kwa mke wake, mnaweza kufuga kuku pia ili mjifunze kwa jogoo 🤣🤣🤣
Tchaao.