Wanaume mmepitwa mapenzi na mahaba na Jogoo

Wanaume mmepitwa mapenzi na mahaba na Jogoo

Najua haiwahusu ila nimeanza ufugaji wa kuku wa kienyeji sasa basi nina majike wanne na jogoo moja, nimeshtushwa sana jinsi jogoo anavyowajali wake zake,
Kwanza, jogoo hali mpaka majike wale, anawaitia chakula yeye anasimama pembeni,
Pili, anawapeleka sehemu ya kutagia yaani anatengeneza sehemu ya jike wake kua comfy wakitaga hadi kulalia,
Tatu, anaishi nao wote kwa upendo mkubwa, hawabagui, hawapigi
Nne, anawalinda dhidi ya maadui ukimsogolea jike wake anatishia kukurukia, na kwa watoto wakiwa wanawafukuza majike wake hata awe mbali vipi atakuja mbio na kutaka kupigana,

Sasa kilichonifanya nilete huu uzi ni baada ya kuona Jogoo anawashinda akili, maarifa na mapenzi wanaume wengi kwa wake zao,
Imagine janaume zima limejaza misuli kwenye mikono yake linampiga mwanamke kama linakanda maandazi,
Janaume zima linakataa kumpeleka mwanamke wake clinic wakati mimba waliitafuta wote, janaume zima lipo radhi kwenda kula mapocho pocho peke yake au na michepuko yake huku mke na watoto wanashindia andazi moja moja, yaani wanaume wa kitanzania wengi wenu mna ubinafsi sana, mwanamke aliyekutoa kwenye ukoko enzi hizo unavaa kandambili ukishazipata unaanza kumuona mluga luga hana hadhi hata ya kuongozana na wewe, mwanamke wako amekuzalia watoto wazuri, ameharibu shape yake mwisho wa siku unamuona mzee, kiroba ananuka maziwa, shame!

Kuna siku tumeenda clinic ya mtoto, akaja mwanamke mjamzito ameongozana na mwanaume wake basi lile janaume eti linajishtukia kuonekana kama yupo nae, muda wote kainama kwenye simu huku anatupiga kijicho cha pembeni, mwanamke wa watu anamsemesha jamaa hamjibu na akijibu anajibu kama anakereka, ikafika muda wakaitwa waingie kwa nurse khe jamaa asigome nini yule dada akamwambia kwa sauti ya chini lakini wakuda tukainasa, "baba T mbona unanitia aibu lakini sio vizuri" basi likageuka tena kutuangalia akatukuta tumemkodolea macho kama yote likamwambia "tangulia si nakuja bhana" baadae kwa kujivuta vuta sana likaingia, alivyoona warembo tumekaa tumetulia akaona mkewe anamchoresha duh! na limgongo lake lililopinda kama chura mzee, mxiiiiiiiiue

Kuna hawa wasiosaidia wake zao mizigo yaan unakuta wametoka shopping janaume lipo busy linachat mwanamke kaelemewa na mizigo, hua wananikera sana wakati mwingine huwaomba wawasaidie wakati mwingine naishia kusonya tu,

Haya nyie wanaume suruali ujumbe wenu ndio huo mjirekebishe, heshimuni wake zenu, wapendeni, wajalini, walindeni kama Jogoo anavyofanya kwa mke wake, mnaweza kufuga kuku pia ili mjifunze kwa jogoo 🤣🤣🤣

Tchaao.
Kama jogoo unamuona anatuzidi, si uende akuwowe yaishe? Hata. hivyo, namshukuru mheshimiwa rais daktari profesa SSH mwanamke mwenzio ambaye siku zote ameonyesha hili kwa kutoandamana na nonihino wake.
 
ahsante mkakaflani
533932bda74e516d805aa7ba41c1a6af.jpg
 
Jogoo hamuachi jike wake hata iweje, umeona sasa hadi jogoo anajua ili kumpata mwanamke sharti utoe chochote kitu ila nyie mkiombwa buku tu mnafungulia nyuzi mia mbili kwa saa
😂😂😂Utasikia wakuu za sahizi
Huyu demu nilimuomba namba nikamtongoza baada ya siku mbil akaniomba buku hivi huyu anafaa kweli😂😂😂😂
 
Najua haiwahusu ila nimeanza ufugaji wa kuku wa kienyeji sasa basi nina majike wanne na jogoo moja, nimeshtushwa sana jinsi jogoo anavyowajali wake zake,
Kwanza, jogoo hali mpaka majike wale, anawaitia chakula yeye anasimama pembeni,
Pili, anawapeleka sehemu ya kutagia yaani anatengeneza sehemu ya jike wake kua comfy wakitaga hadi kulalia,
Tatu, anaishi nao wote kwa upendo mkubwa, hawabagui, hawapigi
Nne, anawalinda dhidi ya maadui ukimsogolea jike wake anatishia kukurukia, na kwa watoto wakiwa wanawafukuza majike wake hata awe mbali vipi atakuja mbio na kutaka kupigana,

Sasa kilichonifanya nilete huu uzi ni baada ya kuona Jogoo anawashinda akili, maarifa na mapenzi wanaume wengi kwa wake zao,
Imagine janaume zima limejaza misuli kwenye mikono yake linampiga mwanamke kama linakanda maandazi,
Janaume zima linakataa kumpeleka mwanamke wake clinic wakati mimba waliitafuta wote, janaume zima lipo radhi kwenda kula mapocho pocho peke yake au na michepuko yake huku mke na watoto wanashindia andazi moja moja, yaani wanaume wa kitanzania wengi wenu mna ubinafsi sana, mwanamke aliyekutoa kwenye ukoko enzi hizo unavaa kandambili ukishazipata unaanza kumuona mluga luga hana hadhi hata ya kuongozana na wewe, mwanamke wako amekuzalia watoto wazuri, ameharibu shape yake mwisho wa siku unamuona mzee, kiroba ananuka maziwa, shame!

Kuna siku tumeenda clinic ya mtoto, akaja mwanamke mjamzito ameongozana na mwanaume wake basi lile janaume eti linajishtukia kuonekana kama yupo nae, muda wote kainama kwenye simu huku anatupiga kijicho cha pembeni, mwanamke wa watu anamsemesha jamaa hamjibu na akijibu anajibu kama anakereka, ikafika muda wakaitwa waingie kwa nurse khe jamaa asigome nini yule dada akamwambia kwa sauti ya chini lakini wakuda tukainasa, "baba T mbona unanitia aibu lakini sio vizuri" basi likageuka tena kutuangalia akatukuta tumemkodolea macho kama yote likamwambia "tangulia si nakuja bhana" baadae kwa kujivuta vuta sana likaingia, alivyoona warembo tumekaa tumetulia akaona mkewe anamchoresha duh! na limgongo lake lililopinda kama chura mzee, mxiiiiiiiiue

Kuna hawa wasiosaidia wake zao mizigo yaan unakuta wametoka shopping janaume lipo busy linachat mwanamke kaelemewa na mizigo, hua wananikera sana wakati mwingine huwaomba wawasaidie wakati mwingine naishia kusonya tu,

Haya nyie wanaume suruali ujumbe wenu ndio huo mjirekebishe, heshimuni wake zenu, wapendeni, wajalini, walindeni kama Jogoo anavyofanya kwa mke wake, mnaweza kufuga kuku pia ili mjifunze kwa jogoo 🤣🤣🤣

Tchaao.
Mbona sisi tunafanya zaidi ya haya sema tu nyie hamuyaoni na kingine zaidi, tunachinja huyo huyo jogoo kuwalisha kipindi mkiwa wajawazito. Tunawafanyia vituko pale tunapotambua kuwa mimba si zetu ila jogoo ana uhakika kuwa mimba ni yake maana hana kazi ya kufanya zaidi ya kushinda na wake zake na kuwadanganya kwa kuwaitia chakula ambacho mara nyingi kunakuwa hakuna anawadanganya tu ili awapande. Sisi hatufanyi hivyo, tunawaletea pizza na vyakula mvitakavyo. Je, unataka kunifuga nikupe mapenzi ya uhakika?
 
Una majike manne na jogoo mmoja [ ndoa za mitala hizo}
Point zote 1-4 jogoo anaweza kuyafanya hayo kwa kuwa kuku jike HAMDHARAU , HAMTUKANI WALA HAMNYIMI UTAMU KOLEA.
funzo: Hata binadamu wa kike wangekuwa watulivu na wakarimu tena wenye heshima kama madike ya kuku ni ukweli usiopingika kwamba kumbi zote za starehe zingefungwa.
 
😂😂😂Utasikia wakuu za sahizi
Huyu demu nilimuomba namba nikamtongoza baada ya siku mbil akaniomba buku hivi huyu anafaa kweli😂😂😂😂
Hiyo "wakuu za sahizi" imenivunja mbavu,
Yaani umepita mule mule😂🤣
Hapo watajaa kumwaga nyongo zao za kuombwa buku buku yaan watatapika haswaaa
 
Hiyo "wakuu za sahizi" imenivunja mbavu,
Yaani umepita mule mule😂🤣
Hapo watajaa kumwaga nyongo zao za kuombwa buku buku yaan watatapika haswaaa
😂😂😂Ndo zao "wakuu hii imeekaje"nipige chini 😃 et kisa kaombwa buku
 
sio wababa wote wako hivyo, mie wanangu nlikuwa nawapeleka clinic nikifika pale hata kama nimechelewa napewa kipaumbele chap hata dk 10 haziishi nishasepa,, wale manesi walinizoea kabisa,, siku akienda wife anakula msoto wa foleni.
 
Back
Top Bottom