Wanaume kwanini mna tabia mbaya?

Wanaume kwanini mna tabia mbaya?

Sababu kubwa hapa ni mwanamke mwenyewe...unakuta wewe unaamka saa 11 alfajiri lakini mkeo anaamka saa mbili sasa unadhani kitatokea nini zaidi ya kuoga kunyoosaha nguo nakusepa?
Wanawake lazima mtambue kuwa haya ni manyanyaso makubwa sana kwa waume zenu.
 
Kuna mmoja alichemsha samaki na magamba yake
Haaa haa huyo kwao hakuna samaki kazoea kununua wale wa barabarani huyo mzima hamjui kumtengeneza, mf.watu wengi wananunua kuku za vipande hawajui kumtengeneza kuku mzima sasa mpelekee kuku mzima au nazi kama hajalitumbukiza lote kwenye sufuria la mchele

Sent from my SM-T800 using JamiiForums mobile app
 
Yaan mi naona live sio kusimuliwa unakuta familia wana uwezo lakin chakula hakifanani na hiyo nyumba,,,wanakula hovyo hovyo tu ,,, yaan watoto kula pilau mpaka sikukuu na sikukuu
Mimi hiyo family ya bi mkubwa nilikuwa na urafiki na binti wa huyo baba siku nimeenda kwa mdogo Mungu wangu nilichoka.

Sent from my SM-T800 using JamiiForums mobile app
 
Inakuwaje unaacha kunywa chai kwako unaenda kunywa chai hotelini ,unakunywa chai ya maziwa kwanini usinunue kwako maziwa mkeo akapika mkanywa na wanao,,,hujisikii vibaya wala kujishtukia au kujishuku?
Sio jambo jema kabisa,na sio haki yaan wanawake hebu kuweni wakali kabisa waume zenu muwabane wawe wanakunywa chai home kama ni ya rangi mnywe wote,,,halaf muwadai pesa za matumizi waongeze wenzenu wanatanua huko bar bill kubwa laki au zaidi we unakunywa chai ya rangi mnywe chai ya rangi kwa kupenda n mle vizuri

Wanaume na nyie acheni ubahili kama mnavyoonyesha ubavu na ujeuri wa pesa bar,tunawaomba na majumbani mwenu muanze hiyo jeuri muache matumizi ya kutosha watoto wale vizurii, sio watoto kula vizuri mpaka matumbo yanapata mshituko maana hayajazoea kula vyema
Pendeni familia zenu basi ,,wanasema family first
mkiwa bar utasema nyumbani pako vyema ,ukienda nyumbani hovyoo hovyo watoto wanakula kwa kulamba lamba tu hawashibi sio vizuri kabisa
Nadhani nimeeleweka na mjirekebishe mle hotelin kwa sababu maalumu alaa
Acha umbea aiseee, maisha ya watu yanakuhusu niniiii??

Sent from my TECNO H6 using JamiiForums mobile app
 
Hata kama tunakula vinono... si tunakula kwa jasho letu. Watoto wasubiri wakiwa wakubwa nao watafaidi...
Mtoto anajengwa akiwa mdogo mkuu

Sent from my SM-T800 using JamiiForums mobile app
 
Naunga mkono hoja,

Vitu vingine unaweza kuchukulia kawaida.

ila ndugu zangu mlio na familia badirikeni, unakutana na jamaa Hotelini asubuhi anapiga supu ya kuku na vyapati safi wakati familia yake home wanapiga chai ya rangi na vipande vya mihogo, mchana anapiga lunch matata sana wakati familia yake inakula ugali na matembele, usiku yupo bar anatoa ofa kwa wanawake wasioeleweka wakati home mke wake ana khanga moja imepauka watoto wanashindia vibukta vimetoboka hatari, mtu hataki hata siku moja kutoka out na mkewe maana kamchakaza mkewe anaishia kuhonga kwa michepuko.

Mlio kwenye ndoa muda wa kubadirika sasa.

Ndiyo maana wanapata laana za watoto wanazeeka vibaya

Sent from my SM-T800 using JamiiForums mobile app
 
Mi huwa nachukizwa na hii tabia mbaya ya kujumuisha kundi zima kwa makosa ya mabwege wachache,unaposema wanaume tuna tabia mbaya unamjumlisha hadi babaako,wajomba,mababu na wanaume wengine wote hata wasio na tabia ulizozitaja,

Say no to generalisation
 
Naunga mkono hoja,

Vitu vingine unaweza kuchukulia kawaida.

ila ndugu zangu mlio na familia badirikeni, unakutana na jamaa Hotelini asubuhi anapiga supu ya kuku na vyapati safi wakati familia yake home wanapiga chai ya rangi na vipande vya mihogo, mchana anapiga lunch matata sana wakati familia yake inakula ugali na matembele, usiku yupo bar anatoa ofa kwa wanawake wasioeleweka wakati home mke wake ana khanga moja imepauka watoto wanashindia vibukta vimetoboka hatari, mtu hataki hata siku moja kutoka out na mkewe maana kamchakaza mkewe anaishia kuhonga kwa michepuko.

Mlio kwenye ndoa muda wa kubadirika sasa.

Waambie hao wabadilike
 
Back
Top Bottom