hili jambo mi naliona hivi
1. Tabia za vijana wa kike na kiume kabla ya ndoa
Siku hizi ni kama vile malezi muhimu kwa watoto kutoka kwa wazazi na jamii inayowazunguka yamepungua kwa wengi. Pia hata baada ya kuvunja ungo/kubalehe hakuna mafunzo ya kimaandalizi ya kujenga tabia njema ambazo ndizo zinahitajika kwa mume/mke wakati ukifika.
Binti akikua huku hapendi kazi za mikono, hafatilii mama anavyolea watoto, hafatilii namna mama anavyoendesha familia akiwa kama mtendaji mkuu, mvivu, anapenda movies tu, anapenda kununa na kuzirazira. Hata akishafikia wakati wa kuwa tayari kuolewa mara nyingi hizi tabia atakuwa nazo. Anaweza kuzificha kwa muda tu lakini muda si mrefu huzionyesha.
Hata vijana wa kiume, wakikua huku wakiwa na dharau kwa dada zao, hawajitumi kwa kazi za nyumbani kama kuweka mazingira safi, hawapendi kujifunza namna baba anavyosimamia miradi, wanakaa vijiweni tu, wanatongoza wasichana tu na kujiingiza kwenye mapenzi ya kilaghai.
Hata wakishakuwa wakubwa katika muda wa kuoa tegemea hawawezi kuwa waume ambao mabinti watawataka, ila wanaweza jificha kwa muda lakini tabia zitajitokeza tu.
Kwa hiyo tunachokiona leo hii kuhusu mahusiano mengi kutofikia ndoa na watu kusema hawaendani ni sawa na kusema siku hizi watu hawana tabia na mienendo mizuri.
2. Utaratibu wa kuoana
Utaratibu wenye tija ni unaoanzia urafiki, uchumba halafu ndoa.
Kipindi cha urafiki kunakuwa na mawasiliano na mazungumzo ya kawaida kabisa. Au ni watu wanaoonana mara kwa mara sokoni, chuo, kanisani, mtandaoni etc. Wakati huu ni mzuri kwa kumfuatilia mtu tabia zake halisi kwa kuwa ni rahisi kujua na yeye si rahisi kuzificha.
~Uchumba
Hapa inahusisha makubaliano ya awali kati ya binti na kijana wa kiume. Baada ya wao kuelewana na kukubaliana huanza safari ya uchumba. Uchumba rasmi hufikiwa kwa kupeleka posa na kuanza taratibu za ndoa kifamilia.
NB: HAPA SI MAHALI PA KUFANYA TENDO LA NDOA.
Madhara yake ni makubwa. Ndiyo sababu ya wanaume wengi kutokuoa haraka, kama anapata tendo kuna haraka gani ya kuoa? Pili ikitokea mkaachana uchumba na mmeshafanya tendo hiyo huhesabika kwamba mlishaungana kimwili kwa kufanya kwenu tendo. Wengine huona wamechezewa na wanaweza kuchezewa na watu wengi sana. Wadada wengi waliotulia hujikuta wanakuwa malaya kwa kudanganywa na wanaume kwa kisingizio cha nitakuoa. Pia mimba zinaingia sana na kutolewa sana kama tendo litafanyika hapa.
~Ndoa
Hapa mara nyingi ni kukamilisha maelewano yenu mbele ya mashahidi na kupata cheti cha ndoa cha serikali.
Hapa tendo la ndoa ni kiunganishi kikuu.
Hapa kila mtu ni mmiliki halali wa mwenzake.
Hatakiwi mtu mwingine kuwaingilia wala wanandoa hawatakiwi kutoka nje.