hekimanyingi
JF-Expert Member
- Jul 12, 2013
- 679
- 573
Kwa sababu kuwa muda mrefu kunamfanya mtu kumfahamu mpenzi wake kwa undani hivyo ni rahisi kugundua yale madhaifu na mema ya mpenzi wake. Haina maana kuwa kwenye uhusiano wa muda mrefu kunamfanya mtu aoe au kuolewa. Mahusiano ya muda mrefu yanasaidia kufahamiana zaidi ila haitoi uhakika wa ndoa ya kudumu. Japo inategemea mahusiano yapo vipi maana watu wanaweza kuwa na uhusiano wa muda mrefu lakini hawana mpango thabiti na mikakati ya baadaye. Kwa mfano; mipango ya kutambulishana, idadi ya watoto, imani ya dini, taratibu za kitamaduni na kadhalika. Mambo kama usaliti na hasira yanaweza kupelekea mahusiano yakafutika hata kama yalikuwa na mpango au yamedumu. Cha msingi ni kuomba Mungu na kuridhiana kwa uthabiti kabisa na kumjengea mazingira mpenzi wako kwamba upamoja wenu ni wa kudumu si wa muda bila kusahau kutumia gharama ya muda, mali na hali.Hakuna mahusiano yasiyo na gharama. Vinginevyo utalalamika kuachwa au kuacha kumbe weye huvumiliki.Ivi ni kweli kwamba wanaume wengi hawawaoi wapenzi wao wa mda mrefu?
Na matokeo yake kuwaacha na kuoa msichana mwingine
Na sababu huwa ni nini?