Wanaume, kuleni hili tunda!

Wanaume, kuleni hili tunda!

Deal done.
Karibuni wadau, nimeyapanda kama maua mbele ya nyumba na shambani nimeweka kama tamati ya shamba langu na jirani.

Niliwahi shambani kwenda kuyaondoa yote msije vamia, kwa sasa nauza kwa dose, karibuni.
 
Wanawake tukitumia inakuwaje? Mimi nimeyala sana enzi hizo nikiwa mdogo mdogo. Tulikuwa tunayaita 'mafurahishaa". Hivyo vimiba vyake vikikuingia ni kero , unawashwa sana.
Sikuona madhara
Haha ! Hujamalizia yalikuwa yanaitwa mafurahisha nini?
 
Tabora enzi za udogo mafurahisha tulikuwa tunayapiga kwa majani ya matawi kuondoa vimiiba vyake.
Sijui kwanini yanaitwa mafurahisha, inawezekana kuna kaukweli ndani yake.
Vile vimiba vilikuwa nuksi, vikiingia kwenye sweta kama la shule utashinda unafurahishwa siku nzima.
Sisi tulikuwa tunafuta na udongo.
 
Nakumbuka tukiwa wadogo walikuwa wanasema ukiyala hayo matunda basi hicho ambacho umeshindwa kukimalizia kilikuwa kinaanza kucheza cheza. Kwa wewe uliyewahi kuyala, madai hayo ni ya kweli ?
Nimecheka!!!!!!!.
Wewe haukuyala? Kwa kweli hicho kipindi nayala sikumbuki hama ' nilichoshindwa kuandika ' kilipata mabadiliko au furaha yoyote.

Ila OP amesema kwa wanaume tuu ndio mnafurahiswa. Vipi wewe ulivyokula?
 
Hilo jina najiuliza nani aliyapa jina hilo hayo matunda na kwanini aliyapa jina hilo maana hata kwetu Iringa tulikuwa tunayaita hivyo, mafurahisha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimecheka!!!!!!!.
Wewe haukuyala? Kwa kweli hicho kipindi nayala sikumbuki hama ' nilichoshindwa kuandika ' kilipata mabadiliko au furaha yoyote.

Ila OP amesema kwa wanaume tuu ndio mnafurahiswa. Vipi wewe ulivyokula?
Japo nilikuwa nikiyaona kila siku nikiwa mdogo, Ila sina kumbukumbu ya kuwahi kuyala. Ninachokimbuka ni hiyo "Tabia yake" ambayo ilimbatanishwa kwenye jina lake.

Haha ! Mleta uzi kasema wale wanaume tu waliopo kwenye ndoa. Bahati mbaya zaidi sipo kwenye ndoa. Nikiwa kwenye ndoa ntakuja na mrejesho haha kama kweli yanaleta furaha haha !
 
Mimi kipind nakuwa yalikuwepo nayaona ila hatukujua kama yanaliwa sikuwah kuona mtoto yeyote anatumia mtaan kwetu
Asee mimi ndio kwaaanza nimejua humu jamiiforum kwamba haya makitu yanaliwa, hata hivyo bado naona kama sumu vileee...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom