Wanaume acheni kupiga wake zenu

Wanaume acheni kupiga wake zenu

Tangu nazaliwa huu mwaka wangu wa 50 wa kuzaliwa, sijawahi kuona Mama yangu Mzazi anapigwa na Baba yangu Mzazi...

Tangu naolewa huu NI mwaka wangu wa ndoa Miaka 30 sijawahi KUMWONA MUME WANGU ananipiga labda kama ananipiga mechi (dyudyu)

Hivi kwani sikuhizi vijana wamekuwaje? Mbona vijana Mnapiga wake zenu shida Nene?

Nipo na dadangu hapa ananiambia sijui Mwimbaji Martha Mwaipaja ameachana na mumewe kisa Amepigwa

Na mumewe anajiita Nabii

Sa mbona watumishi wa Mungu mnatuchanganya lakini

Ila sio mbaya maana Yesu alisema siku ya mwisho kutakuwa na Manabii wa Uongo!

Alafu kuna kasheria kamepita kanasema mwanamke ukipigwa mumeo anafungwa so watoto wangu muwe na akili ya kukimbilia kwenye dola mkipigwa

Jamaani wadogozangu wanaume naombeni msipige wake zenu mkioa plz...

WANAUME ACHENI KUPIGA WAKE ZENU.

Wanawake nao wajiangalie majibu wanaotujibu hayafai, mfano unambamba na text za jamaa kamtumia za mapenzi ukihoji unajibiwa hovyo, au anaenda maeneo ambayo huyafahamu na hakuagi na akirudi ukimuuliza anakaa kimya huo ububu lazima kichapo kitembee.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanawake nao wajiangalie majibu wanaotujibu hayafai, mfano unambamba na text za jamaa kamtumia za mapenzi ukihoji unajibiwa hovyo, au anaenda maeneo ambayo huyafahamu na hakuagi na akirudi ukimuuliza anakaa kimya huo ububu lazima kichapo kitembee.

Sent using Jamii Forums mobile app
Inategemea umemuulizaje ulipomfuma
Ungemwuliza mpenzi huyu nani tena anataka kututenganisha wakati Dini imesema NI kifo tuvkisitutenganishe

Ungeona anacheka anakujibu vizuri
Tatizo unaleta uafande na udikteta kwenye penzi unategemea nini?
Mwanamke hapigwi wala hafokewi
 
doh Mungu anakuooona!
Mungu alikupa mikono utalime ardhi na kumlinda mke na watoto wako vita ikija sio kupiga mwanamke
Hayo ni majukumu yetu. Ila ukiwa na mdomo provocative lazma uguswe kidogo urudi kwenye mstari.

Utakubaliana nami kuwa unapokutana na kofi lisilojulikana hata wewe mwenyewe lazima utakaa ujiulize imekuaje kuaje na mwishowe hekima inatumika badala ya hisia.

Sent using Boeing 737-MAX 8
 
Ndio nasema hv, huwezi kuishi ndani ya ndoa kwa taratibu za kwenu jinsi wazazi wako walivyokulea kisa una miaka 32+.
Kumuelewa mwenzio anapenda nini na hapendi nini?.. Wewe pia... Sio umri wako uwe kinga ya kutoelekezana..(never)
Mfano: sitaki urudi home usiku lakn wewe unakaidi kisa nimekukuta umeota nywele siwezi kukupangia... Kweli? Hii ndoa au disco vumbi?
Hili jambo huwa hawalielewi. Wanapenda kuleta "lifestyle" walizotoka nazo kwa wazazi ndani ya ndoa!

Sent using Boeing 737-MAX 8
 
Back
Top Bottom