Wanasheria wetu! Tumaini jipya?

Wanasheria wetu! Tumaini jipya?

Miaka ile ya 2000 wakati wa Gen P. Musharaf wa Pakistan, vyama vingine vyote vya siasa vikiwa vimebanwa mbavu na kuminywa hasa.... Likatokea jambo la nadra sana, sikumbuki vizuri ilikuwaje lakini nakumbuka wanasheria walichokonolewa wakachokozwa
Hawakukubali wakaandaa maandamo ya amani kuelekea Islamabad mji mkuu wa Pakistan, maandamano hayo yalitokea miji mingine mikuu kama Peshawar, Lahore na Karachi
Nakumbuka wiki ya maandalizi ya yale maandamano wanasheria walitishwa sana... Lakini wakashikilia msimamo wao wa kuandamana kwa amani.... Na hatimaye wakaandamana.......
Huku kwetu kuna kila dalili ya yale ya Pakistan kujirudia.... Ni wazi na sio siri vyama vya siasa vile vyenye nguvu vimebanwa kila kona na vinafanyiwa hujuma zisizoisha kila uchao, viongozi wanakatishwa tamaa kwa malundo ya kesi, hujuma ni nyingi mno na kesi pia ni nyingi.... Ni mkakati maalum uliosukwa kwa ufundi kudhoofisha na hatimaye kuua kabisa vyama makini vya upinzani
Lakini siku zote penye nia pana njia! Wote tunajua hofu waliyokuwa nayo watawala kwa Lisu kuchaguliwa kuwa rais wa chama cha wanasheria Tanganyika! Tulishuhudia vibweka vya kila aina.... Wanasheria wakagoma kuburuzwa, wakagoma kupangiwa wakagoma kupelekeshwa! Na kubwa kuliko yote wakagoma KUNUNULIWA.....
Mshikamano wao wakati ule wa uchaguzi likikuwa jambo geni, wengi walidhani baada ya pale wataachana njiapanda.... HAWAKUFANYA HIVYO..... kauli yao imekuwa SOLIDARITY FOREVER!
Mambo ya nadra yameendelea kutokea kwenye kaliba hii ya wasomi wanataaluma mahiri.... Tumeshuhudia kwenye kesi ya Lisu, tumeshuhudia kwenye kesi ya mwanamama machachari Bi Fatma Karume.... kuna bonding ya aina yake kwa hii kaliba ya sheria... Mamlaka hazipedi kabisa hili jambo lakini pengine ndio ule wakati umetimia sasa..... A long way to freedom

Sent using Jamii Forums mobile app
we bora uendelee na mada zako za kichawi na kiganga huku naona bado ni mweupe kabisa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uko sahihi kabisa kiongozi. Sheikh Ponda kapata misukosuko mahakamani, hakuna mwanasheria anaezumgumzia hilo, hofu sasa inakuwaje mzee huyu kama hana uwezo wa kumlipa wakili? Au kwa hawa wanasheria Sheikh Ponda si raia na hastahili huduma? kama ni hivyo ingefaa wangeweka vigezo vyao vya kumtetea mtu.
TLS miaka mingi imekwa na sifa nzuri, zaidi ya miaka 50. Juzi imepata raisi wake mpya na katika hotuba yake ya kwanza baada ya kuchaguliwa alihutubia siasa badala ya kuhutubia masuala ya TLS. alisema wazi raisi na serikali kwa ujumla wanaingilia TLS kisa yeye kagombea, na akadiriki kuihusisha TLS na CHADEMA.
Ni aibu sana.
Wanajiharibia sifa ktk jamii, kitawahudumia wana Cdm tu, na hapo kitatokea kitu, anguko la Cdm litakuwa ni anguko la TLS pia. Kubwa zaidi, utatokea mpasuko chamani, watagawanyika, wenye mrengo wa cdm, wenye mrengo kinyume na cdm na wale wenye kuithamini taaluma yao na waitakayo iwe kitaaluma tu. We macho walione mapema hili.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanajiharibia sifa ktk jamii, kitawahudumia wana Cdm tu, na hapo kitatokea kitu, anguko la Cdm litakuwa ni anguko la TLS pia. Kubwa zaidi, utatokea mpasuko chamani, watagawanyika, wenye mrengo wa cdm, wenye mrengo kinyume na cdm na wale wenye kuithamini taaluma yao na waitakayo iwe kitaaluma tu. We macho walione mapema hili.

Sent using Jamii Forums mobile app
Na CHADEMA iangalie sana hawa wasomi. Wasomi wakishaingia kwenye chama kama chadema na wakaingiza usomi wao, hakika Chadema hakitasimama imara.
 
Kwann uundiwe?lengo ni nn kama c kufuata yale atakaye aliyekuundia?



Sent using Jamii Forums mobile app

Kuna bodi ya wahandisi
Kuna bodi ya wahasibu
Kwanini isiwepo bodi ya wanasheria?. Wanasheria wanacho kipi special ambacho hao wanataaluma wengine hawana?.

Tanzania inachelewa kupata maendeleo kwa sababu ya kutegemea kupata kitu kipya kupitia njia zile zile za zamani.
 
poa ninapambana na hali yangu.
Sio hali yako hali ya watanzania wote
Kuna bodi ya wahandisi
Kuna bodi ya wahasibu
Kwanini isiwepo bodi ya wanasheria?. Wanasheria wanacho kipi special ambacho hao wanataaluma wengine hawana?.

Tanzania inachelewa kupata maendeleo kwa sababu ya kutegemea kupata kitu kipya kupitia njia zile zile za zamani.
Kweni hicho walichonacho kina LISU ni nn?tena kinawigo mpana sana na ndo maana kuna wanatamani kifutwe .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sio hali yako hali ya watanzania wote

Kweni hicho walichonacho kina LISU ni nn?tena kinawigo mpana sana na ndo maana kuna wanatamani kifutwe .

Sent using Jamii Forums mobile app
Hiyo TLS ni kama saccos fulani, ni chombo kilichoundwa enzi ya mkoloni. Hakifanani na mahitaji ya karne ya sasa.

Wanasheria kama walivyo wataalam wengine, wanahitaji kuwa chini ya chombo kitakachosimamia (regulatory body) uendeshaji wa shughuli zao kitaalam. Ndivyo dunia yenye maendeleo inavyoendesha shughuli zake.
 
Hiyo TLS ni kama saccos fulani, ni chombo kilichoundwa enzi ya mkoloni. Hakifanani na mahitaji ya karne ya sasa.

Wanasheria kama walivyo wataalam wengine, wanahitaji kuwa chini ya chombo kitakachosimamia (regulatory body) uendeshaji wa shughuli zao kitaalam. Ndivyo dunia yenye maendeleo inavyoendesha shughuli zake.
Siku zote najua una mawazo ya kichovu , lakini sikudhani kama una mawazo ya kishamba kiasi hiki !
 
Siku zote najua una mawazo ya kichovu , lakini sikudhani kama una mawazo ya kishamba kiasi hiki !
Wewe ambaye ni bendera hufuata upepo ndio mshamba kwa sababu kila kitu unakitazama katika mtazamo wa mwanaharakati wa leo badala ya kutazama mambo katika mtazamo wa miaka 10 au 20 au 40 ijayo.
 
Asante kwa kutukubali. Fahamu kuwa tasnia yetu hairandani na porojo,utapeli na propaganda. Ni mambo ya kifungu kwa kifungu;hoja kwa hoja. Mambo yako mahakamani mkuu!

I wish mngeamka mapema zaidi naona mmechelewa sana.
 
Hiyo TLS ni kama saccos fulani, ni chombo kilichoundwa enzi ya mkoloni. Hakifanani na mahitaji ya karne ya sasa.

Wanasheria kama walivyo wataalam wengine, wanahitaji kuwa chini ya chombo kitakachosimamia (regulatory body) uendeshaji wa shughuli zao kitaalam. Ndivyo dunia yenye maendeleo inavyoendesha shughuli zake.

wewe. nakuomba ufahamu kuwa. mawakili ni tofauti na sekta zingine kama wahandisi na wahasibu. wanasheria is about human right. na mwenye mamlaka makumbwa anayeweza kukandamiza haki za binadamu ni serikali. sasa haiwezekani itengenezwe board inayoendeshwa na serikali kuwashugulikia wanasheria ambao kiukweri wanatetea watu against na serikali agency ambayo ni mahakama. jiulize sasa wanasiasa wengi, wafanyabiashara wengi wanashikwa na kupelekwa mahakamani. je kama ndiyo na mawakili ataongozwa na board inayomilikiwa na serikali itakuwaje kuwatetea watu waliopelekwa na serikali mahakamani?. kumbuka tuna mihimili mitatu. mahakama, bunge na serikali. na hadi sasa kwa yeyote mwenye uwezo wa kuona vizuri mihimili hiyo haipo sawa kwani ipo mfukoni mwa mkulu. lolote akiamua linatekelezwa. nafikri siku ya mahakama mkulu aliagazi kesi za madai zishugulikiwe haraka ili serikali ipate pesa pia ulisikia habari ya wabunge upinzani bungeni washugulikiwe ili wasiwe na kinga ili wakija huku nae awashugulikie. sasa nakuuliza wanasheria au mawakili wakiwa chini ya board ya serikali itakuwaje?. kunauhuru wa kutoa mawazo but kwa wazo lako hili unasitaili kunyongwa wewe.
 
Wanajiharibia sifa ktk jamii, kitawahudumia wana Cdm tu, na hapo kitatokea kitu, anguko la Cdm litakuwa ni anguko la TLS pia. Kubwa zaidi, utatokea mpasuko chamani, watagawanyika, wenye mrengo wa cdm, wenye mrengo kinyume na cdm na wale wenye kuithamini taaluma yao na waitakayo iwe kitaaluma tu. We macho walione mapema hili.

Sent using Jamii Forums mobile app
TLS is combated by government politically that is why tls also must react politically. pond is ttached kiitikadi hivyo na yeye anatakiwa kureact kiitikadi pia. this is the war about separation of power. siyo kila kitu kwenye mfuko wa mkulu
 
Na CHADEMA iangalie sana hawa wasomi. Wasomi wakishaingia kwenye chama kama chadema na wakaingiza usomi wao, hakika Chadema hakitasimama imara.
chd tiari imekufa. kwa sasa inafufuka kwa sitail mpya na itakuwa na nguvu zaidi naomba nikudokeze hata uongozi unaouona kwa sasa wa cdm utapotea and new leader utakakuja na ile hali ya ukanda itapotea siasa za sasa siyo za kushikana mkono kuwa huyu mtoto wa dada au shemeji. siasa za sasa ni je unaweza himili mishindo?. wale watakaoweza kuimalika katika hiki kipindi cha mkulu ndiyo next political leader. na wale wote unaowaona wanasema ndiyo mkulu ndiyo watapotea na mkulu baada ya kuondoka madalakani. kumbuka sasa siasa za upinzani zinabadilika kutoka kwenye hoja ya ufisadi kwenda kwenye hoja za separation of power na hiki ndicho mkulu tutamkumba nacho sana kwa sabahu umuhimu wa mihimili mitatu unaonekana unahitajika sana sasa kuliko awamu zote zilizoita kutokana na sera zake zakuongoza.
 
Mpare kaacha kazi ya uganga na ramli sasa anatabiri kwenye politiki...hao unaowasifia ni vibaraka wa watu kama wewe ulivyo wewe kwa hao unaowasifia, wanasheria wenyewe Lissu asiyetaka kutumia akili, aliye na mihemko, hapana mpare panda kule milimani kawahamasishe wenzio wafanye kazi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tasnia ya sheria tayari imeingiliwa na siasa. Inshu ya Pakistani ni ya kipekee kabisa. Musharaf alifukuza wanasheria (majaji) katika utumishi wa umma na ndio ikawa chanzo cha maandamano, migomo na machafuko. Kwa hapa tz mambo ni tofauti. Siasa zinalazimishwa ziingie katika sheria. TLS nayo inalazimishwa iwe ya kisiasa pasipo kuzingatia kwamba ndani ya TLS kila kitu kinaenda kwa utaratibu wake kikanuni.
Siasa zimefanya baadhi ya wanasheria wawe na kiburi, wanavimba vichwa kwa sababu wana wafuasi wa kisiasa. Wanalazimisha walete siasa hadi kwenye masuala ya sheria.
Ifikie hatua umma ufahamu kuwa hakuna siasa mahakamani. Mpinzani au mfuasi wa chama cha upinzani akishindwa kesi wanasema mahakimu au majaji wamenunuliwa, wakishinda wanatamba kuwa mahakama ni mkombozi wao. Mahakama ikishaingiliwa kisiasa hatutakuwa tena na uhuru wa mahakama. siasa ya namna yeyote ile au ya kutoka kwa yeyote yule, ikiwa ni pamoja na umma, ni hatari sana kwa uhuru wa mahakama.
Tasnia ya sheria ibaki kuwa taaluma. Sheria ikihusishwa ma masuala ya siasa hakika taifa litaangukia pabaya.
Absolutely true, TLS ndio ilikua kimbilio la wanyonge lkn sasa ishaakua kama chama cha siasa, kwa hali ilivyo ukienda TLS ukiwa mfuasi wa chama fulan huwez pata msaada alaf inakuaje iitwe chama cha wanataaluma

Sent using Jamii Forums mobile app
 
wewe. nakuomba ufahamu kuwa. mawakili ni tofauti na sekta zingine kama wahandisi na wahasibu. wanasheria is about human right. na mwenye mamlaka makumbwa anayeweza kukandamiza haki za binadamu ni serikali. sasa haiwezekani itengenezwe board inayoendeshwa na serikali kuwashugulikia wanasheria ambao kiukweri wanatetea watu against na serikali agency ambayo ni mahakama. jiulize sasa wanasiasa wengi, wafanyabiashara wengi wanashikwa na kupelekwa mahakamani. je kama ndiyo na mawakili ataongozwa na board inayomilikiwa na serikali itakuwaje kuwatetea watu waliopelekwa na serikali mahakamani?. kumbuka tuna mihimili mitatu. mahakama, bunge na serikali. na hadi sasa kwa yeyote mwenye uwezo wa kuona vizuri mihimili hiyo haipo sawa kwani ipo mfukoni mwa mkulu. lolote akiamua linatekelezwa. nafikri siku ya mahakama mkulu aliagazi kesi za madai zishugulikiwe haraka ili serikali ipate pesa pia ulisikia habari ya wabunge upinzani bungeni washugulikiwe ili wasiwe na kinga ili wakija huku nae awashugulikie. sasa nakuuliza wanasheria au mawakili wakiwa chini ya board ya serikali itakuwaje?. kunauhuru wa kutoa mawazo but kwa wazo lako hili unasitaili kunyongwa wewe.
Umeongea vitu vya msingi na hii ni changamoto ya kimfumo kikatiba, hapa unajadili mamlaka ya Rais kuwa jaji na pia kuwa mbunge kikatiba, mada haiko huko. Nadhani mada si board iliyotaka kuundwa, bali utendaji wa kisiasa wa TLS, tunahoji Tls ni tawi la chama cha kisiasa ama haki pekee inayozisimamia ni haki za kisiasa?

Hapo tu, kiufupi, wenye hekima wanahisi TLS inamezwa na cdm hivyo ikapoteza muelekeo wake wa kusimamia haki za jamii, kisiasa, kiuchumi, na kijamii. Wanafunzi wamekatwa asilimia 15 ya mikopo kinyume na mikataba, nyongeza za mishahara (haki za mtumishi) hazipo, manyanyaso mengi ktk jamii yote madogo, Lisu mchochezi mawakili kibao az if mwenyewe asingeweza kuisaidia mahakama kutenda haki, huyu naye kaguswa tena kwa nia njema ya utekelezaji wa majukumu ya kazi, mawakili 30. Hapo tu ndo penye shida.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umeongea vitu vya msingi na hii ni changamoto ya kimfumo kikatiba, hapa unajadili mamlaka ya Rais kuwa jaji na pia kuwa mbunge kikatiba, mada haiko huko. Nadhani mada si board iliyotaka kuundwa, bali utendaji wa kisiasa wa TLS, tunahoji Tls ni tawi la chama cha kisiasa ama haki pekee inayozisimamia ni haki za kisiasa?

Hapo tu, kiufupi, wenye hekima wanahisi TLS inamezwa na cdm hivyo ikapoteza muelekeo wake wa kusimamia haki za jamii, kisiasa, kiuchumi, na kijamii. Wanafunzi wamekatwa asilimia 15 ya mikopo kinyume na mikataba, nyongeza za mishahara (haki za mtumishi) hazipo, manyanyaso mengi ktk jamii yote madogo, Lisu mchochezi mawakili kibao az if mwenyewe asingeweza kuisaidia mahakama kutenda haki, huyu naye kaguswa tena kwa nia njema ya utekelezaji wa majukumu ya kazi, mawakili 30. Hapo tu ndo penye shida.

Sent using Jamii Forums mobile app
saw nakuelewa. but nikukumbushe kuwa huwezi kuwatetea watu wakati wewe uhatalini kupotezwa. mawakili sasa wanatapata kujinasua na swala la kuwekwa mfukoni mwa mkulu. sasa wote wamevulungwa na lissu kama amejitoa kimasomaso. hivyo kisa cha lissu ndiyo vuguvugu lilipoanzia. nafikri tunapaswa tutulie kwanza ikifika mawakili wajinasua kwenye mikono ya mkuu ndiyo wataweza kufanya na mengine makuu ya kuijulisha serikali kuwa mamlaka yao hayaamanishi kutenda wanavyotaka kwa kuwa wanadola.
 
wewe. nakuomba ufahamu kuwa. mawakili ni tofauti na sekta zingine kama wahandisi na wahasibu. wanasheria is about human right. na mwenye mamlaka makumbwa anayeweza kukandamiza haki za binadamu ni serikali. sasa haiwezekani itengenezwe board inayoendeshwa na serikali kuwashugulikia wanasheria ambao kiukweri wanatetea watu against na serikali agency ambayo ni mahakama. jiulize sasa wanasiasa wengi, wafanyabiashara wengi wanashikwa na kupelekwa mahakamani. je kama ndiyo na mawakili ataongozwa na board inayomilikiwa na serikali itakuwaje kuwatetea watu waliopelekwa na serikali mahakamani?. kumbuka tuna mihimili mitatu. mahakama, bunge na serikali. na hadi sasa kwa yeyote mwenye uwezo wa kuona vizuri mihimili hiyo haipo sawa kwani ipo mfukoni mwa mkulu. lolote akiamua linatekelezwa. nafikri siku ya mahakama mkulu aliagazi kesi za madai zishugulikiwe haraka ili serikali ipate pesa pia ulisikia habari ya wabunge upinzani bungeni washugulikiwe ili wasiwe na kinga ili wakija huku nae awashugulikie. sasa nakuuliza wanasheria au mawakili wakiwa chini ya board ya serikali itakuwaje?. kunauhuru wa kutoa mawazo but kwa wazo lako hili unasitaili kunyongwa wewe.
Umeandika mengi lakini yameongozwa na intellectual pride.

Hizo fani nyingine na zenyewe hazina umuhimu kama walionao wanasheria?.

TLS iliundwa wakati wa mkoloni, mahitaji ya mwanasheria wakati ule sio ya leo hii.

Kuwepo kwa bodi ya wanasheria hakumaanishi kwamba maslahi ya wanasheria yatashindwa kutimizwa kwa kigezo cha maslahi ya wenye kuongoza nchi. Wanasheria hawawezi kukwepa kuwa na regulatory body katika nyakati hizi.

Lipo ombwe ambalo kwa uwepo wake, mambo mengi muhimu yanaweza kushindwa kufanyika kwa faida ya wanasheria wenyewe.

Tatizo naloliona ni wanasheria wenyewe kuingiziwa mindsets za uanaharakati na taasisi nyingine.

Kumbuka kuwa wanasheria na wenyewe kwa muda mrefu wamekuwa ni sehemu ya mfumo mbovu ndani ya mfumo unaopaswa kuwa msafi mbele ya jamii. Wamekuwa sehemu ya corrupt culture ambayo imekuwa ikiisumbua Tanzania tangu enzi za awamu ya pili mpaka leo.
 
Back
Top Bottom