Tasnia ya sheria tayari imeingiliwa na siasa. Inshu ya Pakistani ni ya kipekee kabisa. Musharaf alifukuza wanasheria (majaji) katika utumishi wa umma na ndio ikawa chanzo cha maandamano, migomo na machafuko. Kwa hapa tz mambo ni tofauti. Siasa zinalazimishwa ziingie katika sheria. TLS nayo inalazimishwa iwe ya kisiasa pasipo kuzingatia kwamba ndani ya TLS kila kitu kinaenda kwa utaratibu wake kikanuni.
Siasa zimefanya baadhi ya wanasheria wawe na kiburi, wanavimba vichwa kwa sababu wana wafuasi wa kisiasa. Wanalazimisha walete siasa hadi kwenye masuala ya sheria.
Ifikie hatua umma ufahamu kuwa hakuna siasa mahakamani. Mpinzani au mfuasi wa chama cha upinzani akishindwa kesi wanasema mahakimu au majaji wamenunuliwa, wakishinda wanatamba kuwa mahakama ni mkombozi wao. Mahakama ikishaingiliwa kisiasa hatutakuwa tena na uhuru wa mahakama. siasa ya namna yeyote ile au ya kutoka kwa yeyote yule, ikiwa ni pamoja na umma, ni hatari sana kwa uhuru wa mahakama.
Tasnia ya sheria ibaki kuwa taaluma. Sheria ikihusishwa ma masuala ya siasa hakika taifa litaangukia pabaya.